< 1 Samweli 3 >

1 Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
Forsothe the child Samuel `mynystride to the Lord bifor Heli, and the word of the Lord was preciouse; in tho daies was noon opyn reuelacioun.
2 Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
Therfor it was doon in a dai, Heli lay in his bed, and hise iyen dasewiden, and he myyte not se the lanterne of God, bifor that it was quenchid.
3 Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
Forsothe Samuel slepte in the temple of the Lord, where the ark of God was.
4 Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
And the Lord clepide Samuel; and he answeride and seide, Lo!
5 Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
Y. And he ran to Hely, and seide to hym, Lo! Y; for thou clepidist me. Which Hely seide, Y clepide not thee; turne thou ayen and slepe.
6 Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
And he yede and slepte. And the Lord addide eft to clepe Samuel; and Samuel roos, and yede to Hely, and seide, Lo! Y; for thou clepidist me. And Heli answeride, Y clepide not thee, my sone; turne thou ayen and slepe.
7 Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
Forsothe Samuel knew not yit the Lord, nether the `word of the Lord was shewid to hym.
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
And the Lord addide, and clepide yit Samuel the thridde tyme; `which Samuel roos and yede to Heli,
9 Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
and seide, Lo! Y; for thou clepidist me. Therfor Heli vndirstood, that the Lord clepide the child; and Heli seide to Samuel, Go and slepe; and if he clepith thee aftirward, thou schalt seie, Speke thou, Lord, for thi seruaunt herith. Therfor Samuel yede and slepte in his place.
10 Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
And the Lord cam, and stood, and clepide as he hadde clepid the secunde tyme, Samuel, Samuel. And Samuel seide, Speke thou, Lord, for thi seruaunt herith.
11 Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
And the Lord seide to Samuel, Lo! Y make a word in Israel, which word who euer schal here, bothe hise eeris schulen rynge.
12 Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
In that dai Y schal reise ayens Heli alle thingis, whiche Y spak on his hows; Y schal bigynne, and Y schal ende.
13 Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
For Y biforseide to hym, that Y schulde deme his hows with outen ende for wickidnesse; for he knew, that hise sones diden vnworthili, and he chastiside not hem.
14 Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
Therfor Y swoor to the hows of Heli, that the wickidnesse of his hows schal not be clensid bi sacrifices and yiftis til in to with outen ende.
15 Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
Forsothe Samuel slepte til the morewtid, and he openyde the doris of the hows of the Lord; and Samuel dredde to schewe the reuelacioun to Heli.
16 lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
Therfor Heli clepide Samuel, and seide, Samuel, my sone. And he answeride and seide, Y am redi.
17 Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
And Heli axide hym, What is the word which the Lord spak to thee? Y preye thee, hide thou not fro me; God do to thee `these thingis, and encreesse these thingis, if thou hidist fro me a word of alle wordis that ben seid to thee.
18 Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
And Samuel schewide to hym alle the wordis, and `hidde not fro hym. And Heli answeride, He is the Lord; do he that, that is good in hise iyen.
19 Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
Forsothe Samuel encreeside, and the Lord was with hym, and noon of alle hise wordis felde in to erthe.
20 Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
And al Israel fro Dan to Bersabee knew, that feithful Samuel was a profete of the Lord.
21 Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.
And the Lord addide `that he schulde appere in Silo, for the Lord was schewid to Samuel in Silo bi the `word of the Lord; and the word of Samuel cam to al Israel.

< 1 Samweli 3 >