< 1 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na amani.
Pauluselt, Siilaselt ja Timoteoselt, Tessalooniklaste kogudusele Jumalas Isas ja Issandas Jeesuses Kristuses: Armu ja rahu teile!
2 Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima.
Me täname alati Jumalat teie kõikide eest, mainides teid pidevalt oma palvetes ning
3 Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.
meelde tuletades Jumala ja meie Isa ees teie usus tehtud tööd, armastuses nähtud vaeva ja teie püsivust lootuses meie Issanda Jeesuse Kristuse peale.
4 Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua,
Me teame, Jumalast armastatud vennad ja õed, et tema on teid valinud,
5 kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu.
sest meie evangeelium ei ole teie juurde tulnud ainult sõnades, vaid ka väes ja Pühas Vaimus ning sügava veendumusega. Te ju teate, kuidas me teie juures teie heaks elasime.
6 Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu.
Te võtsite eeskujuks meid ning Issandat, kui te suurest kannatusest hoolimata sõna vastu võtsite Püha Vaimu rõõmuga.
7 Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya.
Nõnda te olete saanud eeskujuks kõigile usklikele Makedoonias ja Ahhaias.
8 Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake.
Sest teie juurest on Issanda sõna kostnud mitte ainult Makedooniasse ja Ahhaiasse, vaid teie usk Jumalasse on saanud tuntuks igal pool. Nii et meil pole vaja enam midagi rääkida,
9 Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli
sest nad ise ju räägivad, kuidas te meid vastu võtsite ning kuidas te olete ebajumalaist ära pöördunud, teenima elavat ja tõelist Jumalat
10 na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.
ning ootama taevast tema Poega Jeesust, kelle ta on surnuist üles äratanud ja kes päästab meid saabuva viha käest.

< 1 Wathesalonike 1 >