< 1 Samweli 26 >

1 Hao Wazifu wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kinachotazamana na Yeshimoni?”
Les Ziphites vinrent trouver Saül à Guibea, en disant: « David ne se cache-t-il pas sur la colline de Hachila, qui est en face du désert? »
2 Hivyo Sauli akashuka kwenda katika Jangwa la Zifu, akiwa na watu wake 3,000 wa Israeli waliochaguliwa, kumsaka Daudi huko.
Alors Saül se leva et descendit au désert de Ziph, ayant avec lui trois mille hommes d'élite d'Israël, pour chercher David dans le désert de Ziph.
3 Sauli akapiga kambi yake kando ya barabara juu ya kilima cha Hakila kinachotazamana na Yeshimoni, lakini Daudi alikuwa anaishi huko jangwani. Alipoona kuwa Sauli amemfuata huko,
Saül campa sur la colline de Hakila, qui est en face du désert, sur le chemin. Mais David resta dans le désert, et il vit que Saül le poursuivait dans le désert.
4 Daudi akatuma wapelelezi na akapata habari kwa hakika kwamba Sauli alikuwa amewasili.
David envoya donc des espions, et il comprit que Saül était certainement venu.
5 Ndipo Daudi akaondoka, akaenda hadi mahali Sauli alikuwa amepiga kambi. Akaona mahali Sauli na Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi, walipokuwa wamelala. Sauli alikuwa amelala ndani ya kambi, jeshi likiwa limemzunguka.
David se leva et arriva au lieu où Saül avait campé, et il vit le lieu où Saül était couché, avec Abner, fils de Ner, chef de son armée. Saül était couché dans l'enceinte des chariots, et le peuple était campé autour de lui.
6 Basi Daudi akamuuliza Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, nduguye Yoabu, akisema, “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kambini kwa Sauli?” Abishai akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe.”
Alors David prit la parole et dit à Achimélec, le Hittite, et à Abishaï, fils de Tseruja, frère de Joab: « Qui descendra avec moi vers Saül au camp? » Abishaï répondit: « Je descendrai avec toi. »
7 Hivyo Daudi na Abishai wakaenda kwenye jeshi wakati wa usiku, tazama Sauli, alikuwa amelala ndani ya kambi na mkuki wake umekitwa ardhini karibu na kichwa chake. Abneri na askari walikuwa wamelala kumzunguka Sauli.
David et Abishaï arrivèrent de nuit auprès du peuple. Et voici que Saül était couché à l'intérieur de la place des chariots, sa lance plantée en terre à sa tête, et Abner et le peuple étaient couchés autour de lui.
8 Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemtia adui yako mikononi mwako. Sasa niruhusu nimchome mpaka ardhini kwa pigo moja la mkuki wangu; sitamchoma mara mbili.”
Alors Abishaï dit à David: « Dieu a livré aujourd'hui ton ennemi entre tes mains. Maintenant, laisse-moi donc le frapper d'un seul coup de lance en terre, et je ne le frapperai pas une seconde fois. »
9 Lakini Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize! Ni nani awezaye kutia mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana na asiwe na hatia?”
David dit à Abischaï: « Ne le fais pas périr, car qui peut étendre sa main contre l'oint de l'Éternel et être innocent? ».
10 Daudi akasema, “Hakika kama vile Bwana aishivyo, Bwana mwenyewe atampiga; au wakati wake utafika, naye atakufa, au atakwenda vitani na kuangamia.
David répondit: « L'Éternel est vivant, l'Éternel le frappera, ou son jour viendra où il mourra, ou il descendra dans la bataille et périra.
11 Lakini Mungu na apishie mbali nisije nikainua mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana. Sasa chukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyo karibu na kichwa chake, tuondoke.”
L'Éternel interdit que j'étende la main contre l'oint de l'Éternel; mais maintenant, prends la lance qui est à sa tête et la cruche d'eau, et allons-y. »
12 Hivyo Daudi akachukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyokuwa karibu na kichwa cha Sauli, nao wakaondoka. Hakuna yeyote aliyeona au kufahamu habari hii, wala hakuna hata mmoja aliyeamka usingizini. Wote walikuwa wamelala, kwa sababu Bwana alikuwa amewatia kwenye usingizi mzito.
Et David prit la lance et la cruche d'eau de la tête de Saül, et ils s'en allèrent. Personne ne le vit, ni ne le sut, et personne ne se réveilla, car ils dormaient tous, car un profond sommeil de Yahvé était tombé sur eux.
13 Kisha Daudi akavuka upande mwingine na kusimama juu ya kilima mahali palipokuwa na nafasi pana kati yao.
Alors David passa de l'autre côté, et se tint sur le sommet de la montagne, très loin, à une grande distance l'un de l'autre.
14 Daudi akalipigia kelele jeshi na Abneri mwana wa Neri, akisema, “Je, Abneri, hutanijibu?” Abneri akajibu, “Nani wewe umwitaye mfalme?”
