< 1 Samweli 28 >

1 Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”
And it came to pass in those days, that the Philistines gathered their hosts together for warfare, to fight with Israel. And Achish said unto David: 'Know thou assuredly, that thou shalt go out with me in the host, thou and thy men.'
2 Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”
And David said to Achish: 'Therefore thou shalt know what thy servant will do.' And Achish said to David: 'Therefore will I make thee keeper of my head for ever.'
3 Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.
Now Samuel was dead, and all Israel had lamented him, and buried him in Ramah, even in his own city. And Saul had put away those that divined by a ghost or a familiar spirit out of the land.
4 Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa.
And the Philistines gathered themselves together, and came and pitched in Shunem; and Saul gathered all Israel together, and they pitched in Gilboa.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu.
And when Saul saw the host of the Philistines, he was afraid, and his heart trembled greatly.
6 Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa njia ya manabii.
And when Saul inquired of the LORD, the LORD answered him not, neither by dreams, nor by Urim, nor by prophets.
7 Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”
Then said Saul unto his servants: 'Seek me a woman that divineth by a ghost, that I may go to her, and inquire of her.' And his servants said to him: 'Behold, there is a woman that divineth by a ghost at En-dor.'
8 Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”
And Saul disguised himself, and put on other raiment, and went, he and two men with him, and they came to the woman by night; and he said: 'Divine unto me, I pray thee, by a ghost, and bring me up whomsoever I shall name unto thee.'
9 Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”
And the woman said unto him: 'Behold, thou knowest what Saul hath done, how he hath cut off those that divine by a ghost or a familiar spirit out of the land; wherefore then layest thou a snare for my life, to cause me to die?'
10 Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”
And Saul swore to her by the LORD, saying: 'As the LORD liveth, there shall no punishment happen to thee for this thing.'
11 Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?” Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
Then said the woman: 'Whom shall I bring up unto thee?' And he said: 'Bring me up Samuel.'
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
And when the woman saw Samuel, she cried with a loud voice; and the woman spoke to Saul, saying: 'Why hast thou deceived me? for thou art Saul.'
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?” Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
And the king said unto her: 'Be not afraid; for what seest thou?' And the woman said unto Saul: 'I see a godlike being coming up out of the earth.'
14 Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
And he said unto her: 'What form is he of?' And she said: 'An old man cometh up; and he is covered with a robe.' And Saul perceived that it was Samuel, and he bowed with his face to the ground, and prostrated himself.
15 Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”
And Samuel said to Saul: 'Why hast thou disquieted me, to bring me up?' And Saul answered: 'I am sore distressed; for the Philistines make war against me, and God is departed from me, and answereth me no more, neither by prophets, nor by dreams; therefore I have called thee, that thou mayest make known unto me what I shall do.'
16 Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako?
And Samuel said: 'Wherefore then dost thou ask of me, seeing the LORD is departed from thee, and is become thine adversary?
17 Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi.
And the LORD hath wrought for Himself; as He spoke by me; and the LORD hath rent the kingdom out of thy hand, and given it to thy neighbour, even to David.
18 Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo.
Because thou didst not hearken to the voice of the LORD, and didst not execute His fierce wrath upon Amalek, therefore hath the LORD done this thing unto thee this day.
19 Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”
Moreover the LORD will deliver Israel also with thee into the hand of the Philistines; and to-morrow shalt thou and thy sons be with me; the LORD will deliver the host of Israel also into the hand of the Philistines.'
20 Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.
Then Saul fell straightway his full length upon the earth, and was sore afraid, because of the words of Samuel; and there was no strength in him; for he had eaten no bread all the day, nor all the night.
21 Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye.
And the woman came unto Saul, and saw that he was sore affrighted, and said unto him: 'Behold, thy handmaid hath hearkened unto thy voice, and I have put my life in my hand, and have hearkened unto thy words which thou spokest unto me.
22 Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”
Now therefore, I pray thee, hearken thou also unto the voice of thy handmaid, and let me set a morsel of bread before thee; and eat, that thou mayest have strength, when thou goest on thy way.'
23 Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.” Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.
But he refused, and said: 'I will not eat.' But his servants, together with the woman, urged him; and he hearkened unto their voice. So he arose from the earth, and sat upon the bed.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu.
And the woman had a fatted calf in the house; and she made haste, and killed it; and she took flour, and kneaded it, and did bake unleavened bread thereof;
25 Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.
and she brought it before Saul, and before his servants; and they did eat. Then they rose up, and went away that night.

< 1 Samweli 28 >