< 1 Samweli 31 >

1 Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa.
Torej Filistejci so se borili zoper Izrael in Izraelci so pobegnili pred Filistejci in padli dol, umorjeni na gori Gilbói.
2 Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
Filistejci so tesno sledili Savlu in njegovim sinovom in Filistejci so usmrtili Jonatana, Abinadába in Malkišúa, Savlove sinove.
3 Mapigano yakawa makali sana kumzunguka Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.
Bitka je postala huda zoper Savla in lokostrelci so ga zadeli; in bil je hudo ranjen od lokostrelcev.
4 Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
Potem je Savel rekel svojemu nosilcu bojne opreme: »Izvleci svoj meč in me prebodi z njim; da ne bi prišli ti neobrezanci in me prebodli in me zlorabili.« Vendar njegov nosilec bojne opreme ni hotel, kajti bil je hudo prestrašen. Zato je Savel vzel meč in padel nanj.
5 Mchukua silaha wake alipoona Sauli amekufa, naye pia akaangukia upanga wake akafa pamoja naye.
Ko je njegov nosilec bojne opreme videl, da je bil Savel mrtev, je tudi sam prav tako padel na svoj meč in umrl z njim.
6 Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.
Tako so ta isti dan skupaj umrli Savel, njegovi trije sinovi, njegov nosilec bojne opreme in vsi njegovi možje.
7 Waisraeli waliokuwa kandokando ya bonde na wale waliokuwa ngʼambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
Ko so Izraelovi možje, ki so bili na drugi strani doline in tisti, ki so bili na drugi strani Jordana, videli, da so Izraelovi možje pobegnili in da so bili Savel in njegovi sinovi mrtvi, so zapustili mesta in pobegnili in Filistejci so prišli ter prebivali v njih.
8 Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa.
Pripetilo se je naslednji dan, ko so prišli Filistejci, da oropajo umorjene, da so našli Savla in njegove tri sinove padle na gori Gilbói.
9 Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao.
Odsekali so njegovo glavo, slekli njegovo bojno opremo in poslali naokoli, v deželo Filistejcev, da to razglasijo v hiši njihovih malikov in med ljudstvom.
10 Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.
Njegovo bojno opremo so položili v hišo Astarte. Njegovo telo pa so pritrdili na obzidje Bet Šeána.
11 Watu wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yale Wafilisti walichomfanyia Sauli,
Ko so prebivalci Jabéš Gileáda slišali o tem, kar so Filistejci storili Savlu,
12 mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, mahali ambapo waliiteketeza kwa moto.
so se vsi hrabri možje vzdignili in hodili vso noč in vzeli Savlovo telo in telesa njegovih sinov z obzidja Bet Šeána in prišli v Jabéš ter jih tam sežgali.
13 Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga siku saba.
In vzeli so njihove kosti in jih pokopali pod drevesom pri Jabéšu in se postili sedem dni.

< 1 Samweli 31 >