< 1 Samweli 24 >

1 Baada ya Sauli kurudi kuwafuatia Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika Jangwa la En-Gedi.”
And whanne Saul turnede ayen, aftir that he pursuede Filisteis, thei telden to hym, and seiden, Lo! Dauid is in the deseert of Engaddi.
2 Basi Sauli akachukua watu hodari 3,000 kutoka Israeli yote kwenda kumsaka Daudi na watu wake karibu na Majabali ya Mbuzi-Mwitu.
Therfor Saul took three thousinde of chosun men of al Israel, and yede to seke Dauid and hise men, yhe on moost brokun rochis, that ben `able to weie to wield geet aloone.
3 Akaja mpaka kwenye mazizi ya kondoo kando ya njia, hapo palikuwa na pango, na Sauli akaingia ndani kujipumzisha. Daudi na watu wake walikuwa wamo mle pangoni kwa ndani zaidi.
And he cam to the fooldis of scheep, that offriden hem silf to the wei goere. And there was a denne, in to which denne Saul entride, that he schulde purge the wombe; forsothe Dauid and hise men weren hid in the ynnere part of the denne.
4 Watu wa Daudi wakasema, “Hii ndiyo siku aliyonena Bwana akikuambia, ‘Nitamtia adui yako mikononi mwako ili wewe umtendee utakavyo.’” Basi Daudi akanyemelea bila kuonekana na kukata upindo wa joho la Sauli.
And the seruauntis of Dauid seiden to hym, Lo! the dai of which the Lord spak to the, Y schal bitake to thee thin enemy, that thou do to hym as it plesith in thin iyen. Therfor Dauid roos, and kittide the hemme of the mentil of Saul priuely.
5 Baada ya hilo, dhamiri ya Daudi ikataabika kwa kukata upindo wa joho la Sauli.
Aftir these thingis Dauid smoot his herte, for he hadde kit awei the hemme of the mentil of Saul.
6 Akawaambia watu wake, “Bwana na apishie mbali nisije nikafanya jambo kama hilo kwa bwana wangu, yeye ambaye ni mpakwa mafuta wa Bwana, au kuinua mkono wangu dhidi yake; kwani yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.”
And Dauid seide to hise men, The Lord be merciful to me, lest Y do this thing to my lord, the crist of the Lord, that Y sende myn hond `in to hym, for he is the crist of the Lord. The Lord lyueth, for no but the Lord smyte hym, ether his dai come, that he die, ether he go doun in to batel and perische, the Lord be merciful to me, that Y sende not myn hond in to the crist of the Lord.
7 Kwa maneno haya Daudi akawaonya watu wake na hakuwaruhusu wamshambulie Sauli. Naye Sauli akaondoka pangoni na kwenda zake.
Forsothe Saul roos out of the denne, and yede in the weie bigunnun.
8 Ndipo Daudi naye akatoka pangoni na kumwita Sauli akisema, “Mfalme, bwana wangu!” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama na kusujudu uso wake mpaka nchi.
Sotheli Dauid roos aftir hym, and he yede out of the denne, and criede aftir the bak of Saul, and seide, My lord, the kyng! And Saul bihelde bihinde him silf; and Dauid bowide hym silf lowe to the erthe, and worschipide.
9 Akamwambia Sauli, “Kwa nini unasikiliza wakati watu wanapokuambia, ‘Daudi amenuia kukudhuru’?
And he seide to Saul, Whi herist thou the wordis of men spekynge, Dauid sekith yuel ayens thee?
10 Leo umeona kwa macho yako mwenyewe jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu huko pangoni. Watu wengine walisisitiza nikuue, lakini nilikuacha, nikisema, ‘Sitainua mkono wangu dhidi ya bwana wangu, kwa sababu yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.’
Lo! to dai thin iyen siyen, that the Lord bitook thee in myn hond in the denne, and Y thouyte that Y wolde sle thee, but myn iye sparide thee; for Y seide, Y schal not holde forth myn hond in to my lord, which is the crist, `that is, anoyntid, of the Lord.
