< 1 Samweli 8 >
1 Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
When Samuel was nowe become olde, he made his sonnes Iudges ouer Israel.
2 Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
(And the name of his eldest sonne was Ioel, and the name of the second Abiah) euen Iudges in Beer-sheba.
3 Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
And his sonnes walked not in his wayes, but turned aside after lucre, and tooke rewards, and peruerted the iudgement.
4 Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
Wherefore all the Elders of Israel gathered them together, and came to Samuel vnto Ramah,
5 Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
And said vnto him, Beholde, thou art olde, and thy sonnes walke not in thy wayes: make vs nowe a King to iudge vs like all nations.
6 Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.
But the thing displeased Samuel, when they said, Giue vs a King to iudge vs: and Samuel prayed vnto the Lord.
7 Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.
And the Lord said vnto Samuel, Heare the voyce of the people in all that they shall say vnto thee: for they haue not cast thee away, but they haue cast me away, that I should not reigne ouer the.
8 Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.
As they haue euer done since I brought them out of Egypt euen vnto this day, (and haue forsaken me, and serued other gods) euen so doe they vnto thee.
9 Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”
Nowe therefore hearken vnto their voyce: howbeit yet testifie vnto them, and shewe them the maner of ye King that shall reigne ouer them.
10 Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.
So Samuel told all the wordes of the Lord vnto the people that asked a King of him.
11 Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.
And he saide, This shall be the maner of the King that shall reigne ouer you: he will take your sonnes, and appoint them to his charets, and to be his horsemen, and some shall runne before his charet.
12 Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.
Also he will make them his captaines ouer thousands, and captaines ouer fifties, and to eare his ground, and to reape his haruest, and to make instruments of warre, and the thinges that serue for his charets.
13 Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.
He will also take your daughters and make them apoticaries, and cookes, and bakers.
14 Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
And he will take your fieldes, and your vineyardes, and your best Oliue trees, and giue them to his seruants.
15 Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.
And he will take the tenth of your seede, and of your vineyards, and giue it to his Eunuches, and to his seruants.
16 Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.
And he will take your men seruants, and your maide seruants, and the chiefe of your yong men, and your asses, and put them to his worke.
17 Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.
He will take the tenth of your sheepe, and ye shall be his seruants.
18 Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”
And ye shall crie out at that day, because of your King, whom ye haue chosen you, and the Lord will not heare you at that day.
19 Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala.
But the people would not heare the voyce of Samuel, but did say, Nay, but there shall be a King ouer vs.
20 Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”
And we also will be like all other nations, and our King shall iudge vs, and goe out before vs, and fight our battels.
21 Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana.
Therefore when Samuel heard all ye wordes of ye people, he rehearsed the in ye eares of ye Lord.
22 Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.” Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”
And the Lord saide to Samuel, Hearken vnto their voyce, and make them a King. And Samuel said vnto the men of Israel, Goe euery man vnto his citie.