< 1 Samweli 5 >

1 Baada ya Wafilisti kuteka Sanduku la Mungu, walilichukua kutoka Ebenezeri mpaka Ashdodi.
Then the Philistims tooke the Arke of God and caried it from Eben-ezer vnto Ashdod,
2 Kisha wakaliingiza lile Sanduku ndani ya hekalu la Dagoni na kuliweka kando ya huyo Dagoni.
Euen the Philistims tooke ye Arke of God, and brought it into the house of Dagon, and set it by Dagon.
3 Watu wa Ashdodi walipoamka asubuhi na mapema kesho yake, kumbe, wakamkuta Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana! Wakamwinua Dagoni na kumrudisha mahali pake.
And when they of Ashdod rose the next day in the morning, beholde, Dagon was fallen vpon his face on the ground before the Arke of the Lord, and they tooke vp Dagon, and set him in his place againe.
4 Lakini asubuhi iliyofuata, walipoamka kumbe, walimkuta huyo Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana! Kichwa chake na mikono vilikuwa vimevunjwa navyo vimelala kizingitini, ni kiwiliwili chake tu kilichokuwa kimebaki.
Also they rose vp earely in the morning the next day, and beholde, Dagon was fallen vpon his face on the ground before the Arke of the Lord, and the head of Dagon and the two palmes of his hands were cut off vpon the thresholde: onely the stumpe of Dagon was left to him.
5 Ndiyo sababu mpaka leo makuhani wa Dagoni wala wengine waingiao katika hekalu la Dagoni huko Ashdodi hawakanyagi kizingiti.
Therefore the Priests of Dagon, and all that come into Dagons house tread not on the thresholde of Dagon in Ashdod, vnto this day.
6 Mkono wa Bwana ulikuwa mzito juu ya watu wa Ashdodi na vijiji jirani, akaleta uharibifu juu yao na kuwatesa kwa majipu.
But the hand of the Lord was heauie vpon them of Ashdod, and destroyed them, and smote them with the emerods, both Ashdod, and the coastes thereof.
7 Watu wa Ashdodi walipoona kile kilichokuwa kikitokea, wakasema, “Sanduku la Mungu wa Israeli kamwe lisikae hapa pamoja na sisi, kwa sababu mkono wake ni mzito juu yetu na juu ya Dagoni mungu wetu.”
And when the men of Ashdod sawe this, they sayd, Let not the Arke of the God of Israel abide with vs: for his hand is sore vpon vs and vpon Dagon our god.
8 Basi wakawaita watawala wote wa Wafilisti pamoja na kuwauliza, “Tutafanya nini na hili Sanduku la Mungu wa Israeli?” Wakajibu, “Sanduku la Mungu wa Israeli na liende Gathi.” Basi wakalihamisha Sanduku la Mungu wa Israeli.
They sent therefore and gathered all the princes of the Philistims vnto them, and sayde, What shall we doe with the Arke of the God of Israel? And they answered, Let the Arke of the God of Israel be caried about vnto Gath: and they caried the Arke of the God of Israel about.
9 Lakini baada ya kulihamisha, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya huo mji wa Gathi, akiuweka katika fadhaa kuu. Mungu akawatesa watu wa huo mji, vijana kwa wazee, kwa kuwaletea majipu.
And when they had caried it about, the hand of the Lord was against the citie with a very great destruction, and he smote the men of the citie both small and great, and they had emerods in their secret partes.
10 Basi wakapeleka Sanduku la Mungu Ekroni. Wakati Sanduku la Mungu lilipokuwa linaingia Ekroni, watu wa Ekroni walilia wakisema “Wamelileta Sanduku la Mungu wa Israeli kwetu ili kutuua sisi na watu wetu.”
Therefore they sent the Arke of God to Ekron: and assoone as the Arke of God came to Ekron, the Ekronites cryed out, saying, They haue brought the Arke of the God of Israel to vs to slay vs and our people.
11 Basi wakawaita watawala wote wa Wafilisti pamoja na kusema, “Liondoeni Sanduku la Mungu wa Israeli na lirudishwe mahali pake, la sivyo litatuua sisi na watu wetu.” Kwa kuwa kifo kilikuwa kimeujaza mji hofu; kwani mkono wa Mungu ulikuwa mzito sana juu yake.
Therefore they sent, and gathered together all the princes of the Philistims and sayd, Sende away the Arke of the God of Israel, and let it returne to his owne place, that it slay vs not and our people: for there was a destruction and death throughout all the citie, and the hand of God was very sore there.
12 Wale ambao hawakufa walipatwa na majipu, na kilio cha mji kilikwenda juu hadi mbinguni.
And the men that dyed not, were smitten with the emerods: and the cry of the citie went vp to heauen.

< 1 Samweli 5 >