< 1 Samweli 8 >

1 Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
Lorsque Samuel fut âgé, il établit ses fils comme juges sur Israël.
2 Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
Or le nom de son premier-né était Joël, et le nom de son second, Abija. Ils étaient juges à Beersheba.
3 Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
Ses fils ne marchèrent pas dans ses voies, mais se détournèrent vers des gains malhonnêtes, acceptèrent des pots-de-vin et pervertirent la justice.
4 Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
Alors tous les anciens d'Israël se rassemblèrent et vinrent trouver Samuel à Rama.
5 Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
Ils lui dirent: « Voici, tu es vieux, et tes fils ne marchent pas dans tes voies. Maintenant, fais-nous un roi pour nous juger comme toutes les nations. »
6 Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.
Mais ce qui déplut à Samuel, c'est qu'ils dirent: « Donne-nous un roi pour nous juger. » Samuel pria Yahvé.
7 Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.
Yahvé dit à Samuel: « Écoute la voix du peuple dans tout ce qu'il te dira, car ce n'est pas toi qu'il a rejeté, mais c'est moi qu'il a rejeté comme roi sur lui.
8 Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.
Ils ont fait tout ce qu'ils ont fait depuis le jour où je les ai fait monter d'Égypte jusqu'à ce jour, en m'abandonnant et en servant d'autres dieux, et ils te feront de même.
9 Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”
Maintenant donc, écoutez leur voix. Cependant, tu protesteras solennellement auprès d'eux, et tu leur indiqueras la voie du roi qui régnera sur eux. »
10 Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.
Samuel rapporta toutes les paroles de Yahvé au peuple qui lui demandait un roi.
11 Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.
Il dit: « Voici comment agira le roi qui régnera sur vous: il prendra vos fils et les mettra à son service, pour ses chars et pour être ses cavaliers; et ils courront devant ses chars.
12 Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.
Il les nommera chefs de milliers et chefs de cinquantaines, et il en chargera de labourer son sol et de moissonner sa récolte, de fabriquer ses instruments de guerre et les instruments de ses chars.
13 Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.
Il prendra tes filles pour en faire des parfumeuses, des cuisinières et des boulangères.
14 Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
Il prendra tes champs, tes vignes et tes oliviers, même tes meilleurs, et les donnera à ses serviteurs.
15 Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.
Il prendra le dixième de tes semences et de tes vignes, et le donnera à ses officiers et à ses serviteurs.
16 Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.
Il prendra tes serviteurs, tes servantes, tes meilleurs jeunes gens et tes ânes, et les affectera à son propre travail.
17 Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.
Il prendra le dixième de vos troupeaux, et vous serez ses esclaves.
18 Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”
Vous crierez en ce jour-là à cause de votre roi que vous vous serez choisi, et Yahvé ne vous répondra pas en ce jour-là. »
19 Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala.
Mais le peuple refusa d'écouter la voix de Samuel, et ils dirent: « Non, mais nous aurons un roi sur nous,
20 Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”
afin que nous soyons aussi comme toutes les nations, et que notre roi nous juge, qu'il sorte devant nous et qu'il mène nos combats. »
21 Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana.
Samuel entendit toutes les paroles du peuple, et il les répéta aux oreilles de l'Éternel.
22 Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.” Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”
Yahvé dit à Samuel: « Écoute leur voix, et fais-leur un roi. » Samuel dit aux hommes d'Israël: « Retournez chacun dans votre ville. »

< 1 Samweli 8 >