< 1 Samweli 23 >

1 Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
Da fik David at vide, at Filisterne belejrede Ke'ila og plyndrede Tærskepladserne.
2 akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
Og David rådspurgte HERREN: "Skal jeg drage hen og slå Filisterne der?" HERREN svarede David; "Drag hen og slå Filisterne og befri Ke'ila!"
3 Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
Men Davids Mænd sagde til ham: "Se, vi lever i stadig Frygt her i Juda; kan der så være Tale om, at vi skal drage til Ke'ila mod Filisternes Slagrækker?"
4 Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
Da rådspurgte David på ny HERREN, og HERREN svarede ham: "Drag ned til Ke'ila, thi jeg giver Filisterne i din Hånd!"
5 Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
David og hans Mænd drog da til Ke'ila, angreb Filisterne, bortførte deres Kvæg og tilføjede dem et stort Nederlag. Således befriede David Ke'ilas Indbyggere.
6 (Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
Dengang Ebjatar, Ahimeleks Søn, flygtede til David - han drog med David ned til Ke'ila - havde han Efoden med.
7 Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
Da Saul fik at vide, at David var kommet til Ke'ila, sagde han: "Gud har givet ham i min Hånd! Thi han lukkede sig selv inde, da han gik ind i en By med Porte og Slåer."
8 Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
Derfor stævnede Saul hele Folket sammen for at drage ned til Ke'ila og omringe David og hans Mænd.
9 Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
Da David hørte, at Saul pønsede på ondt imod ham, sagde han til Præsten Ebjatar: "Bring Efoden hid!"
10 Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
Derpå sagde David: "HERRE, Israels Gud! Din Tjener har hørt, at Saul har i Sinde at gå mod Ke'ila og ødelægge Byen for min Skyld.
11 Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
Vil Folkene i Ke'ila overgive mig i Sauls Hånd? Vil Saul drage herned, som din Tjener har hørt? HERRE, Israels Gud, kundgør din Tjener det!" HERREN svarede: "Ja, han vil!"
12 Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
Så spurgte David: "Vil Folkene i Ke'ila overgive mig og mine Mænd til Saul?" HERREN svarede: "Ja, de vil!"
13 Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
Da brød David op med sine Mænd, henved 600 i Tal, og de drog bort fra Ke'ila og flakkede om fra Sted til Sted. Men da Saul fik at vide, at David var sluppet bort fra Ke'ila, opgav han sit Togt.
14 Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
Nu opholdt David sig i Ørkenen på Klippehøjderne og i Bjergene i Zifs Ørken. Og Saul efterstræbte ham hele tiden, men Gud gav ham ikke i hans Hånd.
15 Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
Og David så, at Saul var draget ud for at stå ham efter Livet. Medens David var i Horesj i Zifs Ørken,
16 Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
begav Sauls Søn Jonatan sig til David i Horesj og styrkede hans Kraft i Gud,
17 Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
idet han sagde til ham: "Frygt ikke! Min Fader Sauls Arm skal ikke nå dig. Du bliver Konge over Israel og jeg den næste efter dig; det ved min Fader Saul også!"
18 Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
Derpå indgik de to en Pagt for HERRENs Åsyn, og David blev i Horesj, medens Jonatan drog hjem.
19 Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
Men nogle Zifiter gik op til Saul i Gibea og sagde: "David holder sig skjult hos os på Klippehøjderne ved Horesj i Gibeat-Hakila sønden for Jesjimon.
20 Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
Så kom nu herned, Konge, som du længe har ønsket; det skal da være vor Sag at overgive ham til Kongen!"
21 Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
Saul svarede: "HERREN velsigne eder, fordi l har Medfølelse med mig!
22 Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
Gå nu hen og pas fremdeles på og opspor, hvor han kommer hen på sin ilsomme Færd; thi man har sagt mig, at han er meget snu.
23 Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
Opspor alle de Skjulesteder, hvor han gemmer sig, og vend tilbage til mig med pålidelig Underretning; så vil jeg følge med eder, og hvis han er i Landet, skal jeg opsøge ham iblandt alle Judas Tusinder!"
24 Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
Da brød de op og drog forud for Saul til Zif. Men David var dengang med sine Mænd i Maons Ørken i Lavningen sønden for Jesjimon.
25 Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
Så drog Saul og hans Mænd ud for at opsøge ham, og da David kom under Vejr dermed, drog han ned til den Klippe, som ligger i Maons Ørken; men da det kom Saul for Øre, fulgte han efter David i Maons Ørken.
26 Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
Saul gik med sine Mænd på den ene Side af Bjerget, medens David med sine Mænd var på den anden, og David fik travlt med at slippe bort fra Saul. Men som Saul og hans Mænd var ved at omringe og gribe David og hans Mænd,
27 mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
kom der et Sendebud og sagde til Saul: "Skynd dig og kom! Filisterne har gjort Indfald i Landet!"
28 Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
Saul opgav da at forfølge David og drog mod Filisterne. Derfor kalder man det Sted Malekots Klippe.
29 Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.
Derpå drog David op til Klippehøjderne ved En-Gedi og opholdt sig der.

< 1 Samweli 23 >