< 1 Samweli 23 >
1 Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
Or, on fit ce rapport à David, et on lui dit: Voilà les Philistins qui font la guerre à Keïla, et qui pillent les aires.
2 akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
Et David consulta l'Éternel, en disant: Irai-je, et frapperai-je ces Philistins? Et l'Éternel répondit à David: Va, et tu frapperas les Philistins, et tu délivreras Keïla.
3 Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
Et les gens de David lui dirent: Voici, nous avons peur ici dans le pays de Juda; que sera-ce donc si nous allons à Keïla, contre les troupes des Philistins?
4 Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
C'est pourquoi David consulta encore l'Éternel; et l'Éternel lui répondit, et dit: Lève-toi, descends à Keïla; car je livrerai les Philistins entre tes mains.
5 Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
Alors David s'en alla avec ses gens à Keïla, et combattit les Philistins, et emmena leur bétail, et il en fit un grand carnage; et David délivra les habitants de Keïla.
6 (Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
Or, quand Abiathar, fils d'Achimélec, s'enfuit vers David à Keïla, il y descendit, ayant l'éphod entre les mains.
7 Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
Et on rapporta à Saül que David était venu à Keïla; et Saül dit: Dieu l'a livré entre mes mains; car, en entrant dans une ville qui a des portes et des barres, il s'est enfermé.
8 Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
Et Saül convoqua tout le peuple à la guerre, pour descendre à Keïla, afin d'assiéger David et ses gens.
9 Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
Mais David, ayant su que Saül machinait contre lui pour le perdre, dit au sacrificateur Abiathar: Apporte l'éphod.
10 Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
Puis David dit: Éternel, Dieu d'Israël, ton serviteur a entendu dire que Saül cherche à venir contre Keïla, pour détruire la ville à cause de moi;
11 Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
Les chefs de Keïla me livreront-ils entre ses mains? Saül descendra-t-il, comme ton serviteur l'a entendu dire? Éternel, Dieu d'Israël, enseigne-le, je te prie, à ton serviteur. Et l'Éternel répondit: Il descendra.
12 Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
David dit encore: Les chefs de Keïla me livreront-ils, moi et mes gens, entre les mains de Saül? Et l'Éternel répondit: Ils te livreront.
13 Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
Alors David se leva avec ses gens, environ six cents hommes, et ils sortirent de Keïla, et s'en allèrent où ils purent; et on rapporta à Saül que David s'était sauvé de Keïla; et il cessa de marcher.
14 Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
Or David demeura au désert, dans des lieux forts, et il se tint sur la montagne, au désert de Ziph. Et Saül le cherchait tous les jours; mais Dieu ne le livra point entre ses mains.
15 Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
David, voyant donc que Saül était sorti pour chercher sa vie, se tenait au désert de Ziph, dans la forêt.
16 Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
Alors Jonathan, fils de Saül, se leva, et s'en alla vers David, à la forêt, et le fortifia en Dieu;
17 Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
Et il lui dit: Ne crains point; car la main de Saül, mon père, ne te trouvera point, mais tu régneras sur Israël, et moi je serai le second après toi; et Saül, mon père, le sait bien aussi.
18 Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
Ils traitèrent donc, tous deux, alliance devant l'Éternel. Et David demeura dans la forêt, et Jonathan retourna en sa maison.
19 Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
Or, les Ziphiens montèrent vers Saül à Guibea, et lui dirent: David ne se tient-il pas caché parmi nous, dans les lieux forts, dans la forêt, au coteau de Hakila, qui est au midi de la région désolée?
20 Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
Maintenant donc, ô roi, si tu souhaites de descendre, descends et ce sera à nous de le livrer entre les mains du roi.
21 Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
Et Saül dit: Que l'Éternel vous bénisse, de ce que vous avez eu pitié de moi!
22 Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
Allez donc, faites encore attention; sachez et reconnaissez le lieu où il a posé son pied, et qui l'y a vu; car on m'a dit qu'il est fort rusé.
23 Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
Reconnaissez donc et sachez quelle est, de toutes les retraites, celle où il est caché; puis revenez vers moi, quand vous en serez assurés, et j'irai avec vous. Et s'il est dans le pays, je le chercherai soigneusement dans tous les milliers de Juda.
24 Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
Ils se levèrent donc et s'en allèrent à Ziph, devant Saül; mais David et ses gens étaient au désert de Maon, dans la plaine, au midi de la région désolée.
25 Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
Ainsi Saül et ses gens allèrent à la recherche; mais on le rapporta à David, et il descendit le rocher et demeura au désert de Maon. Saül, l'ayant appris, poursuivit David au désert de Maon.
26 Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
Et Saül marchait d'un côté de la montagne, et David et ses gens allaient de l'autre côté de la montagne; et David se hâtait de s'en aller de devant Saül. Mais comme Saül et ses gens environnaient David et les siens pour les prendre,
27 mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
Un messager vint vers Saül, et lui dit: Hâte-toi, et viens; car les Philistins se sont jetés sur le pays.
28 Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
Alors Saül s'en retourna de la poursuite de David, et s'en alla à la rencontre des Philistins. C'est pourquoi l'on a appelé ce lieu-là, Séla-Hammachlékoth (Rocher des Évasions).
29 Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.
Puis David monta de là, et demeura dans les lieux forts d'En-Guédi.