< 1 Samweli 3 >

1 Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
Or l’enfant Samuel servait le Seigneur devant Héli, et la parole du Seigneur était précieuse en ces jours-là; il n’y avait pas de vision manifeste.
2 Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
Il arriva donc un certain jour qu’Héli était couché en son lieu (or ses yeux étaient obscurcis, et il ne pouvait pas voir);
3 Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
Avant que la lampe de Dieu fût éteinte, Samuel dormait dans le temple du Seigneur, où était l’arche de Dieu.
4 Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
Et le Seigneur appela Samuel, qui répondant, dit: Me voici.
5 Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
Alors il courut à Héli et dit: Me voici; car vous m’avez appelé. Héli répondit: Je ne t’ai pas appelé; retourne-t’en, et dors. Et il s’en alla, et il dormit.
6 Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
Mais le Seigneur recommença à appeler de nouveau Samuel. Et Samuel, se levant, s’en alla vers Héli et dit: Me voici, parce que vous m’avez appelé. Et Héli répondit: Je ne t’ai pas appelé, mon fils; retourne-t’en et dors.
7 Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
Or, Samuel ne connaissait pas encore le Seigneur, et la parole du Seigneur ne lui avait pas été révélée.
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
Et le Seigneur recommença, et il appela encore Samuel pour la troisième fois. Et Samuel, se levant, s’en alla vers Héli,
9 Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
Et dit: Me voici, parce que vous m’avez appelé. Héli comprit donc que le Seigneur appelait l’enfant, et il dit à Samuel. Va, et dors: et si dans la suite il t’appelle, tu diras: Parlez, Seigneur, parce que votre serviteur écoute. Samuel s’en alla donc et dormit en son lieu.
10 Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
Et le Seigneur vint, et s’arrêta; puis il appela, comme il avait appelé par deux fois: Samuel, Samuel. Et Samuel répondit: Parlez, Seigneur, parce que votre serviteur écoute.
11 Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
Alors le Seigneur dit à Samuel: Voici que moi je vais faire entendre une parole dans Israël; et quiconque l’entendra, ses deux oreilles tinteront.
12 Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
En ce jour-là, je susciterai contre Héli tout ce que j’ai dit sur sa maison: je commencerai et j’achèverai.
13 Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
Car je lui ai prédit que je devais juger sa maison à jamais, pour cause d’iniquité, parce qu’il savait que ses fils agissaient indignement, et qu’il ne les a pas corrigés.
14 Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
C’est pour cela que j’ai juré à la maison d’Héli, que l’iniquité de sa maison ne sera jamais expiée par des victimes et par des offrandes.
15 Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
Or, Samuel dormit jusqu’au matin, et il ouvrit les portes de la maison du Seigneur. Et Samuel craignait de déclarer la vision à Héli.
16 lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
Héli appela donc Samuel et dit: Samuel, mon fils? Celui-ci répondant, dit: Je suis présent.
17 Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
Et il l’interrogea: Quel est le discours que t’a tenu le Seigneur? Je te prie de ne point me le céler. Que Dieu te fasse ceci, et qu’il ajoute cela, si tu me caches quelqu’une de toutes les paroles qui t’ont été dites.
18 Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
Samuel lui déclara donc toutes les paroles, et ne les lui cacha pas. Et Héli répondit: Il est le Seigneur; qu’il fasse ce qui est bon à ses yeux.
19 Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
Or, Samuel grandit, et le Seigneur était avec lui, et nulle de ses paroles ne tomba par terre.
20 Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
Et tout Israël connut depuis Dan jusqu’à Bersabée que Samuel était un fidèle prophète du Seigneur.
21 Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.
Et le Seigneur continua à apparaître à Silo, parce que le Seigneur s’était révélé à Samuel à Silo, selon la parole du Seigneur. Et le discours de Samuel parvint à tout Israël.

< 1 Samweli 3 >