< 1 Samweli 27 >

1 Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
Dawid jednak powiedział sobie w sercu: Któregoś dnia zginę z ręki Saula. Nie ma dla mnie nic lepszego, niż bym uszedł szybko do ziemi Filistynów. Wtedy Saul będzie zrozpaczony szukaniem mnie po wszystkich granicach Izraela. I tak ujdę z jego rąk.
2 Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
Powstał więc Dawid i wraz z sześciuset ludźmi, którzy byli z nim, poszedł do Akisza, syna Maoka, króla Gat.
3 Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
I Dawid mieszkał u Akisza w Gat, on i jego ludzie, każdy ze swoją rodziną: Dawid i jego dwie żony, Achinoam Jizreelitka i Abigail, [dawna] żona Nabala, Karmelitka.
4 Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
A gdy doniesiono Saulowi, że Dawid uciekł do Gat, przestał go szukać.
5 Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
I Dawid powiedział do Akisza: Jeśli teraz znalazłem łaskę w twoich oczach, niech mi dadzą miejsce w jednym z miast tego kraju, abym tam mieszkał. Dlaczego bowiem twój sługa miałby mieszkać w mieście królewskim wraz z tobą?
6 Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
Akisz dał mu więc w tym dniu Siklag. Dlatego Siklag należy do królów Judy aż do dziś.
7 Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
A okres, który Dawid przebywał w krainie Filistynów, wynosił rok i cztery miesiące.
8 Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
Dawid i jego ludzie wyprawiali się i najeżdżali Geszurytów, Girzytów i Amalekitów. Ci bowiem od dawna mieszkali w tej ziemi leżącej przy wejściu do Szur aż do ziemi Egiptu.
9 Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
I Dawid pustoszył tę ziemię, i nie pozostawiał przy życiu ani mężczyzny, ani kobiety. Zabierał zaś owce, woły, osły i wielbłądy, a także szaty, zawracał i przybywał do Akisza.
10 Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
A gdy Akisz pytał: Gdzie byliście dzisiaj na wyprawie? Dawid odpowiadał: Na południu Judy, na południe od Jerachmeelitów i na południe od Kenitów.
11 Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
Dawid nie zostawiał przy życiu ani mężczyzny, ani kobiety, aby ich nie przyprowadzić do Gat. Mówił: Aby nie skarżyli na nas i nie mówili: Tak uczynił Dawid i taki był jego zwyczaj przez wszystkie dni, kiedy mieszkał w ziemi Filistynów.
12 Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”
Akisz zaś wierzył Dawidowi i mówił: Został znienawidzony przez swój lud, Izrael. Pozostanie więc moim sługą na zawsze.

< 1 Samweli 27 >