< 1 Samweli 25 >

1 Basi Samweli akafa, nao Israeli wote wakakusanyika na kumwombolezea; wakamzika nyumbani kwake huko Rama. Kisha Daudi akateremka kwenye Jangwa la Maoni.
Forsothe Samuel was deed; and al Israel was gaderid to gidere, and thei biweiliden hym greetly, and birieden hym in his hows in Ramatha. And Dauid roos, and yede doun in to deseert of Faran.
2 Mtu mmoja huko Maoni, aliyekuwa na makao huko Karmeli, alikuwa tajiri sana. Alikuwa na mbuzi elfu moja na kondoo elfu tatu, aliokuwa akiwakata manyoya huko Karmeli.
Forsothe a `man was in Maon, and his possessioun was in Carmele, and thilke man was ful greet, and thre thousynde scheep and a thousynde geet `weren to hym; and it bifelde that his flocke was clippid in Carmele.
3 Jina la mtu huyo lilikuwa Nabali, naye mkewe aliitwa Abigaili. Alikuwa mwanamke mwenye busara na mzuri wa sura, lakini mumewe, ambaye alikuwa wa ukoo wa Kalebu, alikuwa mwenye hasira na mchoyo katika utendaji wake.
Forsothe the name of that man was Nabal, and the name of his wijf was Abigail; and thilke womman was moost prudent and fair; forsothe hir hosebond was hard and ful wickid and malicious; sotheli he was of the kyn of Caleph.
4 Daudi alipokuwa huko jangwani, akasikia kuwa Nabali alikuwa anakata kondoo manyoya.
Therfor whanne Dauid hadde herde in deseert, that Nabal clippide his floc,
5 Basi akatuma vijana kumi na kuwaambia, “Pandeni kwa Nabali huko Karmeli, mkamsalimie kwa jina langu.
he sente ten yonge men, and seide to hem, Stie ye in to Carmele, and ye schulen come to Nabal, and ye schulen grete hym of my name pesibli;
6 Mwambieni: ‘Amani iwe kwako! Amani iwe kwako pamoja na wa nyumbani mwako! Pia amani iwe pamoja na vyote ulivyo navyo!
and ye schulen seie thus, Pees be to my britheren and to thee, and pees be to thin hows, and pees be to alle thingis, `what euer thingis thou hast.
7 “‘Nasikia kuwa huu ni wakati wa kukata kondoo manyoya. Wachunga mifugo wako walipokuwa pamoja nasi, hatukuwatendea mabaya na wakati wote waliokuwa huko Karmeli hakuna chochote chao kilipotea.
Y herde that thi scheepherdis, that weren with vs in deseert, clippiden thi flockis; we weren neuere diseseful to hem, nether ony tyme ony thing of the floc failide to hem, in al time in which thei weren with vs in Carmele;
8 Waulize watumishi wako nao watakuambia. Kwa hiyo uwatendee wema vijana wangu, kwani tumekuja wakati wa furaha. Tafadhali wape watumishi wako na mwanao Daudi chochote kitakachokuja mkononi mwako kwa ajili yao.’”
axe thi children, and thei schulen schewe to thee. Now therfor thi children fynde grace in thin iyen; for in a good dai we camen to thee; what euer thing thin hond fyndith, yyue to thi seruauntis, and to thi sone Dauid.
9 Watu wa Daudi walipofika wakampa Nabali ujumbe huu kwa jina la Daudi. Kisha wakangojea.
And whanne the children of Dauid hadden come, thei spaken to Nabal alle these wordis in the name of Dauid, and helden pees.
10 Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Huyu Daudi ni nani? Huyu mwana wa Yese ni nani? Watumishi wengi wanakimbia kutoka kwa bwana zao siku hizi.
Forsoth Nabal answeride to the children of Dauid, and seide, Who is Dauith? and who is the sone of Isai? To dai seruauntis encreesiden that fleen her lords.
11 Kwa nini nichukue mkate wangu, maji yangu na nyama niliyochinja kwa ajili ya wakata manyoya wangu, na kuwapa watu ambao hakuna anayejua wanakotoka?”
Therfor schal Y take my looues and my watris, and the fleischis of beestis, whiche Y haue slayn to my schereris, and schal Y yyue to men, whiche Y knowe not of whennus thei ben?
