< 1 Samweli 9 >

1 Kulikuwako Mbenyamini mmoja, mtu maarufu, ambaye aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia wa Benyamini.
Or, il était un homme de la tribu de Benjamin nommé Cis, fils d’Abiel, fils de Séror, fils de Béchorath, fils d’Aphia, fils d’un homme de Jémini, courageux et robuste.
2 Alikuwa na mwana aliyeitwa Sauli, kijana anayevutia sana, hakuwepo aliyelingana naye miongoni mwa Waisraeli, alikuwa mrefu kuliko wengine wote.
Et il avait un fils du nom de Saül, distingué et bon; et il n’était pas d’homme parmi les enfants d’Israël meilleur que lui; de l’épaule et de la tête il surpassait tout le peuple.
3 Basi punda wa Kishi baba yake Sauli walipotea, naye Kishi akamwambia mwanawe Sauli, “Mchukue mmoja wa watumishi mwende pamoja naye kuwatafuta punda.”
Or les ânesses de Cis, père de Saül, s’étaient perdues; et Cis dit à Saül, son fils: Prends avec toi un des serviteurs, et, te levant, va, et cherche les ânesses. Ceux-ci ayant passé par la montagne d’Ephraïm,
4 Hivyo akapita katika nchi ya vilima ya Efraimu na katika eneo la Shalisha, lakini hawakuwapata. Wakaendelea katika sehemu ya Shaalimu, lakini punda hawakuwepo huko. Kisha wakapita katika nchi ya Benyamini, lakini hawakuwapata.
Et par la terre de Salisa, et ne les ayant point trouvées, passèrent aussi par la terre de Salim, et elles n’y étaient pas; et aussi par la terre de Jémini, et ils ne les rencontrèrent pas du tout.
5 Walipofika sehemu ya Sufu, Sauli akamwambia mtumishi aliyekuwa pamoja naye, “Njoo, sisi na turudi, au baba yangu ataacha kufikiria juu ya punda na kuanza kufadhaika kutuhusu sisi.”
Mais lorsqu’ils furent venus dans la terre de Suph, Saül dit au serviteur qui était avec lui: Viens, et retournons-nous-en, de peur que mon père n’ait laissé les ânesses, et qu’il ne soit inquiet sur nous.
6 Lakini mtumishi akajibu, “Tazama, katika mji huu yupo mtu wa Mungu, anayeheshimiwa sana na kila kitu asemacho hutokea kweli. Sasa na twende huko. Huenda atatuambia twende njia ipi.”
Le serviteur lui dit: Voilà qu’il y a un homme de Dieu dans cette ville, homme célèbre, tout ce qu’il dit arrive certainement. Maintenant donc allons là; peut-être nous renseignera-t-il sur la route, à cause de laquelle nous sommes venus.
7 Sauli akamwambia mtumishi wake, “Kama tukienda, tutampa nini huyo mtu? Chakula kimekwisha kwenye mifuko yetu. Hatuna zawadi ya kumpelekea huyo mtu wa Mungu. Je tuna nini?”
Alors Saül dit à son serviteur: Eh bien, nous irons: que porterons-nous à l’homme de Dieu? Le pain a manqué dans nos panetières, nous n’avons pas de présent pour donner à l’homme de Dieu, ni quelque autre chose que ce soit.
8 Mtumishi akamjibu Sauli tena, akasema, “Tazama, nina fedha robo shekeli. Hiyo nitampa huyo mtu wa Mungu ili aweze kutuambia twende kwa njia ipi.”
Le serviteur répondit de nouveau à Saül, et dit: Voici que se trouve dans ma main la quatrième partie d’un statère d’argent, donnons-la à l’homme de Dieu, afin qu’il nous indique notre route.
9 (Zamani katika Israeli, kama mtu alikwenda kuuliza neno kwa Mungu, angalisema, “Njoo na twende kwa mwonaji,” kwa sababu nabii wa sasa alikuwa akiitwa mwonaji.)
