< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
David fugiu de Naioth em Ramah, e veio e disse a Jonathan: “O que eu fiz? Qual é a minha iniqüidade? Qual é o meu pecado diante de seu pai, que ele procura a minha vida?”
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
Ele lhe disse: “Longe disso, você não morrerá”. Eis que meu pai não faz nada grande ou pequeno, mas que ele me revela isso. Por que meu pai esconderia isso de mim? Não é assim”.
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
David jurou além disso, e disse: “Seu pai sabe bem que encontrei favor em seus olhos; e ele diz: 'Não deixe Jonathan saber disso, para que ele não fique de luto'; mas verdadeiramente como Yahweh vive, e como sua alma vive, há apenas um passo entre mim e a morte”.
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
Então Jonathan disse a David: “O que quer que sua alma deseje, eu até o farei por você”.
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
David disse a Jonathan: “Eis que amanhã é a lua nova, e eu não deveria deixar de jantar com o rei; mas deixe-me ir, para que eu possa me esconder no campo até o terceiro dia à noite.
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
Se seu pai sentir minha falta, então diga: “David pediu-me encarecidamente que partisse para correr para Belém, sua cidade; pois lá é o sacrifício anual por toda a família”.
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
Se ele disser: 'Está bem', seu servo terá paz; mas se ele estiver com raiva, saiba que o mal é determinado por ele.
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
Portanto, lide amavelmente com seu servo, pois você trouxe seu servo a um pacto de Iavé com você; mas se há iniqüidade em mim, mate-me você mesmo, pois por que me levaria a seu pai?”.
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
Jonathan disse: “Longe de você, pois se eu soubesse que o mal estava determinado por meu pai a vir sobre você, eu não lhe diria isso?
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
Então David disse a Jonathan: “Quem me dirá se seu pai lhe responder de forma aproximada”?
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
Jonathan disse a David: “Venha! Vamos sair para o campo”. Ambos saíram para o campo.
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
Jonathan disse a David: “Por Javé, o Deus de Israel, quando amanhã a esta hora eu tiver sondado meu pai, ou no terceiro dia, eis que, se houver bondade para com David, não o enviarei então e o revelarei a você?
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
Yahweh faz isso a Jonathan e mais ainda, se agradar a meu pai fazer-te mal, se eu não te revelar e mandar-te embora, para que possas ir em paz. Que Yahweh esteja com você como esteve com meu pai.
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
Você não só me mostrará a bondade amorosa de Javé enquanto eu ainda viver, que eu não morra;
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
mas você também não cortará sua bondade de minha casa para sempre, não, não quando Javé tiver cortado todos os inimigos de Davi da superfície da terra”.
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
Então Jonathan fez um pacto com a casa de Davi, dizendo: “Yahweh o exigirá nas mãos dos inimigos de Davi”.
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
Jonathan fez David jurar novamente, pelo amor que tinha por ele; pois ele o amava como amava sua própria alma.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
Então Jonathan lhe disse: “Amanhã é a lua nova, e você sentirá sua falta, porque seu assento estará vazio”.
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
Quando tiver ficado três dias, desça rapidamente e venha para o lugar onde se escondeu quando isto começou, e permaneça junto à pedra Ezel.
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
Vou atirar três flechas de seu lado, como se atirasse em uma marca.
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
Eis que enviarei o menino, dizendo: 'Vá, encontre as flechas! Se eu disser ao rapaz: 'Eis que as flechas estão deste seu lado'. Tomai-as'; então venham, pois há paz para vocês e nenhum perigo, pois Yahweh vive.
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
Mas se eu disser isto ao menino: 'Eis que as flechas estão além de você', então siga seu caminho, pois Yahweh o mandou embora.
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
Quanto ao assunto de que você e eu falamos, eis que Yahweh está entre você e eu para sempre”.
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
Então, David se escondeu no campo. Quando a lua nova chegou, o rei se sentou para comer comida.
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
O rei sentou-se em seu assento, como em outras ocasiões, até mesmo no assento junto à parede; e Jonathan levantou-se, e Abner sentou-se ao lado de Saul, mas o lugar de Davi estava vazio.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
Mesmo assim, Saul não disse nada naquele dia, pois pensou: “Algo aconteceu com ele”. Ele não está limpo. Certamente ele não está limpo”.
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
No dia seguinte, após a lua nova, no segundo dia, a casa de David estava vazia. Saul disse a Jonathan seu filho: “Por que o filho de Jesse não veio comer, nem ontem, nem hoje”?
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
Jonathan respondeu a Saul: “David pediu-me sinceramente permissão para ir a Belém.
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
Ele disse: “Por favor, deixe-me ir, pois nossa família tem um sacrifício na cidade”. Meu irmão me ordenou que estivesse lá”. Agora, se eu encontrei favor em seus olhos, por favor, deixe-me ir embora e ver meus irmãos”. Portanto, ele não veio à mesa do rei”.
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
Então a raiva de Saul queimou contra Jonathan, e ele lhe disse: “Filho de uma mulher perversa e rebelde, não sei que você escolheu o filho de Jesse para sua vergonha e para a vergonha da nudez de sua mãe?
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
Enquanto o filho de Jessé viver na terra, você não será estabelecido, nem o seu reino. Portanto, agora enviai-o e trazei-o até mim, pois ele certamente morrerá”!
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
Jonathan respondeu a Saul, seu pai, e lhe disse: “Por que ele deveria ser condenado à morte? O que ele fez”?
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
Saul lançou-lhe sua lança para golpeá-lo. Por isto Jonathan sabia que seu pai estava determinado a matar David.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
Então Jonathan levantou-se da mesa com raiva feroz, e não comeu nada no segundo dia do mês; pois estava de luto por Davi, porque seu pai o havia tratado com vergonha.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
Pela manhã, Jonathan foi para o campo na hora marcada com David, e um garotinho com ele.
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
Ele disse a seu menino: “Corra, encontre agora as flechas que eu atiro”. Enquanto o garoto corria, ele atirou uma flecha além dele.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
Quando o menino chegou ao lugar da flecha que Jonathan tinha atirado, Jonathan chorou atrás do menino e disse: “A flecha não está além de você?
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
Jonathan chorou depois do garoto: “Vá rápido! Rápido! Não demore!” O menino de Jonathan juntou as flechas e veio até seu mestre.
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
Mas o garoto não sabia de nada. Somente Jonathan e David sabiam do assunto.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
Jonathan deu suas armas ao menino e lhe disse: “Vá, leve-as para a cidade”.
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
Assim que o menino se foi, David se levantou do sul, caiu de cara no chão e se curvou três vezes. Eles se beijaram e choraram um com o outro, e David foi o que mais chorou.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
Jonathan disse a David: “Vá em paz, porque ambos juramos em nome de Javé, dizendo: 'Javé está entre mim e você, e entre minha descendência e sua descendência, para sempre'”. Ele se levantou e partiu; e Jonathan foi para a cidade.

< 1 Samweli 20 >