< 1 Samweli 24 >

1 Baada ya Sauli kurudi kuwafuatia Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika Jangwa la En-Gedi.”
Et lorsque Saül fut revenu, après avoir poursuivi les Philistins, on lui porta une nouvelle, en disant: Voilà que David est dans le désert d’Engaddi.
2 Basi Sauli akachukua watu hodari 3,000 kutoka Israeli yote kwenda kumsaka Daudi na watu wake karibu na Majabali ya Mbuzi-Mwitu.
Saül donc, prenant trois mille hommes choisis de tout Israël, alla pour chercher David et ses hommes, même sur les rochers les plus escarpés, qui sont accessibles seulement aux chamois.
3 Akaja mpaka kwenye mazizi ya kondoo kando ya njia, hapo palikuwa na pango, na Sauli akaingia ndani kujipumzisha. Daudi na watu wake walikuwa wamo mle pangoni kwa ndani zaidi.
Et il vint aux parcs de brebis, qui s’offraient à lui pendant qu’il était en chemin; et il y avait là une caverne, dans laquelle entra Saul pour un besoin naturel: or, David et ses hommes étaient cachés dans la partie intérieure de la caverne.
4 Watu wa Daudi wakasema, “Hii ndiyo siku aliyonena Bwana akikuambia, ‘Nitamtia adui yako mikononi mwako ili wewe umtendee utakavyo.’” Basi Daudi akanyemelea bila kuonekana na kukata upindo wa joho la Sauli.
Et les serviteurs de David lui dirent: Voici le jour dont le Seigneur vous a dit: C’est moi qui te livrerai ton ennemi, afin que tu lui fasses comme il plaira à tes yeux. David se leva donc, et coupa sans bruit le bord du manteau de Saül.
5 Baada ya hilo, dhamiri ya Daudi ikataabika kwa kukata upindo wa joho la Sauli.
Après cela David frappa sa poitrine de ce qu’il avait coupé le bord du manteau de Saül.
6 Akawaambia watu wake, “Bwana na apishie mbali nisije nikafanya jambo kama hilo kwa bwana wangu, yeye ambaye ni mpakwa mafuta wa Bwana, au kuinua mkono wangu dhidi yake; kwani yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.”
Et il dit à ses hommes: Que le Seigneur me soit propice, afin que je ne commette point ce crime contre mon seigneur, le christ du Seigneur, que de porter ma main sur lui, parce qu’il est le christ du Seigneur.
7 Kwa maneno haya Daudi akawaonya watu wake na hakuwaruhusu wamshambulie Sauli. Naye Sauli akaondoka pangoni na kwenda zake.
Et David réprima ses hommes par ses paroles, et il ne permit pas qu’ils s’élevassent contre Saül: or, Saül se levant de la caverne, continuait son chemin commencé.
8 Ndipo Daudi naye akatoka pangoni na kumwita Sauli akisema, “Mfalme, bwana wangu!” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama na kusujudu uso wake mpaka nchi.
Or David se leva aussi après lui; et, sorti de la caverne, il cria derrière Saül, disant: Mon seigneur roi! Et Saül regarda derrière lui, et David, s’inclinant penché vers la terre, se prosterna,
9 Akamwambia Sauli, “Kwa nini unasikiliza wakati watu wanapokuambia, ‘Daudi amenuia kukudhuru’?
Et dit à Saül: Pourquoi écoutez-vous les paroles d’hommes qui disent: David cherche votre perte?
10 Leo umeona kwa macho yako mwenyewe jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu huko pangoni. Watu wengine walisisitiza nikuue, lakini nilikuacha, nikisema, ‘Sitainua mkono wangu dhidi ya bwana wangu, kwa sababu yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.’
Voilà qu’aujourd’hui vos yeux ont vu que le Seigneur vous a livré à ma main dans la caverne; et j’ai pensé à vous tuer, mais mon œil vous a épargné; car j’ai dit: Je n’étendrai pas ma main sur mon seigneur, parce que c’est le christ du Seigneur.