11 Tazama, baba yangu, ona kipande hiki cha joho lako mkononi mwangu! Nilikata upindo wa joho lako lakini sikukuua. Basi ujue na kutambua kuwa sina hatia ya kutenda mabaya wala ya kuasi. Wewe sijakukosea, lakini wewe unaniwinda mimi ili kuuondoa uhai wangu.
But rathere, my fadir, se thou, and knowe the hemme of thi mentil in myn hond, for whanne Y kittide aweie the hemme of thi mentil, Y nolde holde forth myn hond in thee; perseyue thou, and see, for nether yuel nether wickidnesse is in myn hond, nether Y synnede ayens thee; but thou aspiest my lijf, that thou do it awei.
12 Bwana na ahukumu kati yangu na wewe. Naye Bwana alipize mabaya unayonitendea, lakini mkono wangu hautakugusa.
The Lord deme bitwixe me and thee, and the Lord venge me of thee; but myn hond be not in thee,
13 Kama msemo wa kale usemavyo, ‘Kutoka kwa watenda maovu hutoka matendo maovu,’ kwa hiyo mkono wangu hautakugusa wewe.
as it is seid also in eld prouerbe, Wickidnesse schal go out of wickid men; therfor myn hond be not in thee.
14 “Je, mfalme wa Israeli ametoka dhidi ya nani? Ni nani unayemfuatia? Je, ni mbwa mfu? Ni kiroboto?
`Whom pursuest thou, kyng of Israel, whom pursuest thou? Thou pursuest a deed hound, and a quyk fle.
15 Bwana na awe mwamuzi wetu, yeye na aamue kati yetu. Yeye na anitetee shauri langu; anihesabie haki kwa kuniokoa mkononi mwako.”
The Lord be iuge, and the Lord deme bitwixe me and thee, and se, and deme my cause, and delyuere me fro thin hond.
16 Daudi alipomaliza kusema haya, Sauli akamuuliza, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Ndipo Sauli akalia kwa sauti kuu, akisema,
Sotheli whanne Dauid hadde fillid spekynge siche wordis to Saul, Saul seide, Whether this is thi vois, my sone Dauid? And Saul reiside his vois, and wepte.
17 “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi; umenitendea mema, lakini mimi nimekutendea mabaya.
And he seide to Dauid, Thou art more iust than Y; for thou yauest goodis to me; forsothe Y yeldide yuelis to thee.
18 Sasa umeniambia juu ya mema uliyonitendea. Bwana alinitia mikononi mwako, lakini wewe hukuniua.
And thou schewidist to me to dai, what goodis thou hast do to me, how the Lord bitook me in thin hond, and thou killidist not me.
19 Je, mtu ampatapo adui yake, humwacha aende zake bila kumdhuru? Bwana na akulipe mema kwa jinsi ulivyonitenda leo.
For who, `whanne he fyndith his enemy, schal delyuere hym in good weie? But the Lord yelde to thee this while, for that, that thou wrouytist to dai in me.
20 Ninajua kwamba hakika utakuwa mfalme na ya kwamba ufalme wa Israeli utakuwa imara mikononi mwako.
And now, for Y woot, that thou schalt regne moost certeynli, and schalt haue in thin hond the rewme of Israel, swere thou to me in the Lord,
21 Sasa niapie kwa Bwana kwamba hutakatilia mbali uzao wangu wala kulifuta jina langu kutoka jamaa ya baba yangu.”
that thou do not a wei my seed aftir me, nether take a wey my name fro the hows of my fadir.
22 Basi Daudi akamwapia Sauli. Kisha Sauli akarudi zake nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.
And Dauid swoor to Saul. Therfor Saul yede in to his hows, and Dauid and hise men stieden to sikire placis.

< 1 Samweli 24 >