12 Watu wa Daudi wakageuka na kurudi. Walipofika, wakaarifu kila neno.
Therfor the children of Dauid yeden ayen bi her weie; and thei turneden ayen, and camen, and telden to hym alle wordis whiche Nabal hadde seid.
13 Daudi akawaambia watu wake, “Jifungeni panga zenu!” Basi wakajifunga panga zao, naye Daudi akajifunga upanga wake. Watu kama mia nne hivi wakapanda pamoja na Daudi, na watu mia mbili wakabaki na vifaa.
Thanne Dauid seide to hise children, Ech man be gird with his swerd. And alle men weren gird with her swerdis, and Dauid also was gird with his swerd; and as foure hundrid men sueden Dauid, forsothe two hundrid leften at the fardels.
14 Mmoja wa watumishi akamwambia Abigaili, mkewe Nabali: “Daudi alituma wajumbe kutoka jangwani kumpa bwana wetu salamu zake, lakini akawavurumishia matukano.
Forsothe oon of hise children telde to Abigail, wijf of Nabal, and seide, Lo! Dauid sente messangeris fro deseert, that thei schulden blesse oure lord, and he turnede hem awey;
15 Hata hivyo watu hawa walikuwa wema sana kwetu. Hawakututendea mabaya, na wakati wote tulipokuwa nje huko mashambani karibu nao, hatukupotewa na kitu chochote.
these men weren good ynow, and not diseseful to vs, and no thing perischide `in ony tyme in al the tyme in which we lyueden with hem in deseert;
16 Usiku na mchana walikuwa ukuta wakituzunguka wakati wote tulipokuwa tukichunga kondoo zetu karibu nao.
thei weren to vs for a wal, bothe in niyt and in dai, in alle daies in whiche we lesewiden flockis at hem.
17 Sasa fikiri juu ya jambo hili na uone unaweza kufanya nini, kwa sababu maafa yanakaribia juu ya bwana wetu na nyumba yake yote. Yeye ni mtu mwovu kiasi kwamba hakuna mtu awezaye kuzungumza naye.”
Wherfor biholde thou, and thenke, what thou schalt do; for malice is fillid ayens thin hosebonde, and ayens `thin hows; and he is the sone of Belial, so that no man may speke to him.
18 Abigaili akafanya haraka, akachukua mikate mia mbili, viriba viwili vya divai, kondoo watano waliochinjwa vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu kavu, mikate mia mbili ya tini, akavipakia juu ya punda.
Therfor Abigail hastide, and took two hundrid looues, and two vessels of wyn, and fyue whetheris sodun, and seuene buyschelis and an half of flour, and an hundrid bundles of dried grape, and two hundrid gobetis of dried figus; and puttide on assis,
19 Kisha akawaambia watumishi wake, “Tangulieni; mimi nitakuja nyuma yenu.” Lakini hakumwambia Nabali mumewe.
and seide to hir children, Go ye bifor me; lo! Y schal sue you `aftir the bak. Forsothe sche schewide not to hir hosebonde Nabal.
20 Ikawa alipokuwa amepanda punda wake kwenye bonde la mlima, tazama, Daudi na watu wake wakawa wanateremka kumwelekea, naye akakutana nao.
Therfor whanne sche hadde stied on the asse, and cam doun `at the roote of the hil, and Dauid and hise men camen doun in to the comyng `of hir; whiche also sche mette.
21 Daudi alikuwa amesema, “Ilikuwa ni kazi bure kuchunga kwangu kote mali za huyu mtu huko jangwani hivi kwamba hakuna chochote chake kilichopotea. Yeye amenilipa baya kwa ajili ya wema.
And Dauid seide, Verili in veyn Y haue kept alle thingis that weren of this Nabal in the deseert, and no thing perischide of alle thingis that perteyneden to hym, and he hath yolde to me yuel for good.
22 Bwana na amshughulikie Daudi, tena kwa ukali, ikiwa kesho asubuhi nitambakizia mwanaume hata mmoja aliye hai miongoni mwa watu wake wote!”
The Lord do these thingis, and adde these thingis to the enemyes of Dauid, if Y schal leeue of alle thingis that perteynen to him til the morewe a pisser to the wal.
23 Abigaili alipomwona Daudi, akashuka haraka kwenye punda wake, akainama kifudifudi uso wake mpaka nchi mbele ya Daudi.
Sotheli whanne Abigail siy Dauid, sche hastide, and yede doun of the asse; and sche fel doun bifor Dauid on hir face, and worschipide on the erthe.
