< 1 Samweli 23 >
1 Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
And people told to David saying there! [the] Philistines [are] fighting against Keilah and they [are] plundering the threshing floors.
2 akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
And he enquired David by Yahweh saying ¿ will I go and will I strike? the Philistines these. And he said Yahweh to David go and you will strike the Philistines and you will deliver Keilah.
3 Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
And they said [the] men of David to him here! we here in Judah [are] fearful and indeed? if we will go Keilah against [the] battle lines of [the] Philistines.
4 Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
And he repeated again David to enquire by Yahweh. And he answered him Yahweh and he said arise go down Keilah for I [am] about to give [the] Philistines in hand your.
5 Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
And he went David (and men his *Q(K)*) Keilah and he fought against the Philistines and he drove away livestock their and he defeated them a defeat great and he delivered David [the] inhabitants of Keilah.
6 (Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
And it was when fled Abiathar [the] son of Ahimelech to David Keilah an ephod it came down in hand his.
7 Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
And it was told to Saul that he had gone David Keilah and he said Saul he has alienated him God in hand my for he has shut himself up by going in a city of doors and bar[s].
8 Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
And he summoned Saul all the people for battle to go down Keilah to lay siege against David and against men his.
9 Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
And he knew David that on him Saul [was] plotting evil and he said to Abiathar the priest bring near! the ephod.
10 Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
And he said David O Yahweh [the] God of Israel certainly he has heard servant your that [is] seeking Saul to come to Keilah to destroy the city because of me.
11 Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
¿ Will they deliver up me [the] citizens of Keilah in hand his ¿ will he come down Saul just as he has heard servant your O Yahweh [the] God of Israel tell please to servant your. And he said Yahweh he will come down.
12 Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
And he said David ¿ will they deliver up [the] citizens of Keilah me and men my in [the] hand of Saul and he said Yahweh they will deliver [you] up.
13 Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
And he arose David and men his about six hundred man and they went out from Keilah and they went about at where they went about and to Saul it was told that he had escaped David from Keilah and he ceased to go forth.
14 Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
And he dwelt David in the wilderness in the strongholds and he dwelt in the hill country in [the] wilderness of Ziph and he sought him Saul all the days and not he gave him God in hand his.
15 Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
And he saw David that he had come forth Saul to seek life his and David [was] in [the] wilderness of Ziph at Horesh.
16 Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
And he arose Jonathan [the] son of Saul and he went to David Horesh and he strengthened hand his in God.
17 Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
And he said to him may not you be afraid for not it will find you [the] hand of Saul father my and you you will reign over Israel and I I will become to you second in rank and also Saul father my [is] knowing [it is] thus.
18 Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
And they made [the] two of them a covenant before Yahweh and he remained David at Horesh and Jonathan he went to house his.
19 Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
And they went up Ziphites to Saul Gibeah towards saying ¿ not [is] David hiding himself with us in the strongholds at Horesh on [the] hill of Hakilah which [is] from [the] south of Jeshimon.
20 Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
And now to all [the] desire of self your O king to come down come down and [belongs] to us to deliver up him in [the] hand of the king.
21 Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
And he said Saul [be] blessed you by Yahweh for you have had compassion on me.
22 Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
Go please prepare still and know and see place his where it is foot his who? has he seen him there for someone has said to me certainly he is crafty he.
23 Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
And see and know from all the hiding places where he hides himself there and you will return to me to a certain [thing] and I will go with you and it will be if there he [is] in the land and I will search out him among all [the] thousands of Judah.
24 Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
And they arose and they went Ziph towards before Saul and David and men his [were] in [the] wilderness of Maon in the Arabah to [the] south of Jeshimon.
25 Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
And he went Saul and men his to seek [him] and people told to David and he went down the rock and he remained in [the] wilderness of Maon and he heard Saul and he pursued after David [the] wilderness of Maon.
26 Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
And he went Saul from [the] side of the mountain from this and David and men his [were] from [the] side of the mountain from this and he was David hurrying away to go from before Saul and Saul and men his [were] surrounding David and men his to catch them.
27 mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
And a messenger he came to Saul saying make haste! and come! for they have made a raid [the] Philistines on the land.
28 Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
And he turned back Saul from pursuing after David and he went to meet [the] Philistines there-fore people called the place that Sela Hammahlekoth.
29 Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.
And he went up David from there and he dwelt in [the] strongholds of En Gedi.