(Autrefois dans Israël ainsi parlaient tous ceux qui allaient consulter Dieu: Venez, et allons au voyant; car celui qui est appelé prophète aujourd’hui, se nommait autrefois voyant.)
10 Sauli akamwambia mtumishi wake, “Vyema, njoo na twende.” Basi wakaenda mjini alipokuwepo huyo mtu wa Mungu.
Alors Saül dit à son serviteur: Ta parole est excellente. Viens, allons. Et ils allèrent dans la ville, dans laquelle était l’homme de Dieu.
11 Walipokuwa wakipanda mlima kwenda mjini, wakakutana na baadhi ya wasichana wanakuja kuchota maji, nao wakawauliza, “Je, mwonaji yuko?”
Et lorsqu’ils montaient la pente de la ville, ils trouvèrent des jeunes filles, qui sortaient pour puiser de l’eau, et ils leur demandèrent: Est-il ici le voyant?
12 Wakajibu, “Yuko, yu mbele yenu amewatangulia, sasa fanyeni haraka, ndiyo tu amekuja mjini kwetu leo, kwa kuwa watu wana dhabihu huko mahali pa juu.
Celles-ci répondant, leur dirent: Il est ici: le voici devant toi, hâte-toi maintenant; car il est venu aujourd’hui dans la ville, parce qu’il y a aujourd’hui un sacrifice pour le peuple sur le haut lieu.
13 Mara tu mwingiapo mjini, mtamkuta kabla hajapanda kwenda mahali pa juu kula. Watu hawataanza kula mpaka atakapofika kwa sababu ni lazima kwanza yeye abariki dhabihu, ndipo wale walioalikwa watakapokula. Pandeni sasa, mtamkuta kwa wakati huu.”
Entrant dans la ville, vous le trouverez aussitôt, avant qu’il monte le haut lieu pour manger; car le peuple ne doit pas manger, jusqu à ce qu’il vienne, parce que c’est lui qui bénit l’hostie, et que c’est après cela que mangent ceux qui ont été appelés. Montez donc maintenant, parce qu’aujourd’hui vous le trouverez.
14 Wakapanda mjini, nao walipokuwa wakiingia mjini, tazama, Samweli alikuwa akija kuelekea walikokwenda mahali pa juu.
Et ils montèrent à la ville. Et comme ils marchaient au milieu de la ville, parut Samuel, sortant au-devant d’eux, pour monter sur le haut lieu.
15 Basi siku moja kabla Sauli hajaja, Bwana alikuwa amemfunulia Samweli jambo hili:
Or, le Seigneur avait ouvert l’oreille de Samuel, un jour avant que n’arrivât Saül, disant:
16 “Kesho wakati kama huu nitakupelekea mtu kutoka nchi ya Benyamini. Umtie mafuta awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli, ndiye atakayewakomboa watu wangu na mkono wa Wafilisti. Nimewaangalia watu wangu, kwa kuwa kilio chao kimenifikia.”
À cette heure même qui est maintenant, demain j’enverrai vers toi un homme de la terre de Benjamin, et tu l’oindras chef sur mon peuple d’Israël; et il sauvera mon peuple de la main des Philistins, parce que j’ai regardé mon peuple; car leur clameur est venue jusqu’à moi.
17 Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekuambia habari zake, kwamba yeye atawatawala watu wangu.”
Et lorsque Samuel eut regardé Saül, le Seigneur lui dit: Voici l’homme dont je t’avais parlé, c’est celui-là qui régnera sur mon peuple.
18 Sauli akamkaribia Samweli langoni na kumuuliza, “Tafadhali, je, waweza kuniambia mahali nyumba ya mwonaji ilipo?”
Or Saül s’approcha de Samuel au milieu de la porte, et dit: Indique-moi, je te prie, où est la maison du voyant.
19 Samweli akamjibu Sauli, “Mimi ndiye mwonaji, panda utangulie mbele yangu mpaka mahali pa juu, kwa kuwa leo itakupasa kula pamoja nami na asubuhi nitakuruhusu uende na nitakuambia yale yote yaliyo moyoni mwako.
