< 1 Samweli 30 >

1 Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
Lorsque David arriva avec ses hommes le troisième jour à Siceleg, les Amalécites avaient fait une invasion dans le Négéb et à Siceleg; ils avaient frappé Siceleg et l'avaient brûlée;
2 nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
et ils avaient fait prisonniers les femmes et tous ceux qui s'y trouvaient, petits et grands, sans tuer personne, et ils les avaient emmenés, et s'étaient remis en route.
3 Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
Lors donc que David et ses gens arrivèrent à la ville, ils virent qu'elle était brûlée, et que leurs femmes, leurs fils et leurs filles avaient été emmenés captifs.
4 Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
Et David et le peuple qui était avec lui élevèrent la voix et pleurèrent jusqu'à ce qu'ils n'eussent plus la force de pleurer.
5 Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
Les deux femmes de David avaient été aussi emmenées captives, Achinoam de Jezraël, et Abigaïl de Carmel, femme de Nabal.
6 Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
David fut dans une grande angoisse, car la troupe parlait de le lapider, parce que tout le peuple avait de l'amertume dans l'âme, chacun au sujet de ses fils et de ses filles. Mais David reprit courage en Yahweh, son Dieu.
7 Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
David dit au prêtre Abiathar, fils d'Achimélech: « Apporte-moi l'éphod. » Abiathar apporta l'éphod à David.
8 naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
Et David consulta Yahweh en disant: « Poursuivrai-je cette bande? L'atteindrai-je? » Yahweh lui répondit: « Poursuis, car certainement tu atteindras et tu délivreras. »
9 Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
Et David se mit en marche, lui et les six cents hommes qui étaient avec lui. Lorsqu'ils furent arrivés au torrent de Bésor, les traînards s'arrêtèrent.
10 kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
Et David continua la poursuite avec quatre cents hommes; deux cents hommes s'étaient arrêtés, trop fatigués pour passer le torrent de Bésor.
11 Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
Ils trouvèrent dans les champs un Egyptien, qu'ils amenèrent à David. Ils lui donnèrent du pain qu'il mangea, et ils lui firent boire de l'eau;
12 kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
ils lui donnèrent une tranche d'un gâteau de figues sèches et deux gâteaux de raisins secs. Dès qu'il eut pris de la nourriture, ses esprits lui revinrent, car il n'avait mangé de nourriture ni bu d'eau depuis trois jours et trois nuits.
13 Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
David lui dit: « A qui es-tu et d'où es-tu? » Il répondit: « Je suis un esclave égyptien, au service d'un Amalécite, et voilà trois jours que mon maître m'a abandonné, parce que j'étais malade.
14 Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
Nous avons fait une incursion dans le Négéb des Céréthiens, et sur le territoire de Juda, et dans le Négéb de Caleb, et nous avons brûlé Siceleg. »
15 Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
David lui dit: « Veux-tu me conduire vers cette bande? » Il répondit: « Jure-moi par le nom de Dieu que tu ne me tueras pas et que tu ne me livreras pas aux mains de mon maître, et je te conduirai vers cette bande. »
16 Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
Lorsqu'il l'eut conduit, voici que les Amalécites étaient répandus sur toute la contrée, mangeant, buvant et dansant, à cause de tout le grand butin qu'ils avaient enlevé du pays des Philistins et du pays de Juda.
17 Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
David les battit depuis le crépuscule du soir jusqu'au soir du lendemain, et aucun d'eux n'échappa, excepté quatre cents jeunes hommes, qui s'enfuirent, montés sur des chameaux.
18 Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
David sauva tout ce que les Amalécites avaient pris, et David sauva ses deux femmes.
19 Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
Il ne leur manqua personne, ni petit ni grand, ni fils ni fille, ni aucune partie du butin, ni rien de ce qu'on leur avait enlevé: David ramena tout.
20 Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
Et David prit tout le menu et le gros bétail, et ils se mirent en marche devant ce troupeau, en disant: « C'est le butin de David. »
21 Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
David revint vers les deux cents hommes qui avaient été trop fatigués pour suivre David, et qu'on avait laissés au torrent de Bésor; ils s'avancèrent au-devant de David et au-devant du peuple qui était avec lui. S'approchant d'eux, David les salua amicalement.
22 Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
Tout ce qu'il y avait d'hommes méchants et vils parmi les gens qui étaient allés avec David prirent la parole et dirent: « Puisqu'ils ne sont pas venus avec nous, nous ne leur donnerons rien du butin que nous avons sauvé, sinon à chacun sa femme et ses enfants; qu'ils les emmènent et s'en aillent. »
23 Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
Mais David dit: « N'agissez pas ainsi, mes frères, avec ce que Yahweh nous a donné; car il nous a gardés, et il a livré entre nos mains la bande qui était venue contre nous.
24 Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
Et qui vous écouterait dans cette affaire? La part doit être la même pour celui qui est descendu au combat et pour celui qui est resté près des bagages: ils partageront ensemble. »
25 Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
Il en fut ainsi dès ce jour et dans la suite, et David a fait de cela une loi et une règle qui subsiste jusqu'à ce jour.
26 Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
De retour à Siceleg, David envoya une partie du butin aux anciens de Juda, ses amis, en disant: « Voici un présent pour vous sur le butin des ennemis de Yahweh. »
27 Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
Il fit ces envois à ceux de Béthel, à ceux de Ramoth du Négéb, à ceux de Jéther,
28 kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
à ceux d'Aroër, à ceux de Séphamoth, à ceux d'Estamo,
29 na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
à ceux de Rachal, à ceux des villes de Jéraméélites, à ceux des villes des Cinéens,
30 na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
à ceux d'Arama, à ceux de Cor-Asan, à ceux d'Athach,
31 na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.
à ceux d'Hébron et dans tous les lieux où David et ses gens avaient passé.

< 1 Samweli 30 >