< 1 Samweli 4 >

1 Nalo neno la Samweli likaja kwa Israeli yote. Basi Waisraeli walitoka kwenda kupigana dhidi ya Wafilisti. Waisraeli wakapiga kambi huko Ebenezeri, nao Wafilisti wakapiga kambi huko Afeki.
Or la parole de Samuel était pour tout Israël. Et Israël sortit en guerre à la rencontre des Philistins, et campa près d'Ében-Ézer; et les Philistins campèrent à Aphek.
2 Wafilisti wakapanga safu za majeshi yao kupambana na Israeli, wakati vita vilipoenea, Israeli wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua askari wa Israeli wapatao 4,000 kwenye uwanja wa vita.
Et les Philistins se rangèrent en bataille contre Israël; et le combat s'engagea, et Israël fut battu par les Philistins, qui tuèrent en bataille rangée dans la campagne, environ quatre mille hommes.
3 Askari waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakawauliza, “Kwa nini Bwana ameruhusu leo tushindwe mbele ya Wafilisti? Tuleteni Sanduku la Agano la Bwana kutoka Shilo, ili lipate kwenda pamoja nasi, na kutuokoa kutoka mikono ya adui zetu.”
Et le peuple étant rentré au camp, les anciens d'Israël dirent: Pourquoi l'Éternel nous a-t-il laissé battre aujourd'hui par les Philistins? Faisons venir de Silo l'arche de l'alliance de l'Éternel, et qu'il vienne au milieu de nous, et nous délivre de la main de nos ennemis.
4 Hivyo wakawatuma watu huko Shilo, nao wakalichukua Sanduku la Agano la Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekaa kwenye kiti chake cha enzi kati ya makerubi. Nao wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, walikuwako huko pamoja na Sanduku la Agano la Mungu.
Le peuple envoya donc à Silo, d'où l'on apporta l'arche de l'alliance de l'Éternel des armées, qui habite entre les chérubins; et les deux fils d'Héli, Hophni et Phinées, y étaient avec l'arche de l'alliance de Dieu.
5 Wakati Sanduku la Agano la Bwana lilikuja kambini, Waisraeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu hata ardhi ikatikisika.
Et comme l'arche de l'Éternel entrait au camp, tout Israël jeta de si grands cris de joie, que la terre en retentit.
6 Wafilisti waliposikia makelele wakauliza, “Ni nini makelele haya yote katika kambi ya Waebrania?” Walipofahamu kuwa Sanduku la Bwana limekuja kambini,
Et les Philistins, entendant le bruit des cris de joie, dirent: Que veulent dire ces grands cris de joie au camp des Hébreux? Et ils surent que l'arche de l'Éternel était venue au camp.
7 Wafilisti wakaogopa, wakasema, “Mungu amekuja kambini, ole wetu. Halijatokea jambo kama hili tangu hapo.
Et les Philistins eurent peur, car ils disaient: Dieu est venu au camp; et ils dirent: Malheur à nous! car il n'en était pas ainsi ces jours passés;
8 Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka mikononi mwa miungu hii yenye nguvu? Ni miungu ile iliyowapiga Wamisri kwa mapigo ya aina zote huko jangwani.
Malheur à nous! qui nous délivrera de la main de ces Dieux puissants? Ce sont ces Dieux qui ont frappé les Égyptiens de toute sorte de plaies au désert.
9 Tuweni hodari, enyi Wafilisti! Tuweni wanaume, la sivyo mtakuwa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa kwenu. Kuweni wanaume, mpigane!”
Philistins, renforcez-vous, et agissez en hommes, de peur que vous ne soyez esclaves des Hébreux, comme ils ont été les vôtres; soyez donc hommes, et combattez.
10 Basi Wafilisti wakapigana, nao Waisraeli wakashindwa na kila mtu akakimbilia hemani mwake. Mauaji yalikuwa makubwa sana, Israeli wakapoteza askari 30,000 waendao kwa miguu.
Les Philistins combattirent donc, et Israël fut battu, et chacun s'enfuit en sa tente; la défaite fut très grande, et trente mille hommes de pied d'Israël y périrent.
11 Sanduku la Mungu likatekwa, na hao wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakauawa.
Et l'arche de Dieu fut prise; et les deux fils d'Héli, Hophni et Phinées, moururent.
