< 1 Samweli 29 >

1 Wafilisti wakakusanya majeshi yao yote huko Afeki, nao Waisraeli wakapiga kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli.
Les Philistins rassemblèrent toutes leurs troupes à Aphec, et Israël était campé près de la source, en Jezraël.
2 Watawala wa Wafilisti walipokuwa wakipita pamoja na vikosi vyao vya mamia na vya maelfu, Daudi na watu wake walikuwa wakitembea huko nyuma pamoja na Akishi.
Pendant que les princes des Philistins s’avançaient en tête des centaines et des milliers, et que David et ses gens marchaient à l’arrière-garde avec Achis,
3 Majemadari wa Wafilisti wakauliza, “Vipi kuhusu hawa Waebrania?” Akishi akajibu, “Huyu si Daudi, aliyekuwa afisa wa Sauli mfalme wa Israeli? Ameshakuwa pamoja nami kwa zaidi ya mwaka, naye tangu alipomwacha Sauli hadi sasa, sikuona kosa lolote kwake.”
les chefs des Philistins dirent: « Qu’est-ce que ces Hébreux? » Achis répondit aux chefs des Philistins: « N’est-ce pas ce David, serviteur de Saül, roi d’Israël, qui est avec moi depuis des jours et depuis des années, sans que j’aie trouvé en lui la moindre chose à reprocher, depuis qu’il a passé vers nous jusqu’à ce jour. »
4 Lakini majemadari wa Wafilisti wakamkasirikia na kusema, “Mrudishe mtu huyu, apate kurudi mahali pale ulipompangia. Haimpasi kufuatana pamoja nasi vitani, asije akageuka, akawa kinyume chetu vitani. Ni kwa njia ipi bora zaidi angeweza kujipatia tena kibali kwa bwana wake, isipokuwa kwa vichwa vya watu wetu wenyewe?
Mais les chefs des Philistins s’irritèrent contre Achis, et les chefs des Philistins lui dirent: « Renvoie cet homme, et qu’il retourne dans le lieu où tu l’as établi; qu’il ne descende pas avec nous à la bataille, de peur qu’il ne soit pour nous un adversaire pendant le combat. Et comment pourrait-il rentrer en grâce auprès de son maître, si ce n’est en lui offrant les têtes de ces hommes?
5 Je, huyu si ndiye Daudi walioimba kumhusu katika ngoma zao, wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
N’est-ce pas ce David pour qui l’on chantait en dansant: Saül a tué ses mille, et David ses dix mille. »
6 Basi Akishi akamwita Daudi na kumwambia, “Kama vile Bwana aishivyo, wewe umekuwa mtu mwaminifu, nami ningependa utumike pamoja nami katika jeshi. Tangu siku ile uliyofika kwangu hadi sasa, sijaona kosa lolote kwako, lakini hao watawala hawakukubali.
Achis appela David et lui dit: « Aussi vrai que Yahweh est vivant! tu es un homme droit, et je vois de bon œil toute ta conduite avec moi dans le camp, car je n’ai rien trouvé de mauvais en toi, depuis le jour où tu es venu vers moi jusqu’à ce jour; mais tu déplais aux yeux des princes.
7 Rudi na uende kwa amani; usifanye chochote cha kuwakasirisha watawala wa Kifilisti.”
Retourne donc et va-t-en en paix, pour ne rien faire de désagréable aux yeux des princes des Philistins. »
8 Daudi akamuuliza Akishi, “Lakini mimi nimefanya nini? Je, umeona nini kibaya juu ya mtumishi wako tangu siku ile niliyokuja kwako hadi leo? Kwa nini nisirudi na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?”
David dit à Achis: « Mais qu’ai-je fait, et qu’as-tu trouvé en ton serviteur, depuis le jour où je suis venu auprès de toi jusqu’à ce jour, pour que je n’aille pas combattre les ennemis de mon seigneur le roi? »
9 Akishi akamjibu Daudi, “Mimi ninajua ya kuwa wewe umekuwa wa kupendeza machoni pangu kama vile malaika wa Mungu. Lakini hao majemadari wa Wafilisti wamesema, ‘Huyu haimpasi kwenda vitani pamoja nasi.’
Achis répondit et dit à David: « Je sais que tu as été bon à mon égard comme un ange de Dieu; mais les chefs des Philistins disent: il ne montera pas avec nous à la bataille.
10 Sasa amka mapema, pamoja na watumishi wa bwana wako waliofuatana nawe, nanyi ondokeni asubuhi mara kutakapopambazuka.”
Ainsi lève-toi de bon matin, toi et les serviteurs de ton seigneur qui sont venus avec toi; levez-vous de bon matin, et dès qu’il fera jour, partez. »
11 Hivyo Daudi na watu wake wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda zao kurudi katika nchi ya Wafilisti, nao Wafilisti wakapanda kwenda Yezreeli.
David et ses gens se levèrent de bonne heure, pour partir dès le matin et retourner au pays des Philistins; et les Philistins montèrent à Jezraël.

< 1 Samweli 29 >