< 1 Samweli 3 >

1 Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
Mek'vne Şamuelee, Eliyne k'ane Rəbbis k'ılyvalla ha'a vuxha. Mane gahbışil Rəbbin cuvabıy gyaguybı zarada-zarada eyxhenbı deşdiy.
2 Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
Sa xəmde Eliy cune tyulee g'alirxhu ıxha. Mang'une uleppışik'le yugda g'ece ıxha deş.
3 Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
Şamuelymee Rəbbine xaa g'alirxhu eyxhe. Allahna q'utyeb mane xaa vuxha. Maana Allahna bazirıb k'əpq'ı' vuxha deş.
4 Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
Rəbbee Şamuelilqa ona'a, mang'veeyir «İnyaa vorva» alidghıniy qele.
5 Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
Qiyğar Eliyne k'anyaqa g'adarxhun «Zalqa onu'iynne, zı inyaa vorva» uvhu. Eliyeemee «Zı onu'u deş, hoora g'alixheva» eyhe. Şamuelir ark'ın g'ılexhana.
6 Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
Rəbbee «Şamuelyva» meed ona'an. Şamuel meer oza qıxha Eliyne k'anyaqa ark'ın «Zalqa onu'iynne? Zı inyaa vorva!» eyhe. Eliyee «Zı onu'u deş. Dix, hoora g'alixheva» alidghıniy qele.
7 Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
Şamuelik'le manke Rəbb ats'a deşdiy, Rəbbee mang'us cuvabıd aaqı deşdiy.
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
Rəbbee xhebe'es Şamuelilqa onu'umee, mana tyuleençe suğotsu Eliyne k'anyaqa ark'ın, eyhen: – Ğu zalqa onu'uva, zı inyaa vor. Manke Eliylqa hiyxharan, mek'vne Şamuelilqa onu'una Rəbb ıxhava.
9 Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
Mançil-allad Şamuelik'le eyhen: – Hoora g'alixhe, meed valqa one'ee, inəxüd eyhe: «Yuşan he'e, ya Rəbb, Yiğne g'ulee k'ırı iliyxhe vod.» Şamuelir ark'ın cune tyuleqa k'eç'ena.
10 Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
Rəbb arı maa'ar ulyorzul şene ögiylin xhinne «Şamuel! Şamuelyva!» ona'anan. Şamuelee eyhen: – Yuşan he'e, ya Rəbb, Yiğne g'ulee k'ırı iliyxhe vod.
11 Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
Rəbbee Şamuelik'le inəxüd eyhe: – Zı İzrailil məxbına iş g'avces, g'ayxhiyng'un k'ırı g'avayghas.
12 Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
Mane yiğıl, Eliyne xizanne hək'ee uvhuyn gırgın, Zı qomançe k'anyaqqamee ha'asın.
13 Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
Zı cuk'le uvhunniy, cuk'le ats'ane bınahbışil-alla Zı cune xizanıs gırgıne gahbışisda cazaa hevles. Mang'une dixbışe Zı g'eliqqa huvu. Eliyeemee manbışin ögü ı'xı' deş.
14 Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
Zı mançil-allad Eliyne xizanıs k'ınniy g'assır: Eliyne xizanne bınahıle q'urbanıkayiy menne-menne ıkekkane karbışika ılyheç'es deş.
15 Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
Şamuel miç'eerilqamee g'ılexhana, qiyğar oza qıxha Rəbbine xaan akkabı aaqa. Mana cus Allahee gyagu'iyn kar Eliys yuşan ha'as qəyq'ənna.
16 lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
Eliyeemee mang'ulqa onu'u eyhen: – Şamuel, yizda dix. Şamueleeyid «Zı inyaa vorva» mang'us alidghıniy qele.
17 Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
Eliyee mang'uke qiyghanan: – Rəbbee vak'le hucoovana uvhu? Hucoona ixhes, man zale dyugul hıma'a. Allahee vak'le uvhuynçin, ğu zale saxheeyid dyugul he'ee, hasre Mang'vee vak divan qaqqecen.
18 Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
Şamuelee mang'us gırgın yuşan ha'an, vuççud dyugul ha'a deş. Eliyeeme eyhen: – Mana Rəbb vorna, hasre Cus nəxüdiy ıkkan həməxüdud he'ecen.
19 Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
Şamuel xər qexhe. Rəbb mang'uka ıxha, Rəbbee Şamuelik'le uvhuyn gırgın kar eyxhen.
20 Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
Rəbbee Şamuelike hək'erar peyğambar hı'iy, gırgıne İzrailik'lecad Danile Beer-Şevalqamee ats'axhxhen.
21 Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.
Rəbb meer Şiloyee gyagva giyğal. Mang'vee Cune cuvabıka Vucecar Vuc Şamuelik'le hagva.

< 1 Samweli 3 >