12 Siku ile ile mtu mmoja wa kabila la Benyamini akakimbia kutoka kwenye uwanja wa vita na kwenda Shilo, nguo zake zikiwa zimeraruka na akiwa na mavumbi kichwani mwake.
Or, un homme de Benjamin s'enfuit de la bataille, et arriva à Silo ce jour-là, les vêtements déchirés, et de la poussière sur la tête;
13 Alipofika, Eli alikuwa ameketi juu ya kiti chake kando ya barabara akiangalia, kwa sababu moyo wake ulikuwa na hofu kwa ajili ya Sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kueleza kilichokuwa kimetokea, mji wote ukalia.
Et comme il arrivait, voici, Héli était assis sur son siège à côté du chemin, en attente; car son cœur tremblait à cause de l'arche de Dieu. Cet homme entra donc dans la ville pour porter ces nouvelles, et toute la ville se mit à crier.
14 Eli akasikia kelele za kilio, naye akauliza, “Ni nini maana ya makelele haya?” Yule mtu akafanya haraka kwenda kwa Eli,
Et Héli, entendant ces clameurs, dit: Que veut dire ce bruit, ce tumulte? Et cet homme, se hâtant, vint à Héli, et lui raconta tout.
15 wakati huu Eli alikuwa na miaka tisini na minane nayo macho yake yalikuwa yamepofuka na hakuweza kuona.
Or, Héli était âgé de quatre-vingt-dix-huit ans, et ses yeux étaient fixes, et il ne pouvait plus voir.
16 Akamwambia Eli, “Mimi nimetoka vitani sasa hivi, nimekimbia kutoka huko leo hii.” Eli akamuuliza, “Je, mwanangu, ni nini kimetokea huko?”
L'homme dit donc à Héli: C'est moi qui viens de la bataille; et je me suis échappé de la bataille aujourd'hui. Et Héli dit: Qu'est-il arrivé, mon fils?
17 Yule mtu aliyeleta habari akajibu, “Israeli amekimbia mbele ya Wafilisti, nalo jeshi limepata hasara kubwa. Pia wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa, na Sanduku la Mungu limetekwa.”
Et celui qui apportait les nouvelles répondit, et dit: Israël a fui devant les Philistins; et même il y a eu une grande défaite parmi le peuple, et tes deux fils, Hophni et Phinées, sont morts aussi, et l'arche de Dieu a été prise.
18 Mara alipotaja Sanduku la Mungu, Eli alianguka kutoka kwenye kiti chake kwa nyuma kando ya lango. Shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa kuwa alikuwa mzee tena mzito. Alikuwa amewaongoza Israeli kwa miaka arobaini.
Et dès qu'il eut fait mention de l'arche de Dieu, Héli tomba à la renverse de dessus son siège, à côté de la porte, et il se rompit le cou, et mourut; car c'était un homme vieux et pesant. Il avait jugé Israël quarante ans.
19 Mkwewe, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito na karibu wakati wa kujifungua. Aliposikia habari kwamba Sanduku la Mungu limetekwa na ya kuwa baba mkwe wake na mumewe wamekufa, akapata utungu naye akajifungua lakini akazidiwa na utungu.
Et sa belle-fille, femme de Phinées, qui était enceinte et sur le point d'accoucher, ayant appris la nouvelle que l'arche de Dieu était prise, et que son beau-père et son mari étaient morts, s'affaissa et enfanta; car les douleurs lui survinrent.
20 Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wanamhudumia wakamwambia, “Usikate tamaa, umemzaa mwana.” Lakini hakujibu wala kuweka maanani.
Et comme elle se mourait, celles qui étaient près d'elle, lui dirent: Ne crains point; car tu as enfanté un fils. Mais elle ne répondit rien, et n'y fit aucune attention.
21 Alimwita yule mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,” kwa sababu ya kutekwa kwa Sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na mumewe.
Et elle nomma l'enfant Icabod (sans gloire), en disant: La gloire est ôtée d'Israël; parce que l'arche de l'Éternel était prise, et à cause de son beau-père et de son mari.
22 Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa Sanduku la Mungu limetekwa.”
Elle dit donc: La gloire est ôtée d'Israël; car l'arche de Dieu est prise.

< 1 Samweli 4 >