< 1 Samweli 23 >
1 Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
Davudus xabar abayle: – Filiştinar Qeilalqa k'yoptul, maadın attabı vod q'əra qa'a.
2 akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
Davudee Rəbbike qiyghanan: – Hark'ın Filiştinaaşika səyxene? Rəbbee Davuduk'le eyhen: – Hudoora k'yootle, Filiştinaaşike Qeila g'attivxhan hee'e.
3 Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
Davudne insanaaşemee, Davuduk'le eyhen: – Şi inyaa'acab, Yahudayne cigabışeecab q'əvəyq'ən. Filiştinaaşde Qeilayeene g'oşunbışde ögeeqa şi nəxübne qığeepç'es?
4 Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
Davudee meed Rəbbike qiyghan, Rəbbeeyid mang'uk'le eyhen: – Oza qıxha Qeilayeeqa hak'ne. Zı Filiştinar yiğne xılyaqa qevles.
5 Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
Davudun insanar Qeilayeeqa hapk'ın, maane Filiştinaaşilqa k'yoohar. Manbışin çavra-vəq'ə Davudee g'ahayşu qıkkekkan. Davudee Filiştınbışilqa ver ablyav'u, Qeilayn millet g'attixhan ha'an.
6 (Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
(Mançile oğiylid Aximelekne dixee Evyataree Qeilayeeqa Davudne k'anyaqa g'adayxhvan qöömee, kaahinaaşin ileylığ adayle.)
7 Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
Davud Qeilayeeqa arıva Şaululqa hixhar ha'an. Şaulee eyhen: – Allaheecar mana yizde xılyaqa quvu. Mana ç'ak'ın akkabınaneyiy sat'ulbınane şahareeqa ikkeç'u, vucee cun ögü ı'xı'.
8 Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
Şaulee Qeilayee Davudıy cukan insanar avqasva, gırgına g'oşun dəv'əys sa'a.
9 Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
Davuduk'le Şaulee cuk qəlasın ha'as ıxhay ats'anniy. Mang'vee kaahin Evyatarık'le eyhen: – Kaahinaaşin ileylığ inyaqa qale.
10 Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
Davudeecad meed sak'ı, eyhen: – İzrailyna Allah eyxhena, Rəbb, zak'le g'ayxhiyn, zal-alla Şaulus Qeilayeeqa arı şahar q'əra qaa'asıb vukkan.
11 Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
Qeilayne milletın zı mang'une xılyaqa qelesdaniyxan? Zak'le, Yiğne nukarık'le, g'ayxhiyn ixhesınne, Şaul inyaqa ayresdane? İzrailyna Allah eyxhena, Rəbb, hucoona ixhes, man zak'le eyhe. Rəbbee «Mana ayresdava» alidghıniy qele.
12 Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
Mane gahıl Davudee meed qiyghanan: – Qeilayne milletın, zınayiy yizın insanar mang'une xılyaqa qevlesınbıniyxan? Rəbbee «Qevlesınbıva» eyhe.
13 Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
Davud yixhıd vəşşılqa ələəne insanıka Qeilayeençe qığeç'u, inyaa-şa axva giyğal. Davud Qeilayeençe hixu ark'ınnava, Şaululqa hixhar hı'ımee, mang'vee cuna fıkır badal haa'ana, maqa hayk'an deş.
14 Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
Davud xılyaqa gidexhasde xhinene cigabışee, Zif eyhene sahrayne tepabışee axva eyxhe. Şaulee mana yiğıscar t'abal ha'a ıxha, Allaheemee Davud mang'une xılyaqa gixhas haysar deş.
15 Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
Davud Zifne sahreene Xoreşnang'a mang'uk'le g'iyxhen, Şaulee vucur gik'asva t'abal ha'a.
16 Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
Şaulna dix Yonatan Xoreşeeqa Davudne k'anyaqa arı, mang'us Allahne doyule yik'bı hele.
17 Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
Davuduk'le mang'vee eyhen: – Qı'məyq'ən, yizde dekkıne Şaulne xılyaqa ğu gixhas deş. Ğu İzrailyna paççah ixhes, zınar vale qiyğiyna q'ör'esda insan. Man yizde dekkık'le Şauluk'led çikana ats'an.
18 Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
Qiyğa manbışde q'öng'eesana sana-sang'us Rəbbine ögil cuvab hele. Mançe Yonatan ayk'anna xaaqa, Davudur Xoreş axva.
19 Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
Zifğançenbı Giveayeeqa Şaulusqa abı, eyhen: – Davud yişde k'anene, Yeşimonne canubılyne Xakilayne tepalyne Xoreşee xıl hidixharasde cigabışee dyugulyxha vor.
20 Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
Paççah, vas mısayiy ıkkan, maqa ayre, şicar aqqı mana yiğne xılyaqa qelesda.
21 Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
Şaulee eyhen: – Zas yugvalla hav'uynçil-alla, Rəbbee şos barakat helecen.
22 Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
Sayıb hapk'ın yugda ats'axhxhe, mang'vee g'el nyaqayiy gixhxhı, şavuk'leyiy mana maa'ar g'acu. Zak'le mana süvə xhinnena insan vorva g'ayxhı.
23 Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
Mana dyugulexhen cigabı gırgınbı ats'axhxhe, yugda ats'axhxhad, zasqa savk'le. Zınar maqa şoka ı'qqəsda. Mana nimeletteyiy ine ölkee Yahudee, zı mana gırgınəəng'ə t'abal ha'asda. Mana inçeğana ixheene, mana zı Yahudavolle gırgınəəng'ə t'abal ha'asda.
24 Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
Zifğançenbı oza qeepxha Şaulne ögee Zifqa avayk'an. Davudıy cun insanar Yeşimonne canubılyne, Arava eyhene cigayne Maonne sahree vuxha.
25 Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
Şaulıy cun insanar mana t'abal ha'asva, mane cigeeqa havayk'an. Man Davudulqa hixhar hı'ımee, mana ganznane cigeeqa qarı, Maonne sahree ulyoyzar. Şauluk'le man ats'axhxhamee, Maonne sahree Davuduqar qihna gexha.
26 Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
Şaul cune insanaaşika suvane ine surale, Davudur cune insanaaşika suvane şene surale əlyhəə vooxhe. Davudus, Şaulıle hixu, dyugulyxhes ıkkiykan. Şaulusmee mang'un ögü ı'xı', mana aqqas ıkkiykan.
27 mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
Mane gahıl Şaulusqa xabar ana sa insan arı eyhen: – Zaara ixhe, yı'q'əlqa sak'le, yişde ölkalqa Filiştinar k'yoptul.
28 Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
Şaulee, Davuduqa qihna girxhuy g'aletçu, mançe ayk'anna Filiştinaaşika səyxəs. Mançil-alla mane cigays Sela-Hammaxleqotva (Curepxhayn Ganz) do giyxhe.
29 Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.
Davud mançe En-Gedi eyhene cigeene xıl hidixharasde cigabışeeqa ayk'an.