< 1 Samweli 28 >

1 Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”
En ces jours-là, les Philistins rassemblèrent leurs armées pour faire la guerre, afin de combattre Israël. Akish dit à David: « Sache que tu partiras avec moi dans l'armée, toi et tes hommes. »
2 Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”
David dit à Akish: « Tu sauras donc ce que ton serviteur peut faire. » Achille dit à David: « Je ferai de toi mon garde du corps pour toujours. »
3 Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.
Or Samuel était mort, et tout Israël avait porté son deuil et l'avait enterré à Rama, dans sa propre ville. Saül avait chassé du pays ceux qui avaient des esprits familiers et les sorciers.
4 Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa.
Les Philistins se rassemblèrent, et vinrent camper à Sunem. Saül rassembla tout Israël, et ils campèrent à Guilboa.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu.
Lorsque Saül vit l'armée des Philistins, il eut peur, et son cœur trembla beaucoup.
6 Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa njia ya manabii.
Saül consulta Yahvé, et Yahvé ne lui répondit ni par des songes, ni par l'urim, ni par des prophètes.
7 Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”
Alors Saül dit à ses serviteurs: « Cherche-moi une femme qui a un esprit familier, afin que j'aille la voir et que je la consulte. » Ses serviteurs lui dirent: « Voici une femme qui a un esprit familier à Endor. »
8 Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”
Saül se déguisa, mit d'autres vêtements et partit, lui et deux hommes avec lui, et ils arrivèrent de nuit chez la femme. Il dit: « Je te prie de consulter pour moi l'esprit familier, et de me faire monter celui que je te nommerai. »
9 Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”
La femme lui dit: « Voici, tu sais ce que Saül a fait, comment il a exterminé du pays ceux qui ont des esprits familiers et les sorciers. Pourquoi donc tends-tu un piège à ma vie, pour me faire mourir? »
10 Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”
Saül lui jura par l'Éternel: « L'Éternel est vivant! Tu ne seras pas punie pour cette affaire. »
11 Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?” Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
Alors la femme dit: « Qui dois-je te faire monter? » Il a dit: « Faites monter Samuel pour moi. »
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
Lorsque la femme vit Samuel, elle poussa un grand cri. La femme s'adressa à Saül en disant: « Pourquoi m'as-tu trompée? Car tu es Saül! »
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?” Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
Le roi lui dit: « N'aie pas peur! Que vois-tu? » La femme dit à Saul: « Je vois un dieu qui sort de la terre. »
14 Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
Il lui dit: « A quoi ressemble-t-il? » Elle dit: « Un vieil homme arrive. Il est couvert d'une robe. » Saül comprit qu'il s'agissait de Samuel, et il s'inclina, le visage contre terre, en signe de respect.
15 Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”
Samuel dit à Saül: « Pourquoi m'as-tu dérangé, pour me faire monter? » Saül répondit: « Je suis très angoissé, car les Philistins me font la guerre, et Dieu s'est éloigné de moi, il ne me répond plus, ni par des prophètes, ni par des songes. C'est pourquoi je t'ai appelé, afin que tu me fasses connaître ce que je dois faire. »
16 Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako?
Samuel répondit: « Pourquoi donc m'interroges-tu, puisque l'Éternel s'est éloigné de toi et qu'il est devenu ton adversaire?
17 Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi.
L'Éternel t'a fait ce qu'il avait dit par moi. Yahvé a arraché le royaume de ta main et l'a donné à ton prochain, à David.
18 Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo.
C'est parce que tu n'as pas écouté la voix de l'Éternel et que tu n'as pas exécuté son ardente colère contre Amalek, que l'Éternel t'a fait cela aujourd'hui.
19 Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”
De plus, l'Éternel livrera Israël avec toi entre les mains des Philistins, et demain, toi et tes fils serez avec moi. L'Éternel livrera aussi l'armée d'Israël entre les mains des Philistins. »
20 Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.
Et Saül tomba immédiatement de tout son long sur la terre et fut terrifié, à cause des paroles de Samuel. Il n'avait plus de force en lui, car il n'avait mangé aucun pain de tout le jour ni de toute la nuit.
21 Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye.
La femme s'approcha de Saül, vit qu'il était très troublé et lui dit: « Voici que ton serviteur a écouté ta voix, et moi, j'ai mis ma vie en jeu, et j'ai écouté les paroles que tu m'as dites.
22 Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”
Maintenant, écoute aussi la voix de ton serviteur, et laisse-moi mettre devant toi un morceau de pain. Mange, afin que tu aies des forces pour poursuivre ton chemin. »
23 Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.” Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.
Mais il refusa, et dit: « Je ne mangerai pas. » Mais ses serviteurs, avec la femme, le contraignirent, et il écouta leur voix. Il se leva de terre et s'assit sur le lit.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu.
La femme avait dans la maison un veau gras. Elle se hâta de l'égorger; elle prit de la farine, la pétrit et en fit des pains sans levain.
25 Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.
Elle l'apporta devant Saül et devant ses serviteurs, et ils mangèrent. Puis ils se levèrent et partirent cette nuit-là.

< 1 Samweli 28 >