< 1 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na amani.
Paul, Silvain et Timothée, à l'assemblée des Thessaloniciens, en Dieu le Père et le Seigneur Jésus-Christ: Grâce et paix à vous de la part de Dieu notre Père et du Seigneur Jésus-Christ.
2 Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima.
Nous rendons toujours grâces à Dieu pour vous tous, en vous mentionnant dans nos prières,
3 Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.
nous souvenant sans cesse de votre œuvre de foi, de votre travail d'amour et de votre persévérance d'espérance dans notre Seigneur Jésus-Christ, devant notre Dieu et Père.
4 Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua,
Nous savons, frères aimés de Dieu, que vous êtes des élus,
5 kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu.
et que notre Bonne Nouvelle vous est parvenue non seulement en paroles, mais aussi en puissance, et dans l'Esprit Saint et avec beaucoup d'assurance. Vous savez quelle sorte d'hommes nous nous sommes montrés au milieu de vous à cause de vous.
6 Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu.
Vous êtes devenus nos imitateurs et ceux du Seigneur, ayant reçu la parole dans une grande affliction, avec la joie de l'Esprit Saint,
7 Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya.
de sorte que vous êtes devenus un exemple pour tous ceux qui croient en Macédoine et en Achaïe.
8 Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake.
Car c'est par vous que la parole du Seigneur a été annoncée, non seulement en Macédoine et en Achaïe, mais aussi en tout lieu où votre foi en Dieu s'est répandue, de sorte que nous n'avons rien à dire.
9 Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli
Car ils rapportent eux-mêmes à notre sujet quel accueil nous avons reçu de votre part, et comment vous vous êtes convertis des idoles à Dieu pour servir un Dieu vivant et vrai,
10 na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.
et pour attendre du ciel son Fils, qu'il a ressuscité des morts: Jésus, qui nous délivre de la colère à venir.

< 1 Wathesalonike 1 >