< 1 Samweli 7 >

1 Kisha watu wa Kiriath-Yearimu wakaja na kulichukua Sanduku la Bwana. Wakalipeleka katika nyumba ya Abinadabu juu kilimani na kumweka Eleazari mwanawe wakfu kulichunga Sanduku la Bwana.
Przyszli więc ludzie z Kiriat-Jearim, zabrali arkę PANA i wnieśli ją do domu Abinadaba na wzgórzu. Eleazara zaś, jego syna, poświęcili, aby strzegł arki PANA.
2 Sanduku la Bwana lilibakia huko Kiriath-Yearimu kwa muda mrefu, yaani jumla ya miaka ishirini, nao watu wa Israeli wakaomboleza na kumtafuta Bwana.
A od dnia przybycia arki do Kiriat-Jearim upłynęło dużo czasu, to jest dwadzieścia lat, a cały dom Izraela płakał za PANEM.
3 Naye Samweli akawaambia nyumba yote ya Israeli, “Ikiwa mtamrudia Bwana kwa mioyo yenu yote, basi iacheni miungu migeni na Maashtorethi na kujitoa wenyewe kwa Bwana na kumtumikia yeye peke yake, naye atawaokoa ninyi na mkono wa Wafilisti.”
I Samuel powiedział do całego domu Izraela: Jeśli z całego swego serca nawrócicie się do PANA, wyrzućcie spośród siebie obcych bogów oraz Asztarty i przygotujcie swoje serce PANU, i służcie tylko jemu. Wtedy wybawi was z ręki Filistynów.
4 Hivyo Waisraeli wakaweka mbali Mabaali yao na Maashtorethi, nao wakamtumikia Bwana peke yake.
Synowie Izraela usunęli więc Baalów i Asztarty i służyli tylko PANU.
5 Kisha Samweli akasema, “Wakusanyeni Israeli wote huko Mispa, nami nitawaombea ninyi kwa Bwana.”
Wtedy Samuel powiedział: Zgromadźcie całego Izraela w Mispie, a ja będę modlił się za wami do PANA.
6 Walipokwisha kukutanika huko Mispa, walichota maji na kuyamimina mbele za Bwana. Siku hiyo walifunga na wakaungama, wakisema, “Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana.” Naye Samweli alikuwa kiongozi wa Israeli huko Mispa.
Zgromadzili się więc w Mispie i czerpali wodę, którą wylewali przed PANEM. Pościli tam tego dnia i mówili: Zgrzeszyliśmy przeciw PANU. A Samuel sądził synów Izraela w Mispie.
7 Wafilisti waliposikia kwamba Israeli wamekusanyika huko Mispa, watawala wa Wafilisti wakapanda ili kuwashambulia. Waisraeli waliposikia habari hiyo, waliogopa kwa sababu ya Wafilisti.
A [gdy] Filistyni usłyszeli, że synowie Izraela zgromadzili się w Mispie, wyruszyli książęta filistyńscy przeciw Izraelowi. Kiedy usłyszeli o tym synowie Izraela, zlękli się Filistynów.
8 Wakamwambia Samweli, “Usiache kumlilia Bwana, Mungu wetu, kwa ajili yetu, ili apate kutuokoa na mikono ya Wafilisti.”
I synowie Izraela powiedzieli do Samuela: Nie przestawaj wołać za nami do PANA, naszego Boga, aby nas wybawił z ręki Filistynów.
9 Kisha Samweli akamchukua mwana-kondoo anyonyaye na kumtoa mzima kama sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana. Akamlilia Bwana kwa niaba ya Israeli, naye Bwana akamjibu.
Samuel wziął więc jedno jagnię ssące i złożył je PANU w ofierze całopalnej. I Samuel wołał do PANA za Izraelem, a PAN go wysłuchał.
10 Samweli alipokuwa anatoa hiyo dhabihu ya kuteketezwa, Wafilisti wakasogea karibu ili kupigana vita na Israeli. Lakini siku ile Bwana alinguruma kwa ngurumo kubwa dhidi ya Wafilisti na kuwafanya wafadhaike na kutetemeka hivi kwamba walikimbizwa mbele ya Waisraeli.
A kiedy Samuel składał całopalenie, Filistyni nadciągnęli, aby walczyć z Izraelem. Lecz w tym dniu PAN zagrzmiał wielkim grzmotem nad Filistynami i rozproszył ich tak, że zostali pobici przed Izraelem.
11 Watu wa Israeli wakatoka mbio huko Mispa na kuwafuatia Wafilisti, wakiwachinja njiani hadi mahali chini ya Beth-Kari.
A Izraelici wyruszyli z Mispy, gonili Filistynów i bili ich aż pod Bet-Kar.
12 Ndipo Samweli akachukua jiwe na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni. Akaliita Ebenezeri, akisema, “Hata sasa Bwana ametusaidia.”
Wtedy Samuel wziął kamień, ustawił go między Mispą a Szen i nazwał go Ebenezer, mówiąc: Aż dotąd pomagał nam PAN.
13 Basi Wafilisti wakashindwa na hawakuvamia nchi ya Israeli tena. Katika maisha yote ya Samweli, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya Wafilisti.
Tak zostali upokorzeni Filistyni i już nie przekraczali granic Izraela, a ręka PANA była przeciwko Filistynom po wszystkie dni Samuela.
14 Miji kuanzia Ekroni hadi Gathi, ile ambayo Wafilisti walikuwa wameiteka kutoka Israeli, ilirudishwa kwake, naye Israeli akazikomboa nchi jirani mikononi mwa Wafilisti. Kukawepo amani kati ya Israeli na Waamori.
Izraelowi zostały przywrócone miasta, które Filistyni zabrali Izraelowi, od Ekronu aż do Gat, a ich granice wyzwolił Izrael z ręki Filistynów. I pokój panował między Izraelem a Amorytami.
15 Samweli akaendelea kama mwamuzi juu ya Israeli siku zote za maisha yake.
A Samuel sądził Izraela po wszystkie dni swego życia.
16 Mwaka hadi mwaka aliendelea kuzunguka kutoka Betheli mpaka Gilgali na Mispa, akiamua Israeli katika sehemu hizo zote.
Co roku chodził też i obchodził Betel, Gilgal i Mispę i sądził Izraela we wszystkich tych miejscach.
17 Lakini kila mara alirudi Rama, kulikokuwa nyumbani kwake, huko pia aliwaamua Israeli. Naye huko alimjengea Bwana madhabahu.
Potem wracał do Rama, ponieważ tam był jego dom. Tam sądził Izraela i tam też zbudował ołtarz PANU.

< 1 Samweli 7 >