< 1 Samweli 3 >

1 Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
Nagserbi ti ubing a ni Samuel kenni Yahweh babaen iti panangidalan ni Eli. Manmano ti sao ni Yahweh kadagidiay nga al-aldaw; awan unay ti sirmata maipanggep iti masakbayan.
2 Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
Iti dayta a tiempo, idi ni Eli nga agkapsuten ti panagkitana a saan unayen a makakita, ket agid-idda iti bukodna a pagiddaan,
3 Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
Saan pay idi a naiddep ti pagsilawan ti Dios, ket ni Samuel, matmaturog iti balay ni Yahweh nga ayan ti lakasa ti tulag ti Dios.
4 Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
Inawagan ni Yahweh ni Samuel, a nagkuna, “Adtoyak.”
5 Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
Timmaray ni Samuel iti ayan ni Eli, ket kinunana, “Immayak ta inayabannak.” Kinuna ni Eli, “Saanka nga inayaban; agsublika iti pagiddaam.” Isu a napan nagidda ni Samuel.
6 Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
Immawag manen ni Yahweh, “Samuel.” Bimmangon manen ni Samuel ket napan kenni Eli ket kinunana, “Inayabannak isu nga adtoyak.” Simmungbat ni Eli, “Saanka nga inayaban, anakko; inka pay agidda.”
7 Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
Ita, awan pay ti kapadasan ni Samuel kenni Yahweh, wenno awan pay pulos ti aniaman a mensahe a naipakita kenkuana manipud kenni Yahweh.
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
Inawagan manen ni Yahweh ni Samuel iti maikatlo a gundaway. Bimmangon manen ni Samuel ket napan kenni Eli ket kinunana, “Immayak ta inayabannak.” Ket naamiris ni Eli nga inawagan ni Yahweh ti ubing.
9 Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
Ket kinuna ni Eli kenni Samuel, “Mapanka agidda manen; no awagannaka manen, nasken nga ibagam, 'Agsaoka, O Yahweh, ta dumdumngeg ti adipenmo.”' Isu a napan nagidda manen ni Samuel iti pagid-iddaanna.
10 Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
Immay ni Yahweh ket nagtakder; immawag a kas iti immuna, “Samuel, Samuel.” Ket kinuna ni Samuel, “Agsaoka, ta dumdumngeg ti adipenmo.”
11 Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
Kinuna ni Yahweh kenni Samuel, “Dumngegka, umadanin nga aramidek iti Israel ti banag nga uray la agkintayeg dagiti lapayag ti amin a makangngeg iti daytoy.
12 Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
Iti dayta nga aldaw, ipatungpalkonto kenni Eli dagiti amin nga imbagak maipanggep iti balayna, manipud iti rugi agingga iti pagpatinggaan.
13 Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
Imbagak kenkuana a dandanin nga ukomek a mammaminsan ti balayna gapu iti amin a basol nga ammona, gapu ta nangiyeg iti lunod dagiti annakna kadagiti bagbagida ket saanna ida nga inatipa.
14 Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
Gapu iti daytoy, insapatak iti balay ni Eli a saanto pulos a mapakawan dagiti basol ti balayna babaen iti daton wenno sagut.”
15 Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
Nagidda ni Samuel agingga iti bigat; kalpasanna, linukatanna dagiti ruangan ti balay ni Yahweh. Ngem mabuteng ni Samuel a mangibaga kenni Eli iti maipanggep iti sirmata.
16 lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
Ket inayaban ni Eli ni Samuel a kunana, “Samuel, anakko.” Kinuna ni Samuel, “Adtoyak.”
17 Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
Kinuna ni Eli, “Ania ti imbagana kenka? Saanmo koma nga ilimed kaniak. Dusaennaka ti Dios, ken ad-adda pay koma no ilimedmo kaniak ti aniaman nga imbagana kenka.”
18 Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
Imbaga amin ni Samuel kenkuana; awan ti inlimedna kenkuana. Kinuna ni Eli, “Ni Yahweh daytoy. Aramidenna koma ti kasayaatan a maaramid.”
19 Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
Dimmakkel ni Samuel, ket adda kenkuana ni Yahweh ket awan ti pimmalso kadagiti padtona.
20 Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
Ammo ti entero nga Israel manipud Dan agingga iti Beerseba a nadutokan ni Samuel nga agbalin a profeta ni Yahweh.
21 Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.
Nagparang manen ni Yahweh idiay Silo, ta nagparang isuna a mismo kenni Samuel idiay Silo babaen iti saona.

< 1 Samweli 3 >