< 1 Samweli 31 >

1 Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa.
Or, les Philistins combattirent contre Israël, et les Israélites prirent la fuite devant les Philistins, et furent tués sur la montagne de Guilboa.
2 Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
Et les Philistins poursuivirent Saül et ses fils, et tuèrent Jonathan, Abinadab, et Malkishua, fils de Saül.
3 Mapigano yakawa makali sana kumzunguka Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.
Et l'effort du combat tomba sur Saül; et les archers l'atteignirent, et il fut dangereusement blessé par les archers.
4 Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
Alors Saül dit à son écuyer: Tire ton épée, et m'en transperce, de peur que ces incirconcis ne viennent, et ne me transpercent, et ne me fassent des outrages. Mais son écuyer ne le voulut point faire, car il était fort effrayé. Saül prit donc l'épée, et se jeta dessus.
5 Mchukua silaha wake alipoona Sauli amekufa, naye pia akaangukia upanga wake akafa pamoja naye.
Alors l'écuyer de Saül, voyant que Saül était mort, se jeta aussi sur son épée, et mourut avec lui.
6 Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.
Ainsi moururent en ce jour-là, Saül et ses trois fils, son écuyer et tous ses gens.
7 Waisraeli waliokuwa kandokando ya bonde na wale waliokuwa ngʼambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
Et ceux d'Israël qui étaient de ce côté-ci de la vallée, et de ce côté-ci du Jourdain, ayant vu que les Israélites s'étaient enfuis, et que Saül et ses fils étaient morts, abandonnèrent les villes et s'enfuirent; de sorte que les Philistins vinrent et y habitèrent.
8 Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa.
Et, le lendemain, les Philistins vinrent pour dépouiller les morts; et ils trouvèrent Saül et ses trois fils étendus sur la montagne de Guilboa.
9 Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao.
Et ils lui coupèrent la tête et le dépouillèrent de ses armes; et ils envoyèrent au pays des Philistins, de tous côtés, pour annoncer la nouvelle dans les temples de leurs idoles, et parmi le peuple.
10 Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.
Puis ils mirent ses armes au temple d'Ashtharoth, et pendirent son corps à la muraille de Beth-Shan.
11 Watu wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yale Wafilisti walichomfanyia Sauli,
Or, les habitants de Jabès de Galaad apprirent ce que les Philistins avaient fait à Saül;
12 mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, mahali ambapo waliiteketeza kwa moto.
Et tous les vaillants hommes se levèrent et marchèrent toute la nuit, et enlevèrent le corps de Saül et les corps de ses fils, de la muraille de Beth-Shan; et ils revinrent à Jabès, où ils les brûlèrent.
13 Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga siku saba.
Puis ils prirent leurs os, et les ensevelirent sous le tamarin, près de Jabès; et ils jeûnèrent sept jours.

< 1 Samweli 31 >