Et Samuel répondit à Saül, disant: C’est moi qui suis le voyant: monte devant moi sur le haut lieu, afin que vous mangiez avec moi aujourd’hui, et je t’enverrai le matin; et tout ce qui est dans ton cœur, je te l’expliquerai.
20 Kuhusu wale punda uliowapoteza siku tatu zilizopita, usifadhaike kwa habari yao; wamepatikana. Ni kwa nani ambaye shauku yote ya Israeli imeelekea, kama si kwako na jamaa yote ya baba yako?”
Et quant aux ânesses que tu as perdues, il y a trois jours, ne sois pas inquiet, parce qu’elles sont retrouvées. Et à qui seront toutes les meilleures choses d’Israël? N’est-ce pas à toi et à toute la maison de ton père?
21 Sauli akajibu, “Je, mimi si Mbenyamini, kutoka kabila dogo kuliko yote ya Israeli, nao ukoo wangu si ndio mdogo kuliko koo zote za kabila la Benyamini? Kwa nini uniambie jambo la namna hiyo?”
Mais Saül répondant, dit: Est-ce que je ne suis pas, moi, fils de Jémini, de la plus petite tribu d’Israël, et ma parenté n’est-elle pas la dernière entre toutes les familles de la tribu de Benjamin? Pourquoi donc m’avez-vous tenu ce discours?
22 Kisha Samweli akamleta Sauli na mtumishi wake ndani ukumbini na kuwaketisha mahali pa heshima zaidi miongoni mwa wale waliokuwa wamealikwa; jumla yao walikuwa kama watu thelathini.
C’est pourquoi Samuel prenant Saül et son serviteur, les introduisit dans la salle à manger, et leur donna place à la tête de ceux qui avaient été invités; car ils étaient environ trente personnes.
23 Samweli akamwambia mpishi, “Leta ile sehemu ya nyama niliyokupa, ile niliyokuambia iweke kando.”
Et il dit au cuisinier: Donne la portion, que je t’ai donnée, et que je t’ai commandé de mettre à part auprès de toi.
24 Hivyo mpishi akachukua mguu pamoja na kile kilichokuwa juu yake akaiweka mbele ya Sauli. Samweli akasema, “Hiki ndicho ambacho kimewekwa kwa ajili yako. Ule, kwa sababu kilitengwa kwa ajili yako kwa tukio hili, tangu niliposema, ‘Nimewaalika wageni.’” Naye Sauli akala pamoja na Samweli siku ile.
Or, le cuisinier prit une épaule, et la plaça devant Saül. Et Samuel dit: Voici ce qui est resté, mets-le devant toi, et mange, parce que c’est à dessein qu’on l’a conservé pour toi, quand j’ai invité le peuple. Et Saül mangea avec Samuel en ce jour-là.
25 Baada ya kushuka kutoka mahali pa juu na kufika mjini, Samweli alizungumza na Sauli juu ya dari ya nyumba yake.
Après cela, ils descendirent du haut lieu dans la ville, et Samuel parla avec Saül sur la terrasse, et il prépara un lit à Saül, et Saül dormit.
26 Walipoamka mapema alfajiri, Samweli akamwita Sauli darini, akamwambia, “Jiandae, nami nitakuaga uende zako.” Sauli alipokuwa tayari yeye na Samweli wakatoka nje pamoja.
Lorsque le matin, ils se furent levés, et que déjà il faisait jour, Samuel appela Saül sur la terrasse, disant: Lève-toi et je, t’enverrai. Et Saül se leva, et ils} sortirent tous deux, c’est-à-dire lui-même et Samuel.
27 Hata walipokuwa wakiteremka kuelekea mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi atangulie mbele yetu.” Naye mtumishi akafanya hivyo. “Lakini subiri hapa kwa kitambo kidogo, ili nipate kukupa ujumbe kutoka kwa Mungu.”
Et lorsqu’ils descendaient à l’extrémité de la ville, Samuel dit à Saül: Dis à ton serviteur qu’il nous précède, et qu’il passe outre; mais toi, demeure un peu, afin que je te révèle la parole de Dieu.

< 1 Samweli 9 >