< 1 Samweli 8 >
1 Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
Kad nu Samuēls bija vecs palicis, tad viņš iecēla savus dēlus Israēlim par soģiem.
2 Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
Viņa pirmdzimušā dēla vārds bija Joēls, un tā otrā vārds bija Abijus, tie bija soģi Bēršebā.
3 Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
Bet viņa dēli nestaigāja viņa ceļos, bet dzinās pēc mantas un ņēma dāvanas un grozīja tiesu.
4 Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
Tad visi Israēla vecaji sapulcinājās un nāca pie Samuēla uz Rāmatu,
5 Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
Un uz to sacīja: redzi, tu esi palicis vecs un tavi dēli nestaigā tavos ceļos; tad nu cel mums ķēniņu, kas mūs tiesā, kā tas ir visām tautām.
6 Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.
Un šī valoda Samuēlim nepatika, kad tie sacīja: dod mums ķēniņu, kas mūs tiesā. Un Samuēls pielūdza To Kungu.
7 Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.
Tad Tas Kungs sacīja uz Samuēli: paklausi to ļaužu balsij iekš visa, ko tie uz tevi runā, jo tie nav tevi atmetuši, bet Mani tie ir atmetuši, ka Man vairs nebūs ķēniņam būt pār tiem.
8 Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.
Tā tie arvien ir darījuši no tās dienas, kad Es tos esmu izvedis no Ēģiptes, līdz šai dienai, un Mani atstājuši un kalpojuši citiem dieviem; tā tie tev arīdzan dara.
9 Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”
Un nu klausi viņu balsij, bet apliecini tiem skaidri un dari tiem zināmu, kāda tiesa ķēniņam, kas pār tiem valdīs.
10 Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.
Tad Samuēls visus Tā Kunga vārdus sacīja tiem ļaudīm, kas ķēniņu no viņa prasīja.
11 Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.
Un viņš sacīja: šī būs tā tiesa ķēniņam, kas pār jums valdīs: jūsu dēlus viņš ņems un tos cels uz saviem ratiem un par saviem jātniekiem, un ka tie skrien viņa ratu priekšā.
12 Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.
Un viņš tos cels par virsniekiem pār piecdesmitiem, un ka tie viņa tīrumu ar un viņa labību pļauj, un ka tie viņam taisa kara rīkus un ratu rīkus.
13 Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.
Un jūsu meitas viņš ņems par zalvju(ziežu) taisītājām un par pavārēm un par cepējām.
14 Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
Un jūsu labākos tīrumus un vīna un eļļas dārzus viņš ņems un dos saviem kalpiem.
15 Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.
Un no jūsu druvām un vīna dārziem viņš ņems to desmito un to dos saviem sulaiņiem un kalpiem.
16 Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.
Un viņš ņems jūsu kalpus un jūsu kalpones un jūsu labākos jaunekļus un jūsu ēzeļus, un ar tiem darīs savu darbu.
17 Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.
No jūsu ganāmiem pulkiem viņš ņems to desmito, un jūs būsiet viņam par kalpiem.
18 Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”
Tad jūs gan tai laikā brēksiet sava ķēniņa dēļ, ko jūs sev izvēlējušies, bet Tas Kungs jūs tai dienā neklausīs.
19 Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala.
Bet tie ļaudis negribēja klausīt Samuēla balsij un sacīja: ne tā, bet ķēniņš lai ir pār mums.
20 Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”
Un mēs gribam būt, kā visas citas tautas, un mūsu ķēniņam būs mūs tiesāt un mūsu priekšā iziet un vest mūsu karus.
21 Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana.
Un Samuēls dzirdēja visus tos ļaužu vārdus, un tos atsacīja Tam Kungam.
22 Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.” Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”
Tad Tas Kungs sacīja uz Samuēli: paklausi viņu balsij un cel tiem ķēniņu. Tad Samuēls sacīja uz Israēla ļaudīm: ejat ikkatrs savā pilsētā.