< 1 Samweli 4 >

1 Nalo neno la Samweli likaja kwa Israeli yote. Basi Waisraeli walitoka kwenda kupigana dhidi ya Wafilisti. Waisraeli wakapiga kambi huko Ebenezeri, nao Wafilisti wakapiga kambi huko Afeki.
Or ce que Samuel avait dit, arriva à tout Israël; car Israël sortit en bataille pour aller à la rencontre des Philistins, et se campa près d'Eben-hézer, et les Philistins se campèrent en Aphek.
2 Wafilisti wakapanga safu za majeshi yao kupambana na Israeli, wakati vita vilipoenea, Israeli wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua askari wa Israeli wapatao 4,000 kwenye uwanja wa vita.
Et les Philistins se rangèrent en bataille pour aller à la rencontre d'Israël, et quand on fut dans la mêlée, Israël fut battu devant les Philistins, qui en tuèrent environ quatre mille hommes en la bataille par la campagne.
3 Askari waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakawauliza, “Kwa nini Bwana ameruhusu leo tushindwe mbele ya Wafilisti? Tuleteni Sanduku la Agano la Bwana kutoka Shilo, ili lipate kwenda pamoja nasi, na kutuokoa kutoka mikono ya adui zetu.”
Et le peuple étant revenu au camp, les Anciens d'Israël dirent: Pourquoi l'Eternel nous a-t-il battus aujourd'hui devant les Philistins; faisons-nous amener de Silo l'Arche de l'alliance de l'Eternel, et qu'il vienne au milieu de nous, et nous délivre de la main de nos ennemis.
4 Hivyo wakawatuma watu huko Shilo, nao wakalichukua Sanduku la Agano la Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekaa kwenye kiti chake cha enzi kati ya makerubi. Nao wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, walikuwako huko pamoja na Sanduku la Agano la Mungu.
Le peuple donc envoya à Silo, et on apporta de là l'Arche de l'alliance de l'Eternel des armées, qui habite entre les Chérubins; et là étaient les deux fils d'Héli, Hophni, et Phinées, avec l'Arche de l'alliance de Dieu.
5 Wakati Sanduku la Agano la Bwana lilikuja kambini, Waisraeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu hata ardhi ikatikisika.
Et il arriva que comme l'Arche de l'Eternel entrait au camp, tout Israël se mit à jeter de si grands cris de joie, que la terre en retentissait.
6 Wafilisti waliposikia makelele wakauliza, “Ni nini makelele haya yote katika kambi ya Waebrania?” Walipofahamu kuwa Sanduku la Bwana limekuja kambini,
Et les Philistins entendant le bruit de ces cris de joie, dirent: Que veut dire ce bruit, [et que signifient] ces grands cris de joie au camp de ces Hébreux? et ils surent que l'Arche de l'Eternel était venue au camp.
7 Wafilisti wakaogopa, wakasema, “Mungu amekuja kambini, ole wetu. Halijatokea jambo kama hili tangu hapo.
Et les Philistins eurent peur, parce qu'on disait: Dieu est venu au camp; et ils dirent: Malheur à nous! car ceci n'a pas été aux jours passés.
8 Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka mikononi mwa miungu hii yenye nguvu? Ni miungu ile iliyowapiga Wamisri kwa mapigo ya aina zote huko jangwani.
Malheur à nous! Qui nous délivrera de la main de ces Dieux-là si glorieux? Ce sont ces Dieux qui ont frappé les Egyptiens au désert, outre toutes les autres plaies.
9 Tuweni hodari, enyi Wafilisti! Tuweni wanaume, la sivyo mtakuwa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa kwenu. Kuweni wanaume, mpigane!”
Philistins renforcez-vous, et soyez hommes, de peur que vous ne soyez asservis aux Hébreux, comme ils vous ont été asservis; soyez donc hommes, et combattez.
10 Basi Wafilisti wakapigana, nao Waisraeli wakashindwa na kila mtu akakimbilia hemani mwake. Mauaji yalikuwa makubwa sana, Israeli wakapoteza askari 30,000 waendao kwa miguu.
Les Philistins donc combattirent, et les Israëlites furent battus, et s'enfuirent chacun en sa tente; et il y eut une fort grande défaite, [car] il y demeura d'Israël trente mille hommes de pied.
