< 1 Samweli 29 >

1 Wafilisti wakakusanya majeshi yao yote huko Afeki, nao Waisraeli wakapiga kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli.
Therfor alle the cumpenyes of Filisteis weren gaderid in Aphec, but also Israel settide tentis aboue the welle that was in Jezrael.
2 Watawala wa Wafilisti walipokuwa wakipita pamoja na vikosi vyao vya mamia na vya maelfu, Daudi na watu wake walikuwa wakitembea huko nyuma pamoja na Akishi.
And sotheli the princis of Filisteis yeden in cumpenyes of an hundrid, and in thousyndis; forsothe Dauid and hise men weren in the laste cumpenye with Achis.
3 Majemadari wa Wafilisti wakauliza, “Vipi kuhusu hawa Waebrania?” Akishi akajibu, “Huyu si Daudi, aliyekuwa afisa wa Sauli mfalme wa Israeli? Ameshakuwa pamoja nami kwa zaidi ya mwaka, naye tangu alipomwacha Sauli hadi sasa, sikuona kosa lolote kwake.”
And the princes of Filisteis seiden to Achis, What wolen these Ebreis to hem silf? And Achis seide to the princes of Filisteis, Whether ye knowen not Dauid, that was the seruaunt of Saul, kyng of Israel? and he was with me in many daies, `ether yeeris, and Y foond not in hym ony thing, fro the dai, in which he fledde to me `til to this dai.
4 Lakini majemadari wa Wafilisti wakamkasirikia na kusema, “Mrudishe mtu huyu, apate kurudi mahali pale ulipompangia. Haimpasi kufuatana pamoja nasi vitani, asije akageuka, akawa kinyume chetu vitani. Ni kwa njia ipi bora zaidi angeweza kujipatia tena kibali kwa bwana wake, isipokuwa kwa vichwa vya watu wetu wenyewe?
Sotheli the princes of Filisteis weren wrooth ayens hym, and seiden to hym, The man turne ayen, and sitte in his place, in which thou hast ordened hym, and come he not down with vs in to batel, lest he be maad aduersarie to vs, whanne we han bigunne to fiyte; for hou mai he plese his lord in other maner, no but in oure heedis?
5 Je, huyu si ndiye Daudi walioimba kumhusu katika ngoma zao, wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
Whether this is not Dauid, to whom thei sungen in daunsis, and seiden, Saul smoot in thousyndis, and Dauid smoot in hise ten thousyndis?
6 Basi Akishi akamwita Daudi na kumwambia, “Kama vile Bwana aishivyo, wewe umekuwa mtu mwaminifu, nami ningependa utumike pamoja nami katika jeshi. Tangu siku ile uliyofika kwangu hadi sasa, sijaona kosa lolote kwako, lakini hao watawala hawakukubali.
Therfor Achis clepide Dauid, and seide to hym, The Lord lyueth; for thou art riytful, and good in my siyt, and thi goyng out and `thin entryng is with me in castels, and Y `foond not in thee ony thing of yuel, fro the day in which thou camest to me til to this dai; but thou plesist not the princis.
7 Rudi na uende kwa amani; usifanye chochote cha kuwakasirisha watawala wa Kifilisti.”
Therfor turne thou ayen, and go in pees, and offende thou not the iyen of princis of Filisteis.
8 Daudi akamuuliza Akishi, “Lakini mimi nimefanya nini? Je, umeona nini kibaya juu ya mtumishi wako tangu siku ile niliyokuja kwako hadi leo? Kwa nini nisirudi na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?”
And Dauid seide to Achis, Forsothe what `dide Y, and what hast thou founde in me thi seruaunt, fro the dai in which Y was in thi siyt til in to this dai, that Y come not, and fiyte ayens the enemyes of my lord the kyng?
9 Akishi akamjibu Daudi, “Mimi ninajua ya kuwa wewe umekuwa wa kupendeza machoni pangu kama vile malaika wa Mungu. Lakini hao majemadari wa Wafilisti wamesema, ‘Huyu haimpasi kwenda vitani pamoja nasi.’
Forsothe Achis answeride, and spak to Dauid, Y woot that thou art good, and as the aungel of God in my iyen; but the princes of Filisteis seyden, He schal not stie with vs in to batel.
10 Sasa amka mapema, pamoja na watumishi wa bwana wako waliofuatana nawe, nanyi ondokeni asubuhi mara kutakapopambazuka.”
Therfor rise thou eerli, thou, and thi seruauntis that camen with thee; and whanne ye han ryse bi nyyt, and it bigynneth to be cleer, go ye.
11 Hivyo Daudi na watu wake wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda zao kurudi katika nchi ya Wafilisti, nao Wafilisti wakapanda kwenda Yezreeli.
Therfor Dauid roos bi nyyt, he and hise men, that thei schulden go forth eerli, and turne ayen to the lond of Fylisteis; sotheli Filisteis stieden in to Jezrael.

< 1 Samweli 29 >