< 1 Wathesalonike 2 >
1 Ndugu zangu, kwa kuwa ninyi wenyewe mnajua ya kwamba kuja kwetu kwenu hakukuwa bure,
For ye yourselves know, brethren, that our coming among you hath not been in vain;
2 kama vile mjuavyo, tulikuwa tumeteswa na kutukanwa huko Filipi, lakini hata hivyo, kwa msaada wa Mungu wetu, tulikuwa na ujasiri wa kuwaambia Injili ya Mungu ingawa kulikuwa na upinzani mkubwa.
but after we had suffered before and had been shamefully treated, as ye know, at Philippi, we were bold in our God to speak to you the gospel of God in much conflict.
3 Kwa maana himizo letu halikutokana na hila wala nia mbaya au udanganyifu.
For our teaching is not from error, nor from impurity, nor in guile;
4 Kinyume chake, tulinena kama watu tuliokubaliwa na Mungu tukakabidhiwa Injili. Sisi hatujaribu kuwapendeza wanadamu bali kumpendeza Mungu, yeye ayachunguzaye mawazo ya ndani sana ya mioyo yetu.
but as we have been regarded by God as worthy to be intrusted with the gospel, so we speak, not as pleasing men, but God, who trieth our hearts.
5 Kama mjuavyo, hatukuja kwenu kwa maneno ya kujipendekeza au maneno yasiyo ya kweli ili kuficha tamaa mbaya: Mungu ndiye shahidi yetu.
For neither at any time did we use flattering words, as ye know, nor a cloak of covetousness, God is witness;
6 Wala hatukuwa tunatafuta sifa kutoka kwa wanadamu, wala kutoka kwenu au kwa mtu mwingine awaye yote. Kama mitume wa Kristo tungaliweza kuwa mzigo kwenu,
nor from men sought we glory, either from you, or from others; though we might have used authority as apostles of Christ.
7 lakini tulikuwa wapole katikati yenu, kama mama anayewatunza watoto wake wadogo.
But we were gentle in the midst of you, even as a nurse cherisheth her own children;
8 Tuliwapenda sana kiasi kwamba tulifurahia kushirikiana nanyi, si Injili ya Mungu tu, bali hata maisha yetu, kwa sababu mlikuwa wa thamani mno kwetu.
so having a strong affection for you, we were willing to impart to you, not only the gospel of God, but also our own souls, because ye became dear to us.
9 Ndugu zetu, mnakumbuka juhudi yetu na taabu yetu. Tulifanya kazi usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote wa kwenu wakati tulipokuwa tunawahubiria Injili ya Mungu.
For ye remember, brethren, our labor and toil, how laboring night and day, that we might not be burdensome to any of you, we preached to you the gospel of God.
10 Ninyi wenyewe ni mashahidi na Mungu pia, jinsi tulivyokuwa watakatifu, wenye haki na wasio na lawama miongoni mwenu ninyi mlioamini.
Ye are witnesses, and so is God, how holily, and righteously, and unblamably we conducted ourselves toward you that believe;
11 Maana mnajua kwamba tuliwatendea kila mmoja wenu kama vile baba awatendeavyo watoto wake.
as ye know how we exhorted, and encouraged, and charged every one of you, as a father doth his children,
12 Tuliwatia moyo, tuliwafariji na kuwahimiza kuishi maisha yampendezayo Mungu, anayewaita katika Ufalme na utukufu wake.
that ye should walk in a manner worthy of God, who is calling you to his own kingdom and glory.
13 Nasi pia tunamshukuru Mungu bila kukoma kwa sababu mlipolipokea neno la Mungu mlilosikia kutoka kwetu, hamkulipokea kama neno la wanadamu, bali mlilipokea kama lilivyo hasa, neno la Mungu, litendalo kazi ndani yenu ninyi mnaoamini.
And for this cause we also thank God without ceasing, that, when ye received the word of God which ye heard from us, ye received it not as the word of men, but, as it is in truth, the word of God, which also is powerfully working in you that believe.
14 Kwa maana ninyi ndugu zetu, mlifanyika wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyoko ndani ya Kristo Yesu katika Uyahudi. Mlipata mateso yale yale kutoka kwa watu wenu wenyewe kama vile makanisa hayo yalivyoteswa na Wayahudi,
For ye, brethren, became imitators of the churches of God which are in Judaea in Christ Jesus; for ye also suffered the same things from your own countrymen, as they have from the Jews;
15 wale waliomuua Bwana Yesu na manabii, nasi wakatufukuza pia. Watu hao walimchukiza Mungu na tena ni adui wa watu wote,
who both killed the Lord Jesus, and the prophets, and drove us out, and please not God, and set themselves against all men,
16 wakijitahidi kutuzuia tusizungumze na watu wa Mataifa ili kwamba wapate kuokolewa. Kwa njia hii wanazidi kujilundikia dhambi zao hadi kikomo. Lakini hatimaye ghadhabu ya Mungu imewafikia.
hindering us from speaking to the gentiles that they may be saved, —to fill up their sins always! But the wrath is come upon them to the end.
17 Lakini ndugu zetu, tulipotenganishwa nanyi kwa kitambo kidogo (ingawa kutengana huko kulikuwa kwa mwili tu, si kwa moyo), tulizidi kuwa na shauku kubwa kuwaona uso kwa uso.
But we, brethren, having been bereaved of you for a short time, separated in body, not in heart, used the greater endeavors with much earnestness to see your face.
18 Maana tulitaka kuja kwenu, hasa mimi Paulo, nilitaka kuja tena na tena, lakini Shetani akatuzuia.
Wherefore we purposed to come to you, that is, I Paul, once and again; but Satan hindered us.
19 Kwa maana tumaini letu ni nini, au furaha yetu au taji yetu ya kujisifia mbele za Bwana Yesu Kristo wakati wa kuja kwake? Je, si ni ninyi?
For what is our hope, or joy, or crown of glorying? Is it not even ye, in the presence of our Lord Jesus at his coming?
20 Naam, ninyi ndio fahari yetu na furaha yetu.
For ye are our glory and joy.