< 1 Samweli 3 >

1 Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
and [the] youth Samuel to minister [obj] LORD to/for face: before Eli and word LORD to be precious in/on/with day [the] they(masc.) nothing vision to break through
2 Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
and to be in/on/with day [the] he/she/it and Eli to lie down: lay down in/on/with place his (and eye: seeing his *Q(K)*) to profane/begin: begin faint not be able to/for to see: see
3 Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
and lamp God before to quench and Samuel to lie down: lay down in/on/with temple LORD which there ark God
4 Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
and to call: call to LORD to(wards) Samuel and to say look! I
5 Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
and to run: run to(wards) Eli and to say look! I for to call: call to to/for me and to say not to call: call to to return: again to lie down: lay down and to go: went and to lie down: lay down
6 Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
and to add: again LORD to call: call to still Samuel and to arise: rise Samuel and to go: went to(wards) Eli and to say look! I for to call: call to to/for me and to say not to call: call to son: child my to return: again to lie down: lay down
7 Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
and Samuel before to know [obj] LORD and before to reveal: reveal to(wards) him word LORD
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
and to add: again LORD to call: call to Samuel in/on/with third and to arise: rise and to go: went to(wards) Eli and to say look! I for to call: call to to/for me and to understand Eli for LORD to call: call to to/for youth
9 Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
and to say Eli to/for Samuel to go: went to lie down: lay down and to be if to call: call to to(wards) you and to say to speak: speak LORD for to hear: hear servant/slave your and to go: went Samuel and to lie down: lay down in/on/with place his
10 Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
and to come (in): come LORD and to stand and to call: call to like/as beat in/on/with beat Samuel Samuel and to say Samuel to speak: speak for to hear: hear servant/slave your
11 Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
and to say LORD to(wards) Samuel behold I to make: do word: thing in/on/with Israel which all to hear: hear him to tingle two ear his
12 Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
in/on/with day [the] he/she/it to arise: establish to(wards) Eli [obj] all which to speak: speak to(wards) house: household his to profane/begin: begin and to end: finish
13 Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
and to tell to/for him for to judge I [obj] house: household his till forever: enduring in/on/with iniquity: crime which to know for to lighten to/for them son: child his and not to rebuke in/on/with them
14 Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
and to/for so to swear to/for house: household Eli if: surely yes to atone iniquity: crime house: household Eli in/on/with sacrifice and in/on/with offering till forever: enduring
15 Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
and to lie down: lay down Samuel till [the] morning and to open [obj] door house: temple LORD and Samuel to fear from to tell [obj] [the] vision to(wards) Eli
16 lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
and to call: call to Eli [obj] Samuel and to say Samuel son: child my and to say look! I
17 Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
and to say what? [the] word: thing which to speak: speak to(wards) you not please to hide from me thus to make: do to/for you God and thus to add if to hide from me word: thing from all [the] word: thing which to speak: speak to(wards) you
18 Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
and to tell to/for him Samuel [obj] all [the] word: thing and not to hide from him and to say LORD he/she/it [the] pleasant (in/on/with eye: appearance his *Q(K)*) to make: do
19 Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
and to magnify Samuel and LORD to be with him and not to fall: fall from all word his land: soil [to]
20 Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
and to know all Israel from Dan and till Beersheba Beersheba for be faithful Samuel to/for prophet to/for LORD
21 Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.
and to add: again LORD to/for to see: see in/on/with Shiloh for to reveal: reveal LORD to(wards) Samuel in/on/with Shiloh in/on/with word LORD

< 1 Samweli 3 >