< 1 Samweli 27 >

1 Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
Kinuna ni David iti nakemna, “Addanto ti aldaw a matayak babaen iti ima ni Saul; awan ti kasayaatan nga aramidek no di ti aglibas a mapan idiay daga dagiti Filisteo; Isardengton ni Saul ti panangbirbirokna kaniak iti amin a beddeng ti Israel; iti kastoy a wagas, makalibasak manipud iti imana.”
2 Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
Nagrubwat ni David ket nagdaliasatda, isuna ken dagiti innem a gasut a lallaki a kaduana, a nagturong kenni Akis nga anak ni Maoc, nga ari ti Gat.
3 Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
Nakipagnaed ni David kenni Akis idiay Gat, isuna ken dagiti tattaona, amin al lallaki agraman ti sangkabalayanna, ket kadua ni David ti dua nga asawana a ni Ahinoam a taga-Jezreel, ken ni Abigail a taga-Carmel nga asawa ni Nabal.
4 Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
Naipadamag kenni Saul a naglibas ni David a nagturong idiay Gat, isu a saannan a binirok isuna.
5 Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
Kinuna ni David kenni Akis, “No nasayaatak iti panagkitam, ikkandak koma iti maysa a lugar iti maysa kadagiti siudad iti pagilian, a mabalinko a pagnaedan: ta apay koma a makipagnaed ti adipenmo iti siudad ti ari?
6 Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
Isu nga iti dayta nga aldaw, inted ni Akis kenkuana ti Siklag; dayta ti makagapu a ti Siglak ket kukua dagiti ari ti Juda agingga kadagitoy a tiempo.
7 Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
Maysa a tawen ken uppat a bulan a nagnaed ni David iti daga dagiti Filisteo.
8 Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
Rinaut ni David ken dagiti tattaona dagiti nadumaduma a luglugar, rinautna dagiti tattao a taga-Gesur, Girzi ken Amalec; ta dagitoy dagiti agnanaed iti daga, agturong idiay Shur, agingga iti daga ti Egipto. Agnanaedda sadiay iti nabayag unayen a tiempo.
9 Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
Rinaut ni David ti daga ket awan a pulos ti imbatina a lalaki wenno babai a sibibiag; innalana dagiti karnero, dagiti baka, dagiti asno, dagiti kamelio, ken dagiti pagan-anay; kalpasan daytoy agawid isuna ket dumagas iti ayan ni Akis.
10 Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
Saludsoden ni Akis, “Siasino ti rinautmo ita nga aldaw?” Isungbat ni David, “Rinautko ti abagatan a paset ti Juda,” wenno “Ti abagatan a masakupan iti tribu ti Jerameel,” wenno “Ti abagatan a paset dagiti Kineo.”
11 Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
Awan ti sibibiag nga ibatbati ni David nga uray maysa a lalaki wenno babai a mangidanon kadagitoy idiay Gat, a kunana, “Tapno saanda nga ibaga ti maipapan kadatayo, 'Kastoy ti aramid ni David.”' Dastoy ti masansan nga ar-aramidenna iti panagnaedna iti pagilian dagiti Filisteo.
12 Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”
Namati ni Akis kenni David, a kunana, “Pinagurana iti kasta unay dagiti tattaona nga Israelita kenkuana; isu nga agbalinto isuna nga adipenko iti agnanayon.”

< 1 Samweli 27 >