< 1 Samweli 28 >
1 Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”
And it came to pass, in those days, when the Philistines gathered together their hosts for war, to fight with Israel, that Achish said unto David, Thou must, know, that, with me, shalt thou go forth in the host, thou and thy men.
2 Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”
And David said unto Achish, Therefore, now, shalt thou know what thy servant can do. And Achish said unto David, Therefore, keeper of my head, will I appoint thee, all the days.
3 Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.
Now, Samuel, was dead, and all Israel had lamented him, and buried him in Ramah, even in his own city, —Saul, moreover had put away them who had familiar spirits and them who were oracles, out of the land.
4 Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa.
So then the Philistines gathered themselves together, and came in, and encamped in Shunem, —and Saul gathered together all Israel, and they encamped in Gilboa.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu.
And, when Saul saw the host of the Philistines, he was afraid, and his heart trembled exceedingly.
6 Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa njia ya manabii.
Then Saul enquired of Yahweh, but Yahweh answered him not, —neither by Dreams, nor by the Lights, nor by prophets.
7 Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”
Then said Saul unto his servants—Seek me out a woman that owneth a familiar spirit, that I may even go unto her, and enquire of her. And his servants said unto him, Lo! there is a woman that owneth a familiar spirit in En-dor.
8 Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”
Saul therefore disguised himself, and put on other raiment, and departed—he and two men with him, and they came to the woman by night, —and he said—Divine for me, I pray thee, by the familiar spirit, and bring up for me—whomsoever I shall name unto thee.
9 Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”
And the woman said unto him—Lo! thou, knowest what Saul hath done, how he hath cut off them who have familiar spirits and him who is an oracle, out of the land, —wherefore, then, art thou striking at my life, to put me to death?
10 Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”
So then Saul sware unto her by Yahweh, saying, —By the life of Yahweh, there shall no punishment befall thee for this thing.
11 Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?” Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
Then said the woman, Whom shall I bring up for thee? And he said, Samuel, bring thou up for me.
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
And, when the woman saw Samuel, she made outcry with a loud voice, —and the woman spake unto Saul, saying—Wherefore hast thou deceived me, thou thyself being Saul?
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?” Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
And the king said unto her—Be not afraid, but what sawest thou? And the woman said unto Saul, A god, saw I, coming up out of the earth.
14 Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
And he said to her—What was his form? And she said—An old man, coming up, he being wrapped about with a robe. Then Saul knew, that it was, Samuel, so he inclined his face to the earth, and bowed himself down.
15 Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”
And Samuel said unto Saul, Wherefore hast thou disquieted me, by bringing me up? And Saul said—I am in sore distress, for, the Philistines, are making war against me, and, God, hath turned away from me, and answereth me no more—either by means of the prophets, or by dreams, therefore have I even called for thee, to let me know, what I am to do.
16 Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako?
Then said Samuel, Wherefore, then, shouldst thou ask me, —when, Yahweh, hath turned away from thee, and hath come to be with thy neighbour?
17 Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi.
Therefore hath Yahweh done for him, as he spake by me, —yea Yahweh hath rent the kingdom out of thy hand, and given it to a neighbour of thine—to David.
18 Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo.
As thou didst not hearken unto the voice of Yahweh, neither didst execute the glow of his anger upon Amalek, therefore, this thing, hath Yahweh done unto thee this day;
19 Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”
that Yahweh may deliver, Israel also, with thee, into the hand of the Philistines, and, to-morrow, thou and thy sons with thee are about to fall, —the host of Israel also, will Yahweh deliver, into the hand of the Philistines.
20 Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.
Then Saul hastened, and fell prostrate—the whole length of him—to the earth, and was sore afraid, at the words of Samuel, and indeed, no, strength, was left in him, for he had not eaten food all the day and all the night.
21 Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye.
And the woman came unto Saul, and, when she saw that he was greatly terrified, she said unto him—Lo! thy handmaid hearkened unto thy voice, and I put my life into my hand, and heard thy words which thou didst speak unto me.
22 Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”
Now, therefore, I pray thee, hearken, thou also, unto the voice of thy handmaid, and let me set before thee a morsel of food, and eat thou, —that there may be in thee strength, when thou goest on thy journey.
23 Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.” Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.
But he refused, and said—I will not eat. But, when his servants, and the woman also, strongly urged him, then hearkened he unto their voice, —and rose up from the earth, and sat on the bed.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu.
Now, the woman, had a calf fattening, in the shed. So she hastened, and sacrificed it, —and took meal, and kneaded, and baked thereof, unleavened cakes;
25 Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.
and brought near before Saul and before his servants, and they did eat. Then rose they up and departed, the same night.