24 Akamwangukia miguuni pake na kusema: “Bwana wangu, kosa hili na liwe juu yangu mwenyewe. Tafadhali mruhusu mtumishi wako aseme nawe. Sikia kile mtumishi wako atakachosema.
And sche felde doun to hise feet, and seide, My lord the kyng, this wickydnesse be in me; Y biseche, speke thin handmayden in thin eeris, and here thou the wordis of thi seruauntesse;
25 Bwana wangu na asimjali huyo mtu mwovu Nabali. Yeye anafanana na jina lake; jina lake ni Mpumbavu, nao upumbavu huenda pamoja naye. Lakini kwangu mimi, mtumishi wako, sikuwaona hao watu waliotumwa na bwana wangu.
Y preie, my lord the kyng, sette not his herte on this wickid man Nabal, for bi his name he is a fool, and foli is with hym; but, my lord, Y thin handmayde siy not thi children, whiche thou sentist.
26 “Basi sasa, kwa kuwa Bwana amekuzuia, wewe bwana wangu, kutokumwaga damu na kutolipiza kisasi kwa mikono yako mwenyewe, hakika kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, maadui zako na wote wanaokusudia kumdhuru bwana wangu wawe kama Nabali.
Now therfor, my lord, the Lord lyueth, and thi soule lyueth, which Lord forbeed thee, lest thou schuldist come in to blood, and he sauede thi soule to thee; and now thin enemyes, and thei that seken yuel to my lord, be maad as Nabal.
27 Nayo zawadi hii ambayo mtumishi wako amemletea bwana wangu, wapewe watu wanaofuatana nawe.
Wherfor resseyue thou this blessyng, which thin handmaide brouyte to thee, my lord, and yyue thou to the children that suen thee, my lord.
28 Tafadhali samehe kosa la mtumishi wako, kwa kuwa Bwana kwa hakika ataifanya imara nyumba ya ufalme kwa bwana wangu, kwa sababu anapigana vita vya Bwana.
Do thou awey the wickidnesse of thi seruauntesse; for the Lord makynge schal make a feithful hows to thee, my lord, for thou, my lord, fiytist the batels of the Lord; therfor malice be not foundun in thee in alle dais of thi lijf.
29 Hata ingawa yuko mtu anayekufuatia kuuondoa uhai wako, usiruhusu baya lolote kuonekana kwako siku zote za maisha yako, uhai wa bwana wangu utafungwa salama kwenye furushi la walio hai na Bwana Mungu wako. Lakini uhai wa adui zako atavurumishwa kama vile jiwe kutoka kwenye kombeo.
For if a man risith ony tyme, and pursueth thee, and sekith thi lijf, the lijf of my lord schal be kept as in a bundel of lyuynge trees, at thi Lord God; forsothe the soule of thin enemyes schal be hurlid round aboute as in feersnesse, and sercle of a slynge.
30 Bwana atakapokuwa ameshamtendea bwana wangu kila kitu chema alichoahidi kumhusu yeye na kumweka kuwa kiongozi wa Israeli,
Therfor whanne the Lord hath do to thee, my lord, alle these goode thingis, whiche he spak of thee, and hath ordeyned thee duyk on Israel,
31 bwana wangu hatakuwa na dhamiri inayolemewa na mzigo kwa kumwaga damu kusiko na sababu, au kujilipizia kisasi yeye mwenyewe. Bwana atakapomletea bwana wangu mafanikio, umkumbuke mtumishi wako.”
this schal not be in to siyyng and in to doute of herte to thee, my lord, that thou hast sched out giltles blood, ether that thou hast vengid thee. And whanne the Lord hath do wel to thee, my lord, thou schalt haue mynde on thin handmaide, and thou schalt do wel to hir.
32 Daudi akamwambia Abigaili, “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli aliyekutuma kunilaki leo.
And Dauid seide to Abigail, Blessid be the Lord God of Israel, that sente thee to dai in to my comyng, and blessid be thi speche;
33 Ubarikiwe kwa uamuzi wako mzuri na kwa kunizuia nisimwage damu leo na kulipiza kisasi kwa mikono yangu.
and blessid be thou, that hast forbede me, lest Y yede to blood, and vengide me with myn hond;
34 La sivyo, hakika kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisiwadhuru, kama usingekuja haraka kunilaki, hakuna hata mwanaume mmoja wa Nabali angeachwa hai kufikia mapambazuko.”
ellis the Lord God of Israel lyueth, which forbeed me, `lest Y dide yuel to thee, if thou haddist not soone come in to `metyng to me, a pissere to the wal schulde not haue left to Nabal til to the morewe liyt.
