< 1 Samweli 31 >

1 Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa.
Los filisteos atacaron a Israel, y los hombres de Israel huyeron en fuga ante los filisteos, cayendo muertos en el monte Gilboa.
2 Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
Y los filisteos tomaron a Saúl y sus hijos; y mataron a Jonatán, a Abinadab y a Malquisua, los hijos de Saúl.
3 Mapigano yakawa makali sana kumzunguka Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.
Y la lucha iba mal para Saúl, y los arqueros se cruzaron con él y fue herido por los arqueros.
4 Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
Entonces Saúl dijo al siervo su escudero: Saca tu espada y pásala a través de mí, antes de que estos hombres sin circuncisión vengan y se burlen de mí. Pero su sirviente, lleno de miedo, no lo hizo. Entonces Saúl sacó su espada y cayendo sobre ella, se puso fin a sí mismo.
5 Mchukua silaha wake alipoona Sauli amekufa, naye pia akaangukia upanga wake akafa pamoja naye.
Y cuando su criado vio que Saúl estaba muerto, él hizo lo mismo, y se unió a él en la muerte.
6 Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.
Entonces la muerte alcanzó a Saúl y sus tres hijos y su siervo el mismo día.
7 Waisraeli waliokuwa kandokando ya bonde na wale waliokuwa ngʼambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
Y cuando los hombres de Israel cruzaron el valle y al otro lado del Jordán vieron que el ejército de Israel estaba huyendo y que Saúl y sus hijos estaban muertos, salieron de sus ciudades y huyeron; Y vinieron los filisteos y los tomaron para sí mismos.
8 Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa.
Al día siguiente, cuando los filisteos vinieron a sacar sus bienes de los muertos, vieron a Saúl y sus tres hijos muertos en la tierra en el monte Gilboa.
9 Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao.
Y cortándole la cabeza y quitándole el traje de guerra, enviaron un mensaje a la tierra de los filisteos por todas partes, para llevar las noticias a sus dioses y al pueblo.
10 Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.
Se pusieron sus ropas de guerra en la casa de Astarté. y su cuerpo fue fijado en la pared de Beth-san.
11 Watu wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yale Wafilisti walichomfanyia Sauli,
Y cuando los habitantes de Jabes-galaad tuvieron noticias de lo que los filisteos habían hecho a Saúl,
12 mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, mahali ambapo waliiteketeza kwa moto.
Se levantaron todos los fuertes y valientes, viajando toda la noche, tomaron el cuerpo de Saúl y los cuerpos de sus hijos del muro de Bet-sán; y viniendo a Jabes y los quemaron allí.
13 Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga siku saba.
Y tomando los huesos lo enterraron debajo del árbol tamarisco en Jabes; Y por siete días guardaron ayuno.

< 1 Samweli 31 >