< 1 Samweli 30 >
1 Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
And it comes to pass, in the coming in of David and his men to Ziklag on the third day, that the Amalekites have pushed toward the south, and to Ziklag, and strike Ziklag, and burn it with fire,
2 nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
and they take the women who [are] in it captive; they have not put anyone to death from small to great, and they lead [them] away, and go on their way.
3 Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
And David comes in—and his men—to the city, and behold, [it is] burned with fire, and their wives, and their sons, and their daughters have been taken captive.
4 Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
And David lifts up—and the people who [are] with him—their voice and weep, until they have no power to weep.
5 Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
And the two wives of David have been taken captive, Ahinoam the Jezreelitess, and Abigail wife of Nabal the Carmelite;
6 Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
and David has great distress, for the people have said to stone him, for the soul of all the people has been bitter, each for his sons and for his daughters; and David strengthens himself in his God YHWH.
7 Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
And David says to Abiathar the priest, son of Ahimelech, “Please bring the ephod near to me”; and Abiathar brings the ephod near to David,
8 naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
and David inquires of YHWH, saying, “I pursue after this troop—do I overtake it?” And He says to him, “Pursue, for you certainly overtake, and certainly deliver.”
9 Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
And David goes on, he and six hundred men who [are] with him, and they come to the Brook of Besor, and those left have stood still,
10 kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
and David pursues, he and four hundred men (and two hundred men stand still who have been too faint to pass over the Brook of Besor),
11 Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
and they find a man, an Egyptian, in the field, and take him to David, and give bread to him, and he eats, and they cause him to drink water,
12 kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
and give to him a piece of a bunch of dried figs, and two bunches of raisins, and he eats, and his spirit returns to him, for he has not eaten bread nor drunk water [for] three days and three nights.
13 Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
And David says to him, “Whose [are] you? And where [are] you from?” And he says, “I [am] an Egyptian youth, servant to a man, an Amalekite, and my lord forsakes me, for I have been sick [for] three days,
14 Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
we pushed [to] the south of the Cherethite, and against that which [is] to Judah, and against the south of Caleb, and we burned Ziklag with fire.”
15 Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
And David says to him, “Do you bring me down to this troop?” And he says, “Swear to me by God [that] you do not put me to death, nor do you shut me up into the hand of my lord, and I bring you down to this troop.”
16 Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
And he brings him down, and behold, they are spread out over the face of all the earth, eating, and drinking, and celebrating, with all the great spoil which they have taken out of the land of the Philistines, and out of the land of Judah.
17 Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
And David strikes them from the twilight even to the evening of the next day, and there has not escaped of them a man, except four hundred young men who have ridden on the camels and flee.
18 Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
And David delivers all that the Amalekites have taken; David has also delivered his two wives.
19 Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
And nothing of theirs has lacked, from small to great, and to sons and daughters, and from the spoil, even to all that they had taken to themselves, David has brought back the whole,
20 Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
and David takes the whole of the flock and of the herd [that] they have led on before these livestock, and they say, “This [is] David’s spoil.”
21 Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
And David comes to the two hundred men who were too faint to go after David, and whom they cause to abide at the Brook of Besor, and they go out to meet David, and to meet the people who [are] with him, and David approaches the people, and asks of them of welfare.
22 Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
And every bad and worthless man, of the men who have gone with David, answers, indeed, they say, “Because that they have not gone with us we do not give to them of the spoil which we have delivered, except each his wife and his children, and they lead away and go.”
23 Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
And David says, “You do not do so, my brothers, with that which YHWH has given to us, and He preserves us, and gives the troop which comes against us into our hand;
24 Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
and who listens to you in this thing? For as the portion of him who was brought down into battle, so also [is] the portion of him who is abiding by the vessels—they share alike.”
25 Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
And it comes to pass from that day and forward, that he appoints it for a statute and for an ordinance for Israel to this day.
26 Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
And David comes to Ziklag, and sends of the spoil to [the] elderly of Judah, to his friends, saying, “Behold, a blessing for you of the spoil of the enemies of YHWH,”
27 Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
to those in Beth-El, and to those in South Ramoth, and to those in Jattir,
28 kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
and to those in Aroer, and to those in Siphmoth, and to those in Eshtemoa,
29 na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
and to those in Rachal, and to those in the cities of the Jerahmeelites, and to those in the cities of the Kenites,
30 na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
and to those in Hormah, and to those in Chor-Ashan, and to those in Athach,
31 na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.
and to those in Hebron, and to all the places where David—he and his men—had gone up and down.