< 1 Samweli 28 >
1 Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”
And it was in the days those and they gathered together [the] Philistines armies their for war to fight against Israel and he said Achish to David certainly you will know that with me you will go out in the camp you and men your.
2 Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”
And he said David to Achish therefore you you will know [that] which he will do servant your and he said Achish to David therefore a watchman of head my I will make you all the days.
3 Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.
And Samuel he had died and they had mourned for him all Israel and they had buried him in Ramah in own city his and Saul he had removed the necromancers and the soothsayers from the land.
4 Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa.
And they gathered together [the] Philistines and they came and they encamped at Shunem and he gathered Saul all Israel and they encamped at Gilboa.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu.
And he saw Saul [the] camp of [the] Philistines and he was afraid and it trembled heart his exceedingly.
6 Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa njia ya manabii.
And he enquired Saul by Yahweh and not he answered him Yahweh neither by dreams nor by Urim nor by prophets.
7 Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”
And he said Saul to servants his seek for me a woman [the] owner of necromancy so let me go to her so I may consult her and they said servants his to him there! a woman of an owner of necromancy [is] in En-dor.
8 Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”
And he disguised himself Saul and he was clothed garments other and he went he and two men with him and they came to the woman night and he said (divine *Q(k)*) please for me by necromancy and bring up for me [the one] whom I will say to you.
9 Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”
And she said the woman to him here! you you know [that] which he has done Saul that he has cut off the necromancers and the soothsayer from the land and why? [are] you setting traps on life my to cause to die me.
10 Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”
And he swore to her Saul by Yahweh saying [by] [the] life of Yahweh if it will happen to you punishment in the matter this.
11 Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?” Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
And she said the woman whom? will I bring up for you and he said Samuel bring up for me.
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
And she saw the woman Samuel and she cried out with a voice great and she said the woman to Saul saying why? have you deceived me and you [are] Saul.
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?” Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
And he said to her the king may not you fear for what? have you seen and she said the woman to Saul gods I have seen coming up from the earth.
14 Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
And he said to her what? [is] appearance his and she said a man old [is] coming up and he [is] wrapped a robe and he knew Saul that [was] Samuel it and he bowed low face [the] ground towards and he bowed down.
15 Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”
And he said Samuel to Saul why? have you disturbed me by bringing up me and he said Saul it is distress to me exceedingly and [the] Philistines - [are] fighting against me and God he has turned aside from with me and not he has answered me yet neither by [the] hand of prophets nor by dreams and I have summoned! you to make known to me what? will I do.
16 Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako?
And he said Samuel and why? do you ask me and Yahweh he has turned aside from with you and he has become enemy your.
17 Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi.
And he has done Yahweh to him just as he spoke by hand my and he has torn Yahweh the kingdom from hand your and he has given it to neighbor your to David.
18 Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo.
Since not you listened to [the] voice of Yahweh and not you executed [the] burning of anger his on Amalek there-fore the thing this he has done to you Yahweh the day this.
19 Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”
So he may give Yahweh also Israel with you in [the] hand of [the] Philistines and tomorrow you and sons your [will be] with me also [the] camp of Israel he will give Yahweh in [the] hand of [the] Philistines.
20 Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.
And he made haste Saul and he fell [the] fullness of stature his [the] ground towards and he was afraid exceedingly from [the] words of Samuel also strength not it was in him for not he had eaten food all the day and all the night.
21 Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye.
And she came the woman to Saul and she saw that he was terrified exceedingly and she said to him here! she has listened maidservant your to voice your and I have put life my in palm my and I have listened to words your which you have spoken to me.
22 Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”
And now listen please also you to [the] voice of maidservant your so let me set before you a piece of bread and eat so may it be in you strength for you will go on the way.
23 Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.” Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.
And he refused and he said not I will eat and they urged him servants his and also the woman and he listened to voice their and he arose from the ground and he sat to the bed.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu.
And [belonged] to the woman a calf of [the] stall in the house and she made haste and she slaughtered it and she took flour and she kneaded [it] and she baked it unleavened bread.
25 Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.
And she brought [them] near before Saul and before servants his and they ate and they arose and they went on the night that.