< 1 Samweli 6 >

1 Sanduku la Bwana lilipokuwa limekaa katika nchi ya Wafilisti kwa miezi saba,
صندوق عهد، مدت هفت ماه در فلسطین ماند.
2 Wafilisti waliwaita makuhani wa Dagoni na waaguzi, na kuwaambia, “Tutafanya nini na hili Sanduku la Bwana? Tuambieni jinsi tutakavyolirudisha mahali pake.”
فلسطینی‌ها کاهنان و جادوگران خود را فرا خواندند و از آنها پرسیدند: «با صندوق عهد خداوند چه کنیم؟ بگویید که چگونه آن را به مکان اصلی‌اش برگردانیم؟»
3 Wakajibu, “Kama mtalirudisha Sanduku la Mungu wa Israeli, msilirudishe mikono mitupu bali kwa vyovyote mpelekeeni sadaka ya hatia. Kisha mtaponywa, nanyi mtafahamu kwa nini mkono wake haujaondolewa kwenu.”
آنها جواب دادند: «اگر می‌خواهید صندوق عهد خدای اسرائیل را پس بفرستید، آن را دست خالی نفرستید، بلکه هدیۀ جبران نیز همراه آن بفرستید تا او بلا را متوقف کند. اگر شفا یافتید، آنگاه معلوم می‌شود که این بلا از جانب خدا بر شما نازل شده است.»
4 Wafilisti wakawauliza, “Ni sadaka gani ya hatia tutakayompelekea?” Wakajibu, “Majipu matano ya dhahabu na panya wa dhahabu watano, kulingana na idadi ya watawala wa Wafilisti, kwa sababu tauni iyo hiyo imewaua ninyi na watawala wenu.
مردم پرسیدند: «چه نوع هدیه‌ای بفرستیم؟» آنها گفتند: «به تعداد رهبران فلسطینی‌ها، پنج شیء از طلا به شکل دمل و پنج شیء از طلا به شکل موش که تمام سرزمین ما را ویران کرده‌اند، درست کنید و به احترام خدای اسرائیل، آنها را بفرستید تا شاید بلا را از شما و خدایان و سرزمین شما دور کند.
5 Tengenezeni mifano ya majipu na ya panya wale wanaoharibu nchi yenu, nanyi mheshimuni Mungu wa Israeli. Labda ataondoa mkono wake kutoka kwenu na kwa miungu yenu na nchi yenu.
6 Kwa nini ninyi mnafanya mioyo yenu migumu kama Wamisri na Farao walivyofanya? Je, alipowatendea kwa ukali, hawakuwaachia Waisraeli wakaenda zao?
مانند فرعون و مصری‌ها سرسختی نکنید. آنها اجازه ندادند اسرائیلی‌ها از مصر خارج شوند، تا اینکه خدا بلاهای هولناکی بر آنها نازل کرد.
7 “Sasa basi, wekeni gari jipya la kukokotwa pamoja na ngʼombe wawili ambao wamezaa lakini ambao kamwe hawajafungwa nira. Fungieni hao ngʼombe hilo gari, lakini ondoeni ndama wao na mwaweke zizini.
پس الان ارابه‌ای تازه بسازید و دو گاو شیرده که یوغ بر گردن آنها گذاشته نشده باشد بگیرید و آنها را به ارابه ببندید و گوساله‌هایشان را در طویله نگه دارید.
8 Chukueni hilo Sanduku la Bwana na mliweke juu ya gari la kukokotwa, na ndani ya kasha kando yake wekeni hivyo vitu vya dhahabu mnavyompelekea Bwana kama sadaka ya hatia. Lipelekeni,
صندوق عهد را بر ارابه قرار دهید و هدایای طلا را که برای عذرخواهی می‌فرستید در صندوقچه‌ای پهلوی آن بگذارید. آنگاه گاوها را رها کنید تا هر جا که می‌خواهند بروند.
9 lakini liangalieni kwa makini. Iwapo litakwenda katika nchi yake lenyewe, kuelekea Beth-Shemeshi, basi tutajua kwamba Bwana ndiye alileta haya maafa makubwa juu yetu. Lakini kama halikwenda, basi tutajua kwamba haukuwa mkono wa Bwana uliotupiga na kwamba iliyotokea kwetu ni ajali.”
اگر آنها از مرز ما عبور کرده، به بیت‌شمس رفتند، بدانید خداست که این بلای عظیم را بر سر ما آورده است، اما اگر نرفتند آنگاه خواهیم دانست که این بلاها اتفاقی بوده و دست خدا در آن دخالتی نداشته است.»
10 Basi wakafanya hivyo. Wakachukua ngʼombe wawili wa aina hiyo, wakawafungia hilo gari la kukokotwa, nao ndama wao wakawekwa zizini.
فلسطینی‌ها چنین کردند. دو گاو شیرده را به ارابه بستند و گوساله‌هایشان را در طویله نگه داشتند.
11 Wakaliweka Sanduku la Bwana juu ya hilo gari la kukokotwa pamoja na lile kasha lenye ile mifano ya panya wa dhahabu na ya majipu ya dhahabu.