11 Sanduku la Mungu likatekwa, na hao wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakauawa.
Et l'Arche de Dieu fut prise, et les deux fils d'Héli, Hophni et Phinées, moururent.
12 Siku ile ile mtu mmoja wa kabila la Benyamini akakimbia kutoka kwenye uwanja wa vita na kwenda Shilo, nguo zake zikiwa zimeraruka na akiwa na mavumbi kichwani mwake.
Or un homme de Benjamin s'enfuit de la bataille, et arriva à Silo ce même jour-là, ayant ses vêtements déchirés, et de la terre sur sa tête.
13 Alipofika, Eli alikuwa ameketi juu ya kiti chake kando ya barabara akiangalia, kwa sababu moyo wake ulikuwa na hofu kwa ajili ya Sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kueleza kilichokuwa kimetokea, mji wote ukalia.
Et comme il arrivait, voici, Héli était assis sur un siège à côté du chemin, étant attentif; car son cœur tremblait à cause de l'Arche de Dieu. Cet homme-là donc vint portant les nouvelles dans la ville, et toute la ville se mit à crier.
14 Eli akasikia kelele za kilio, naye akauliza, “Ni nini maana ya makelele haya?” Yule mtu akafanya haraka kwenda kwa Eli,
Et Héli entendant le bruit de ce cri, dit: Que veut dire ce grand tumulte? et cet homme se hâtant vint à Héli, et [lui] raconta [tout].
15 wakati huu Eli alikuwa na miaka tisini na minane nayo macho yake yalikuwa yamepofuka na hakuweza kuona.
Or Héli était âgé de quatre vingt dix-huit ans; et ses yeux étaient tout ternis, et il ne pouvait voir.
16 Akamwambia Eli, “Mimi nimetoka vitani sasa hivi, nimekimbia kutoka huko leo hii.” Eli akamuuliza, “Je, mwanangu, ni nini kimetokea huko?”
Cet homme-là donc dit à Héli: Je suis celui qui viens de la bataille, car je me suis aujourd'hui échappé de la bataille. Et [Héli] dit: Qu'y est-il arrivé, mon fils?
17 Yule mtu aliyeleta habari akajibu, “Israeli amekimbia mbele ya Wafilisti, nalo jeshi limepata hasara kubwa. Pia wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa, na Sanduku la Mungu limetekwa.”
Et celui qui portait les nouvelles répondit, et dit: Israël a fui devant les Philistins, et même il y a eu une grande défaite du peuple; et tes deux fils, Hophni et Phinées, sont morts, et l'Arche de Dieu a été prise.
18 Mara alipotaja Sanduku la Mungu, Eli alianguka kutoka kwenye kiti chake kwa nyuma kando ya lango. Shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa kuwa alikuwa mzee tena mzito. Alikuwa amewaongoza Israeli kwa miaka arobaini.
Et il arriva qu'aussitôt qu'il eut fait mention de l'Arche de Dieu, [Héli] tomba à la renverse de dessus son siège à côté de la porte, et se rompit la nuque du cou, et mourut; car cet homme était vieux et pesant. Or il avait jugé Israël quarante ans.
19 Mkwewe, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito na karibu wakati wa kujifungua. Aliposikia habari kwamba Sanduku la Mungu limetekwa na ya kuwa baba mkwe wake na mumewe wamekufa, akapata utungu naye akajifungua lakini akazidiwa na utungu.
Et sa belle-fille, femme de Phinées, qui était grosse, [et] sur le point d'accoucher, ayant appris la nouvelle que l'Arche de Dieu était prise, et que son beau-père et son mari étaient morts, se courba et enfanta; car ses douleurs lui étaient survenues.
20 Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wanamhudumia wakamwambia, “Usikate tamaa, umemzaa mwana.” Lakini hakujibu wala kuweka maanani.
Et comme elle mourait, celles qui l'assistaient, lui dirent: Ne crains point; car tu as enfanté un fils; mais elle ne répondit rien, et n'en tint point de compte.
21 Alimwita yule mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,” kwa sababu ya kutekwa kwa Sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na mumewe.
Mais elle nomma l'enfant I-Cabod, en disant: La gloire de l'Eternel est transportée d'Israël; parce que l'Arche de l'Eternel était prise, et à cause de son beau-père et de son mari.
22 Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa Sanduku la Mungu limetekwa.”
Elle dit donc: La gloire est transportée d'Israël; car l'Arche de Dieu est prise.

< 1 Samweli 4 >