35 Ndipo Daudi akapokea kutoka mkononi mwake kile alichokuwa amemletea, naye akasema, “Nenda nyumbani kwako kwa amani; nimesikia maneno yako na kukujalia ombi lako.”
Therfor Dauid resseyuede of hir hond alle thingis whiche sche hadde brouyt to hym; and he seide to hir, Go thou in pees in to thin hows; lo! Y herde thi vois, and Y onouride thi face.
36 Abigaili alipokwenda kwa Nabali, alikuwa ndani ya nyumba yake akifanya karamu kama ile ya mfalme. Naye alikuwa ana furaha nyingi, akiwa amelewa sana. Kwa hiyo Abigaili hakumwambia mumewe kitu chochote mpaka asubuhi yake.
Forsothe Abigail cam to Nabal; and, lo! a feeste was to him in his hows, as the feeste of a kyng; and the herte of Nabal was iocounde, for he was `drunkun greetli; and sche schewide not to hym a word litil ether greet til the morewe.
37 Basi asubuhi, Nabali alipokuwa amelevuka, mkewe akamwambia mambo yote, nao moyo wake ukazimia, akawa kama jiwe.
Forsothe in the morewtid, whanne Nabal hadde defied the wiyn, his wijf schewide to hym alle these wordis; and his herte was almest deed with ynne, and he was maad as a stoon.
38 Baada ya siku kumi, Bwana akampiga Nabali, naye akafa.
And whanne ten daies hadden passid, the Lord smoot Nabal, and he was deed.
39 Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “Ahimidiwe Bwana, ambaye amenitetea shauri langu dhidi ya Nabali kwa kuwa alinitendea kwa dharau. Amemzuia mtumishi wake asitende mabaya na Bwana ameuleta ubaya wa Nabali juu ya kichwa chake mwenyewe.” Kisha Daudi akatuma ujumbe kwa Abigaili kumwomba awe mke wake.
Which thing whanne Dauid hadde herd, Nabal deed, he seide, Blessid be the Lord God, that vengide the cause of my schenschip of the hond of Nabal, and kepte his seruaunt fro yuel, and the Lord yeldide the malice of Nabal in to the heed of hym. Therfor Dauid sente, and spak to Abigail, that he wolde take hir wijf to hym.
40 Watumishi wa Daudi wakaenda mpaka Karmeli na kumwambia Abigaili, wakisema, “Daudi ametutuma kwako kukuchukua uwe mkewe.”
And the children of Dauid camen to Abigail in to Carmele, and spaken to hir, and seiden, Dauid sente vs to thee, that he take thee in to wijf to hym.
41 Akainama chini uso wake mpaka ardhini, akasema, “Mjakazi wako yuko hapa, tayari kuwatumikia na kuwanawisha miguu watumishi wa bwana wangu.”
And sche roos, and worschipide lowe to erthe, and seide, Lo! thi seruauntesse be in to an handmayde, that sche waische the feet of the seruauntis of my lord.
42 Abigaili akainuka kwa haraka, akapanda punda wake, akihudumiwa na wajakazi wake watano, akaenda pamoja na wajumbe wa Daudi, naye akawa mkewe.
And Abigail hastide, and roos, and stiede on an asse; and fyue damesels, sueris of hir feet, yeden with hir, and sche suede the messangeris of Dauid, and was maad wijf to hym.
43 Pia Daudi alikuwa amemwoa Ahinoamu wa Yezreeli, wote wawili wakawa wake zake.
But also Dauid took Achynoem of Jezrael, and euer eithir was wijf to hym;
44 Lakini Sauli alikuwa amemwoza Mikali binti yake, aliyekuwa mkewe Daudi, kwa Palti mwana wa Laishi, kutoka Galimu.
forsothe Saul yaf Mycol his douytir, wijf of Dauid, to Phalti, the sone of Lais, that was of Gallym.

< 1 Samweli 25 >