< 1 Samweli 5 >

1 Baada ya Wafilisti kuteka Sanduku la Mungu, walilichukua kutoka Ebenezeri mpaka Ashdodi.
Or. les Philistins prirent l’arche de Dieu, et la transportèrent de la pierre du Secours à Azot.
2 Kisha wakaliingiza lile Sanduku ndani ya hekalu la Dagoni na kuliweka kando ya huyo Dagoni.
Ainsi les Philistins prirent l’arche de Dieu, et ils la portèrent dans le temple de Dagon, et la placèrent auprès de Dagon.
3 Watu wa Ashdodi walipoamka asubuhi na mapema kesho yake, kumbe, wakamkuta Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana! Wakamwinua Dagoni na kumrudisha mahali pake.
Et lorsque les Azotiens se furent levés le lendemain au point du jour, voilà que Dagon gisait renversé contre terre devant l’arche du Seigneur; et ils prirent Dagon, et le rétablirent à sa place.
4 Lakini asubuhi iliyofuata, walipoamka kumbe, walimkuta huyo Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana! Kichwa chake na mikono vilikuwa vimevunjwa navyo vimelala kizingitini, ni kiwiliwili chake tu kilichokuwa kimebaki.
Et de nouveau se levant de matin le jour suivant, ils trouvèrent Dagon gisant sur sa face contre terre, devant l’arche du Seigneur; mais la tête de Dagon et les deux paumes de ses mains coupées étaient sur le seuil de la porte,
5 Ndiyo sababu mpaka leo makuhani wa Dagoni wala wengine waingiao katika hekalu la Dagoni huko Ashdodi hawakanyagi kizingiti.
Et le tronc seul de Dagon était demeuré à sa place. Pour ce motif, les prêtres de Dagon et tous ceux qui entrent dans son temple, ne mettent pas le pied sur le seuil de la porte de Dagon à Azot jusqu’au présent jour.
6 Mkono wa Bwana ulikuwa mzito juu ya watu wa Ashdodi na vijiji jirani, akaleta uharibifu juu yao na kuwatesa kwa majipu.
Or, la main du Seigneur s’appesantit sur les Azotiens, et il les désola; et il frappa Azot et ses confins à la partie la plus secrète du corps. Et les villages et les champs au milieu de cette contrée fourmillèrent de rats qui naquirent, et la confusion causée par une grande mortalité régna dans la ville.
7 Watu wa Ashdodi walipoona kile kilichokuwa kikitokea, wakasema, “Sanduku la Mungu wa Israeli kamwe lisikae hapa pamoja na sisi, kwa sababu mkono wake ni mzito juu yetu na juu ya Dagoni mungu wetu.”
Cependant les hommes d’ Azot voyant une plaie de cette sorte, dirent: Que l’arche du Dieu d’Israël ne demeure pas chez nous, parce que sa main pèse sur nous et sur Dagon notre Dieu.
8 Basi wakawaita watawala wote wa Wafilisti pamoja na kuwauliza, “Tutafanya nini na hili Sanduku la Mungu wa Israeli?” Wakajibu, “Sanduku la Mungu wa Israeli na liende Gathi.” Basi wakalihamisha Sanduku la Mungu wa Israeli.
Et ils envoyèrent chercher, et rassemblèrent tous les satrapes des Philistins auprès d’eux, et dirent: Que ferons-nous de l’arche du Dieu d’Israël? Et les Géthéens répondirent: Que l’arche du Dieu d’Israël soit conduite autour du pays. Et ils conduisirent l’arche du Dieu d’Israël autour du pays.
9 Lakini baada ya kulihamisha, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya huo mji wa Gathi, akiuweka katika fadhaa kuu. Mungu akawatesa watu wa huo mji, vijana kwa wazee, kwa kuwaletea majipu.
Or, eux la conduisant ainsi, la main du Seigneur faisait dans chaque cité un très grand carnage, et il frappait les hommes de chacune de ces villes, depuis le petit jusqu’au grand, et leurs intestins sortant, se pourrissaient. Aussi les Géthéens tinrent conseil et se firent des sièges de peaux.
10 Basi wakapeleka Sanduku la Mungu Ekroni. Wakati Sanduku la Mungu lilipokuwa linaingia Ekroni, watu wa Ekroni walilia wakisema “Wamelileta Sanduku la Mungu wa Israeli kwetu ili kutuua sisi na watu wetu.”
Ils envoyèrent donc l’arche de Dieu à Accaron. Et lorsque l’arche de Dieu fut venue à Accaron, les Accaronites s’écrièrent, disant: Ils nous ont amené l’arche du Dieu d’Israël, pour qu’elle nous tue, nous et notre peuple.
11 Basi wakawaita watawala wote wa Wafilisti pamoja na kusema, “Liondoeni Sanduku la Mungu wa Israeli na lirudishwe mahali pake, la sivyo litatuua sisi na watu wetu.” Kwa kuwa kifo kilikuwa kimeujaza mji hofu; kwani mkono wa Mungu ulikuwa mzito sana juu yake.
C’est pourquoi ils envoyèrent chercher et rassemblèrent tous les satrapes des Philistins, qui dirent: Renvoyez l’arche du Dieu d’Israël, et qu’elle retourne en son lieu, et qu’elle ne nous tue pas avec notre peuple.
12 Wale ambao hawakufa walipatwa na majipu, na kilio cha mji kilikwenda juu hadi mbinguni.
Car la frayeur de la mort se répandait dans chaque ville, et la main de Dieu devenait extrêmement pesante; les hommes aussi, qui n’étaient pas morts, étaient frappés à la partie la plus secrète du corps; et le cri lamentable de chaque cité montait jusqu’au ciel.

< 1 Samweli 5 >