11 Tazama, baba yangu, ona kipande hiki cha joho lako mkononi mwangu! Nilikata upindo wa joho lako lakini sikukuua. Basi ujue na kutambua kuwa sina hatia ya kutenda mabaya wala ya kuasi. Wewe sijakukosea, lakini wewe unaniwinda mimi ili kuuondoa uhai wangu.
Bien plus, mon père, voyez, et reconnaissez le bord de votre manteau dans ma main, et que quand j’ai coupé l’extrémité de votre manteau, je n’ai pas étendu ma main sur vous; remarquez et voyez qu’il n’y a pas de mal en ma main, ni d’iniquité, et que je n’ai pas péché contre vous; mais vous, vous tendez des embûches à mon âme, pour la détruire.
12 Bwana na ahukumu kati yangu na wewe. Naye Bwana alipize mabaya unayonitendea, lakini mkono wangu hautakugusa.
Que le Seigneur juge entre moi et vous, et que le Seigneur me venge de vous; mais que ma main ne soit pas sur vous.
13 Kama msemo wa kale usemavyo, ‘Kutoka kwa watenda maovu hutoka matendo maovu,’ kwa hiyo mkono wangu hautakugusa wewe.
Comme il est dit aussi dans l’ancien proverbe: C’est des impies que sortira l’impiété: que ma main donc ne soit pas sur vous.
14 “Je, mfalme wa Israeli ametoka dhidi ya nani? Ni nani unayemfuatia? Je, ni mbwa mfu? Ni kiroboto?
Qui poursuivez-vous, roi d’Israël? qui poursuivez-vous? c’est un chien mort que vous poursuivez, et une puce.
15 Bwana na awe mwamuzi wetu, yeye na aamue kati yetu. Yeye na anitetee shauri langu; anihesabie haki kwa kuniokoa mkononi mwako.”
Que le Seigneur soit juge, et qu’il juge entre moi et vous; qu’il voie et juge ma cause et qu’il me délivre de votre main.
16 Daudi alipomaliza kusema haya, Sauli akamuuliza, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Ndipo Sauli akalia kwa sauti kuu, akisema,
Or, lorsque David eut achevé de tenir ces discours à Saül, Saül dit: N’est-ce point là ta voix, mon fils David? Et Saül éleva sa voix, et pleura;
17 “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi; umenitendea mema, lakini mimi nimekutendea mabaya.
Puis il dit à David: Tu es plus juste que moi, toi; car toi, tu m’as fait du bien, et moi, je t’ai rendu du mal.
18 Sasa umeniambia juu ya mema uliyonitendea. Bwana alinitia mikononi mwako, lakini wewe hukuniua.
C’est même toi qui m’as montré aujourd’hui le bien que tu m’as fait: comment le Seigneur m’a livré à ta main, et comment tu ne m’as point tué.
19 Je, mtu ampatapo adui yake, humwacha aende zake bila kumdhuru? Bwana na akulipe mema kwa jinsi ulivyonitenda leo.
Qui, en effet, lorsqu’il a trouvé son ennemi, le laisse aller dans une bonne voie? Mais que le Seigneur te paie de retour, pour ce que tu as fait aujourd’hui à mon égard.
20 Ninajua kwamba hakika utakuwa mfalme na ya kwamba ufalme wa Israeli utakuwa imara mikononi mwako.
Et maintenant comme je sais que très certainement tu dois régner, et que tu dois avoir en ta main le royaume d’Israël,
21 Sasa niapie kwa Bwana kwamba hutakatilia mbali uzao wangu wala kulifuta jina langu kutoka jamaa ya baba yangu.”
Jure-moi par le Seigneur que tu ne détruiras point ma race après moi, et que tu n’ôteras pas mon nom de la maison de mon père.
22 Basi Daudi akamwapia Sauli. Kisha Sauli akarudi zake nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.
Et David le jura à Saül. Saul donc s’en alla en sa maison; et David et ses hommes montèrent dans des lieux plus sûrs.

< 1 Samweli 24 >