آنگاه صندوق عهد خداوند و صندوقچهٔ محتوی هدایای طلا را بر ارابه گذاشتند.
12 Kisha hao ngʼombe wakaenda moja kwa moja kuelekea Beth-Shemeshi, wakishuka bila kugeuka kuume au kushoto, huku wakilia njia yote. Watawala wa Wafilisti waliwafuata hao ngʼombe hadi mpakani mwa Beth-Shemeshi.
گاوها یکراست به طرف بیت‌شمس روانه شدند و همان‌طور که می‌رفتند صدا می‌کردند. رهبران فلسطینی تا سرحد بیت‌شمس، به دنبال آنها رفتند.
13 Wakati huu watu wa Beth-Shemeshi walikuwa wakivuna ngano yao huko bondeni, walipoinua macho yao na kuona lile Sanduku, wakafurahi kuliona.
مردم بیت‌شمس در دره مشغول درو گندم بودند. آنها وقتی صندوق عهد خداوند را دیدند، بسیار شاد شدند.
14 Lile gari la kukokotwa lilikuja mpaka kwenye shamba la Yoshua wa Beth-Shemeshi, nalo likasimama kando ya mwamba mkubwa. Watu wakapasua mbao za lile gari la kukokotwa na kutoa dhabihu wale ngʼombe kama sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
ارابه وارد مزرعهٔ شخصی به نام یهوشع شد و در کنار تخته سنگ بزرگی ایستاد. مردم چوب ارابه را شکسته، گاوها را به عنوان قربانی سوختنی به خداوند تقدیم کردند.
15 Walawi walilishusha Sanduku la Bwana, pamoja na lile kasha lililokuwa na vile vitu vya dhahabu na kuviweka juu ya ule mwamba mkubwa. Siku ile watu wa Beth-Shemeshi wakatoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu kwa Bwana.
چند نفر از مردان قبیلهٔ لاوی، صندوق عهد و صندوقچهٔ محتوی اشیاء طلا را برداشته، روی آن تخته سنگ بزرگ گذاشتند. در آن روز مردان بیت‌شمس قربانی سوختنی و قربانیهای دیگر به حضور خداوند تقدیم نمودند.
16 Wale watawala watano wa Wafilisti waliona haya yote, nao wakarudi siku ile ile mpaka Ekroni.
آن پنج رهبر فلسطینی وقتی این واقعه را دیدند، در همان روز به عقرون برگشتند.
17 Haya ndiyo yale majipu ya dhahabu Wafilisti waliyotuma kama sadaka ya hatia kwa Bwana, moja kwa ajili ya Ashdodi, moja kwa Gaza, moja kwa Ashkeloni, moja kwa Gathi, na moja kwa Ekroni.
پنج هدیهٔ طلا به شکل دمل که توسط فلسطینی‌ها جهت عذرخواهی، برای خداوند فرستاده شد، از طرف شهرهای اشدود، غزه، اشقلون، جت و عقرون بود.
18 Nayo hesabu ya wale panya wa dhahabu ilikuwa kulingana na idadi ya miji ya Wafilisti ya watawala watano wa Wafilisti: miji yao iliyozungukwa na maboma, pamoja na vijiji vya miji hiyo. Ule mwamba mkubwa, ambao juu yake waliliweka lile Sanduku la Bwana, ni ushahidi hadi leo katika shamba la Yoshua wa Beth-Shemeshi.
پنج موش طلا نیز به تعداد رهبران فلسطینی بود که بر شهرهای حصاردار و دهات اطرافشان فرمان می‌راندند. آن تخته سنگ بزرگ که صندوق عهد را روی آن گذاشتند تا به امروز در مزرعهٔ یهوشع واقع در بیت‌شمس باقی است.
19 Lakini Mungu aliwapiga baadhi ya watu wa Beth-Shemeshi, akiwaua watu sabini miongoni mwao kwa sababu walichungulia ndani ya Sanduku la Bwana. Watu wakaomboleza kwa sababu ya pigo zito kutoka kwa Bwana,
اما خداوند هفتاد نفر از مردان بیت‌شمس را کشت، زیرا به داخل صندوق عهد نگاه کرده بودند. مردم بیت‌شمس به‌سبب این کشتار سوگواری عظیمی کردند.
20 nao watu wa Beth-Shemeshi wakauliza, “Ni nani awezaye kusimama mbele za Bwana, huyu Mungu aliye mtakatifu? Sanduku litapanda kwenda kwa nani kutoka hapa?”
گفتند: «چه کسی می‌تواند در مقابل خداوند که خدای قدوسی است، بایستد؟ اکنون صندوق عهد را به کجا بفرستیم؟»
21 Kisha wakatuma wajumbe kwa watu wa Kiriath-Yearimu, wakisema, “Wafilisti wamerudisha Sanduku la Bwana. Shukeni na mlipandishe huko kwenu.”
پس قاصدانی را نزد ساکنان قریهٔ یعاریم فرستاده، گفتند: «فلسطینی‌ها صندوق عهد خداوند را برگردانده‌اند. بیایید و آن را ببرید.»

< 1 Samweli 6 >