< 1 Samweli 27 >

1 Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
And David saith unto his heart, 'Now am I consumed one day by the hand of Saul; there is nothing for me better than that I diligently escape unto the land of the Philistines, and Saul hath been despairing of me — of seeking me any more in all the border of Israel, and I have escaped out of his hand.'
2 Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
And David riseth, and passeth over, he and six hundred men who [are] with him, unto Achish son of Maoch king of Gath;
3 Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
and David dwelleth with Achish in Gath, he and his men, each one with his household, [even] David and his two wives, Ahinoam the Jezreelitess, and Abigail wife of Nabal the Carmelitess.
4 Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
And it is declared to Saul that David hath fled to Gath, and he hath not added any more to seek him.
5 Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
And David saith unto Achish, 'If, I pray thee, I have found grace in thine eyes, they give to me a place in one of the cities of the field, and I dwell there, yea, why doth thy servant dwell in the royal city with thee?'
6 Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
And Achish giveth to him in that day Ziklag, therefore hath Ziklag been to the kings of Judah till this day.
7 Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
And the number of the days which David hath dwelt in the field of the Philistines [is] days and four months;
8 Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
and David goeth up and his men, and they push unto the Geshurite, and the Gerizite, and the Amalekite, (for they are inhabitants of the land from of old), as thou comest in to Shur and unto the land of Egypt,
9 Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
and David hath smitten the land, and doth not keep alive man and woman, and hath taken sheep, and oxen, and asses, and camels, and garments, and turneth back, and cometh in unto Achish.
10 Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
And Achish saith, 'Whither have ye pushed to-day?' and David saith, 'Against the south of Judah, and against the south of the Jerahmeelite, and unto the south of the Kenite.'
11 Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
Neither man nor woman doth David keep alive, to bring in [word] to Gath, saying, 'Lest they declare [it] against us, saying, Thus hath David done, and thus [is] his custom all the days that he hath dwelt in the fields of the Philistines.'
12 Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”
And Achish believeth in David, saying, 'He hath made himself utterly abhorred among his people, in Israel, and hath been to me for a servant age-during.'

< 1 Samweli 27 >