< 1 Samweli 27 >

1 Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
Ali David reèe u srcu svojem: poginuæu kadgod od ruke Saulove; nema bolje za me nego da pobjegnem u zemlju Filistejsku, te æe me se Saul okaniti i neæe me više tražiti po krajevima Izrailjevijem; tako æu se izbaviti iz ruku njegovijeh.
2 Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
Tada se podiže David i otide sa šest stotina ljudi koji bijahu s njim k Ahisu sinu Maohovu caru Gatskom.
3 Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
I osta David kod Ahisa u Gatu i ljudi njegovi, svaki sa svojom porodicom, David sa dvije žene svoje, Ahinoamom iz Jezraela i Avigejom iz Karmila ženom Navalovom.
4 Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
I kad javiše Saulu da je David utekao u Gat, presta ga tražiti.
5 Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
A David reèe Ahisu: ako sam našao milost pred tobom, neka mi dadu mjesto u kom gradu ove zemlje, da sjedim ondje, jer zašto da sjedi sluga tvoj s tobom u carskom gradu?
6 Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
I dade mu Ahis onoga dana Siklag. Zato Siklag pripada carevima Judinijem do današnjega dana.
7 Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
I osta David u zemlji Filistejskoj godinu i èetiri mjeseca.
8 Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
I izlažaše David sa svojim ljudima, i udaraše na Gesureje i Gerzeje i na Amalike; jer ti narodi življahu od starine u onoj zemlji od Sura pa do zemlje Misirske.
9 Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
I pustošaše David onu zemlju ne ostavljajuæi u životu ni èovjeka ni žene, i otimaše ovce i volove i magarce i kamile i ruho, i vraæajuæi se dolažaše k Ahisu.
10 Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
I Ahis pitaše: gdje ste danas udarali? A David govoraše: na južnu stranu Judinu, i na južnu stranu Jerameilsku, i na južnu stranu Kenejsku.
11 Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
Ali ne ostavljaše David u životu ni èovjeka ni žene da dovede u Gat govoreæi: da nas ne tuže govoreæi: tako je uradio David. I taki mu bijaše obièaj za sve vrijeme dokle bijaše u zemlji Filistejskoj.
12 Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”
I Ahis vjerovaše Davidu, i govoraše: baš se omrazio s narodom svojim Izrailjem; zato æe mi biti sluga dovijeka.

< 1 Samweli 27 >