Et David cria au peuple et à Abner, fils de Ner, en disant: « Ne réponds-tu pas, Abner? » Abner répondit: « Qui es-tu, toi qui appelles le roi? »
15 Daudi akasema, “Wewe si ni mtu shujaa? Ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukumlinda mfalme bwana wako? Mtu mmoja alikuja kumwangamiza mfalme, bwana wako.
David dit à Abner: « N'es-tu pas un homme? Qui est comme toi en Israël? Pourquoi donc n'as-tu pas veillé sur ton seigneur le roi? Car l'un d'entre eux est venu pour faire périr ton seigneur le roi.
16 Ulichokifanya si kizuri. Kwa hakika kama aishivyo Bwana, wewe na watu wako mnastahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, mpakwa mafuta wa Bwana. Tazameni hapo mlipo. Uko wapi mkuki wa mfalme na gudulia la maji ambavyo vilikuwa karibu na kichwa chake?”
Ce que tu as fait n'est pas bien. L'Éternel est vivant, tu mérites de mourir, car tu n'as pas veillé sur ton seigneur, l'oint de l'Éternel. Vois maintenant où est la lance du roi, et la jarre d'eau qui était à sa tête. »
17 Sauli akatambua sauti ya Daudi, na kusema, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akajibu, “Naam, hiyo ndiyo, bwana wangu mfalme.”
Saül reconnut la voix de David et dit: « Est-ce là ta voix, mon fils David? » David dit: « C'est ma voix, mon seigneur, ô roi. »
18 Pia akaongeza, “Kwa nini bwana wangu anamfuatia mtumishi wake? Nimefanya nini, nalo kosa langu ni lipi nililolifanya niwe na hatia?
Il dit: « Pourquoi mon seigneur poursuit-il son serviteur? Qu'ai-je fait? Quel mal y a-t-il dans ma main?
19 Sasa mfalme bwana wangu na asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama Bwana amekuchochea dhidi yangu, basi yeye na aipokee sadaka yangu. Lakini hata hivyo, kama ni wanadamu waliofanya hivyo, walaaniwe mbele za Bwana! Wao sasa wamenifukuza kutoka sehemu yangu katika urithi wa Bwana wangu wakisema, ‘Nenda ukatumikie miungu mingine.’
Maintenant, que le roi mon seigneur écoute les paroles de son serviteur. Si c'est l'Éternel qui vous a soulevés contre moi, qu'il accepte une offrande. Mais si ce sont les enfants des hommes, ils sont maudits devant l'Éternel, car ils m'ont chassé aujourd'hui pour que je ne m'attache pas à l'héritage de l'Éternel, en disant: « Va servir d'autres dieux! »
20 Basi usiache damu yangu imwagike kwenye ardhi mbali na uso wa Bwana. Mfalme wa Israeli ametoka kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware katika milima.”
Maintenant, que mon sang ne tombe pas en terre loin de la présence de l'Éternel, car le roi d'Israël est sorti pour chercher une puce, comme on chasse une perdrix dans la montagne. »
21 Ndipo Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Rudi, Daudi mwanangu. Kwa kuwa uliyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani leo, sitajaribu kukudhuru tena. Hakika nimetenda kama mpumbavu na nimekosa sana.”
Alors Saül dit: « J'ai péché. Reviens, mon fils David, car je ne te ferai plus de mal, car ma vie était aujourd'hui précieuse à tes yeux. Voici, j'ai fait l'idiot et j'ai commis une grave erreur. »
22 Daudi akajibu, “Mkuki wa mfalme uko hapa. Mmoja wa vijana wako na avuke kuuchukua.
David répondit: « Voici la lance, ô roi! Que l'un des jeunes gens vienne la chercher.
23 Bwana humlipa kila mtu kwa ajili ya haki yake na uaminifu wake. Bwana alikutia katika mikono yangu leo, lakini sikuinua mkono wangu juu ya mpakwa mafuta wa Bwana.
L'Éternel rendra à chacun sa justice et sa fidélité, car l'Éternel t'a livré aujourd'hui entre mes mains, et je n'ai pas voulu étendre ma main contre l'oint de l'Éternel.
24 Kwa hakika kama vile maisha yako yalivyokuwa ya thamani kwangu leo, vivyo hivyo maisha yangu na yawe na thamani kwa Bwana na kuniokoa kutoka taabu zote.”
Voici, comme ta vie a été respectée aujourd'hui à mes yeux, que ma vie soit respectée aux yeux de l'Éternel, et qu'il me délivre de toute oppression. »
25 Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Mwanangu Daudi na ubarikiwe; utafanya mambo makubwa na hakika utashinda.” Basi Daudi akaenda zake, naye Sauli akarudi nyumbani.
Alors Saül dit à David: « Tu es béni, mon fils David. Tu feras de grandes choses et tu seras vainqueur. » David s'en alla donc, et Saül retourna à sa place.

< 1 Samweli 26 >