< 1 Samweli 4 >

1 Nalo neno la Samweli likaja kwa Israeli yote. Basi Waisraeli walitoka kwenda kupigana dhidi ya Wafilisti. Waisraeli wakapiga kambi huko Ebenezeri, nao Wafilisti wakapiga kambi huko Afeki.
And the word of Samuel came to all Israel. Now Israel went out against the Philistines to battle, and pitched beside Eben-ezer; and the Philistines pitched in Aphek.
2 Wafilisti wakapanga safu za majeshi yao kupambana na Israeli, wakati vita vilipoenea, Israeli wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua askari wa Israeli wapatao 4,000 kwenye uwanja wa vita.
And the Philistines put themselves in array against Israel; and when the battle was spread, Israel was smitten before the Philistines; and they slew of the army in the field about four thousand men.
3 Askari waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakawauliza, “Kwa nini Bwana ameruhusu leo tushindwe mbele ya Wafilisti? Tuleteni Sanduku la Agano la Bwana kutoka Shilo, ili lipate kwenda pamoja nasi, na kutuokoa kutoka mikono ya adui zetu.”
And when the people were come into the camp, the elders of Israel said: 'Wherefore hath the LORD smitten us to-day before the Philistines? Let us fetch the ark of the covenant of the LORD out of Shiloh unto us, that He may come among us, and save us out of the hand of our enemies.'
4 Hivyo wakawatuma watu huko Shilo, nao wakalichukua Sanduku la Agano la Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekaa kwenye kiti chake cha enzi kati ya makerubi. Nao wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, walikuwako huko pamoja na Sanduku la Agano la Mungu.
So the people sent to Shiloh, and they brought from thence the ark of the covenant of the LORD of hosts, who sitteth upon the cherubim; and the two sons of Eli, Hophni and Phinehas, were there with the ark of the covenant of God.
5 Wakati Sanduku la Agano la Bwana lilikuja kambini, Waisraeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu hata ardhi ikatikisika.
And when the ark of the covenant of the LORD came into the camp, all Israel shouted with a great shout, so that the earth rang.
6 Wafilisti waliposikia makelele wakauliza, “Ni nini makelele haya yote katika kambi ya Waebrania?” Walipofahamu kuwa Sanduku la Bwana limekuja kambini,
And when the Philistines heard the noise of the shout, they said: 'What meaneth the noise of this great shout in the camp of the Hebrews?' And they knew that the ark of the LORD was come into the camp.
7 Wafilisti wakaogopa, wakasema, “Mungu amekuja kambini, ole wetu. Halijatokea jambo kama hili tangu hapo.
And the Philistines were afraid, for they said: 'God is come into the camp.' And they said: 'Woe unto us! for there was not such a thing yesterday and the day before.
8 Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka mikononi mwa miungu hii yenye nguvu? Ni miungu ile iliyowapiga Wamisri kwa mapigo ya aina zote huko jangwani.
Woe unto us! who shall deliver us out of the hand of these mighty gods? these are the gods that smote the Egyptians with all manner of plagues and in the wilderness.
9 Tuweni hodari, enyi Wafilisti! Tuweni wanaume, la sivyo mtakuwa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa kwenu. Kuweni wanaume, mpigane!”
Be strong, and quit yourselves like men, O ye Philistines, that ye be not servants unto the Hebrews, as they have been to you; quit yourselves like men, and fight.'
10 Basi Wafilisti wakapigana, nao Waisraeli wakashindwa na kila mtu akakimbilia hemani mwake. Mauaji yalikuwa makubwa sana, Israeli wakapoteza askari 30,000 waendao kwa miguu.
And the Philistines fought, and Israel was smitten, and they fled every man to his tent; and there was a very great slaughter; for there fell of Israel thirty thousand footmen.
11 Sanduku la Mungu likatekwa, na hao wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakauawa.
And the ark of God was taken; and the two sons of Eli, Hophni and Phinehas, were slain.
12 Siku ile ile mtu mmoja wa kabila la Benyamini akakimbia kutoka kwenye uwanja wa vita na kwenda Shilo, nguo zake zikiwa zimeraruka na akiwa na mavumbi kichwani mwake.
And there ran a man of Benjamin out of the army, and came to Shiloh the same day with his clothes rent, and with earth upon his head.
13 Alipofika, Eli alikuwa ameketi juu ya kiti chake kando ya barabara akiangalia, kwa sababu moyo wake ulikuwa na hofu kwa ajili ya Sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kueleza kilichokuwa kimetokea, mji wote ukalia.
And when he came, lo, Eli sat upon his seat by the wayside watching; for his heart trembled for the ark of God. And when the man came into the city, and told it, all the city cried out.
14 Eli akasikia kelele za kilio, naye akauliza, “Ni nini maana ya makelele haya?” Yule mtu akafanya haraka kwenda kwa Eli,
And when Eli heard the noise of the crying, he said: 'What meaneth the noise of this tumult?' And the man made haste, and came and told Eli.
15 wakati huu Eli alikuwa na miaka tisini na minane nayo macho yake yalikuwa yamepofuka na hakuweza kuona.
Now Eli was ninety and eight years old; and his eyes were set, that he could not see.
16 Akamwambia Eli, “Mimi nimetoka vitani sasa hivi, nimekimbia kutoka huko leo hii.” Eli akamuuliza, “Je, mwanangu, ni nini kimetokea huko?”
And the man said unto Eli: 'I am he that came out of the army, and I fled to-day out of the army.' And he said: 'How went the matter, my son?'
17 Yule mtu aliyeleta habari akajibu, “Israeli amekimbia mbele ya Wafilisti, nalo jeshi limepata hasara kubwa. Pia wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa, na Sanduku la Mungu limetekwa.”
And he that brought the tidings answered and said: 'Israel is fled before the Philistines, and there hath been also a great slaughter among the people, and thy two sons also, Hophni and Phinehas, are dead, and the ark of God is taken.'
18 Mara alipotaja Sanduku la Mungu, Eli alianguka kutoka kwenye kiti chake kwa nyuma kando ya lango. Shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa kuwa alikuwa mzee tena mzito. Alikuwa amewaongoza Israeli kwa miaka arobaini.
And it came to pass, when he made mention of the ark of God, that he fell from off his seat backward by the side of the gate, and his neck broke, and he died; for he was an old man, and heavy. And he had judged Israel forty years.
19 Mkwewe, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito na karibu wakati wa kujifungua. Aliposikia habari kwamba Sanduku la Mungu limetekwa na ya kuwa baba mkwe wake na mumewe wamekufa, akapata utungu naye akajifungua lakini akazidiwa na utungu.
And his daughter-in-law, Phinehas' wife, was with child, near to be delivered; and when she heard the tidings that the ark of God was taken, and that her father-in-law and her husband were dead, she bowed herself and brought forth; for her pains came suddenly upon her.
20 Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wanamhudumia wakamwambia, “Usikate tamaa, umemzaa mwana.” Lakini hakujibu wala kuweka maanani.
And about the time of her death the women that stood by her said unto her: 'Fear not; for thou hast brought forth a son.' But she answered not, neither did she regard it.
21 Alimwita yule mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,” kwa sababu ya kutekwa kwa Sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na mumewe.
And she named the child Ichabod, saying: 'The glory is departed from Israel'; because the ark of God was taken, and because of her father-in-law and her husband.
22 Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa Sanduku la Mungu limetekwa.”
And she said: 'The glory is departed from Israel; for the ark of God is taken.'

< 1 Samweli 4 >