< 1 Samweli 28 >
1 Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”
Fa: no, eso enoga Filisidini dunu ilia da Isala: ili fi ilima gegemusa: , dadi gagui dunu gilisi. Amola A: igise da Da: ibidima amane sia: i, “Dafawane! Di amola dia dunu da namagale Isala: ili dunuma gegemu.”
2 Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”
Da: ibidi da amane sia: i, “Ma! Dafawane! Na da dia hawa: hamosu dunu. Amola di da na hamobe di siga disu ba: mu.” A: igise da amane sia: i, “Defea! Na da di na da: i gaga: su dunu hamomu.”
3 Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.
Sa: miuele da bogoi dagoi amola Isala: ili dunu ilia bogoi didigia: lalu amola hina: moilaidafa La: ima amoga uli dogoi. Solo da wadela: i ba: la: lusu dunu, gesami dasu amola bosa: ga: su uda amola dunu amo Isala: ili sogega sefasi dagoi ba: i.
4 Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa.
Filisidini dadi gagui dunu da mogodigili asili amola Siouneme moilai gadenene wa: i fi esalu. Solo da Isala: ili dadi gagui dunu gilisili, Giliboua Goumia awalia wa: i fi esalu.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu.
Solo da Filisidini dadi gagui gilisibi ba: loba, e da baligili beda: i galu.
6 Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa njia ya manabii.
Amaiba: le, e da Hina Godema adi hamoma: bela: le adole ba: i. Be Hina Gode da ema golaia ba: su amola Iulimi amola Damimi amoga amola balofede dunu ilia sia: amoga dabe hame adole i.
7 Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”
Amalalu, Solo da ea eagene ouligisu dunuma amane sia: i, “Bosa: ga: su uda afae nagili hogolesima. Amalalu na da ema adole ba: la masunu.” Ilia da ema amane adole i, “Bosa: ga: su uda da Enedo moilaiga esala.”
8 Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”
Amaiba: le, Solo da enoga e dawa: digisa: besa: le, hina: da: i afadenei. E abula eno salawane, gasibi galu e amola dunu aduna eno, amo uda ba: la asi. E amo udama amane sia: i, “Bogoi a: silibuma adole ba: lalu, hobea misunu hou nama olelema. Dunu ea dio na sia: mu, amo ea a: silibu misa: ne sia: ma.”
9 Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”
Bosa: ga: su uda da Soloma bu adole i, “Dia da abuliba: le na bogosu logo fodosala: ? Di da hina bagade Solo ea hamobe hame dawa: sala: ? E da ba: la: lusu dunu amola bosa: ga: su dunu amola uda huluane Isala: ili sogega sefasi dagoi.”
10 Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”
Amalalu, Solo da dafawanedafa sia: amane ilegei, “Esalebe Hina Gode amo Ea Dioba: le, di da amo hou hamosea, se iasu hamedafa ba: mu, amo na da ilegesa.”
11 Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?” Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
Uda da bu adole ba: i, “Na da di ba: ma: ne, nowa bogoi dunu amo misa: ne sia: ma: bela: ?” Solo da adole i, “Sa: miuele!”
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
Be uda da Sa: miuele manebe ba: beba: le, a:a: ia gusa: nu, Soloma amane sia: i, “Di da abuliba: le nama ogogobela: ? Di da hina bagade Solofa galu galebe!”
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?” Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
Hina bagade Solo da ema amane sia: i, “Mae beda: ma! Di da adi ba: sala: ?” Uda da bu adole i, “Na da a: silibu osoba gudunini heda: lebe ba: sa!”
14 Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
E bu adole ba: i, “Amo da adi agoane ba: sala: ?” Uda da amane sia: i, “Amo da dunu da: i hamoi agoai heda: lebe.” “E da abula amoga idinigi galebe.” Amalalu, Solo da amo bogoi a: silibu da Sa: miuele galebeya dawa: digi. Amola e da ema nodomusa: , osoba begudui.
15 Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”
Sa: miuele da Soloma amane sia: i, “Dia da abuliba: le na didilisibala: ? Dia da abuliba: le na buhagima: ne hamobela: ?” Solo da bu adole i, “Bidi hamosu bagade da nama doaga: i dagoi. Filisidini dunu da nama gegenana amola Gode da na yolesi dagoi. E da nama golaia amola balofede dunumadi na adole ba: su amo nama dabe hame adole iaha. Amaiba: le, na da dima wele sia: na misi. Di da nama, na hamomu liligi olelema!”
16 Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako?
Sa: miuele da amane sia: i, “Hina Gode da di yolesili, bu dimawane ha lai dagoi. Amaiba: le, di da abuliba: le na misa: ne wele sia: bela: ?
17 Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi.
Hina Gode da na lafidili dima olelei liligi amo hamoi dagoi. E da dia hina bagade hou amo dima fadegale, Da: ibidima i dagoi.
18 Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo.
Di da Hina Gode Ea sia: i amo mae nabawane, A:malege dunu amola ilia liligi huluane wadela: ma: nedafa hame hamoi. Hina Gode Ea wali dima hamobe amo ea bai da goea.
19 Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”
E da di amola Isala: ili fi amo ali Filisidini dunu ilia lobo da: iya imunu. Aya eso, di amola diagofelali da nama gilisimu. Amola Hina Gode da Isala: ili dadi gagui wa: i amo Filisidini dunu ilia lobo da: iya imunu.”
20 Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.
Amogalu, hedolowane Solo da osoba gala: la sa: ili, mogosusuli dialebe ba: i. E da Sa: miuele ea sia: beba: le baligili beda: i galu. E da amo esoha amola gasia ha: i hame maiba: le, gasa hame ba: i.
21 Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye.
Uda da ema asili, e da baligili beda: i amo ba: beba: le, e amane sia: i, “Dafawane, Hina! Na da dia adole ba: i amo hamobeba: le, na esalusu gadenenewane udidimu agoai ba: i.
22 Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”
Dafawane, wali na dima adoleba: be amo dia hamoma. Na da digili ha: i manu hamoma: ne sia: ma. Di da bu gasa lama: ne, ha: i manu da defea.”
23 Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.” Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.
Solo da ha: i hame manu sia: i. Be ea eagene ouligisu dunu da e ha: i moma: ne logei. E da ouesalu, amalalu ilia sia: nababeba: le, osoba dialu wa: legadole, dia heda: su fafai amoga fila heda: i.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu.
Uda da hedolowane bulamagau mano (amo da sefe fima: ne, e da diasu ganodini ha: i manu iasu) amo fane legei. E da agi lale, hahamonanu, yisidi mae salawane gobei.
25 Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.
E da amo ha: i manu Solo amola ea ouligisu dunu ilia moma: ne, ilia midadi ligisi. Amalu, ilia da amo mai. Amola ilia amo gasia yolesili asi.