< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
David s’enfuit de Naioth en Rama et, étant venu, il dit devant Jonathas: « Qu’ai-je fait? quel est mon crime, quel est mon péché devant ton père, pour qu’il en veuille à ma vie? »
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
Jonathas lui dit: « Loin de là! Tu ne mourras point. Mon père ne fait aucune chose, grande ou petite, sans m’en faire part; pourquoi donc me cacherait-il celle-là? Il n’en est rien. »
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
David répondit avec un serment: « Ton père sait bien que j’ai trouvé grâce à tes yeux, et il aura dit: Que Jonathas ne le sache pas, de peur qu’il en ait de la peine. Mais, aussi vrai que Yahweh est vivant et que ton âme est vivante! il n’y a qu’un pas entre la mort et moi. »
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
Jonathas dit à David: « Tout ce que ton âme dira, je le ferai pour toi. »
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
Et David dit à Jonathas: « Voici, c’est demain la nouvelle lune, et je devrais m’asseoir auprès du roi pour le repas; laisse-moi partir, et je me cacherai dans les champs jusqu’au soir du troisième jour.
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
Si ton père s’aperçoit de mon absence, tu lui diras: David m’a prié de lui laisser faire une course à Bethléem, sa ville, parce qu’il y a là le sacrifice annuel pour toute sa famille.
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
S’il dit: C’est bien! ton serviteur peut être en paix; mais s’il se met en colère, sache que le mal est bien résolu de sa part.
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
Use donc de bonté envers ton serviteur, puisque c’est par une alliance au nom de Yahweh que tu as attiré vers toi ton serviteur. S’il y a quelque faute en moi, mets-moi à mort toi-même, car pourquoi me mènerais-tu à ton père? »
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
Jonathas lui dit: « Loin de toi cette pensée! Car si j’apprends vraiment que le mal est résolu de la part de mon père pour venir sur toi, je jure de t’en informer. »
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
David dit à Jonathas: « Qui m’informera de cela ou de ce que ton père répondrait de fâcheux? »
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
Jonathas dit à David: « Viens, sortons dans les champs; » et ils sortirent tous deux dans les champs.
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
Jonathas dit à David: « Yahweh, Dieu d’Israël! Je sonderai mon père demain ou après-demain, et si cela va bien pour David, et que je n’envoie pas vers toi pour t’en informer,
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
que Yahweh traite Jonathas dans toute sa rigueur! S’il plaît à mon père de te faire du mal, je t’en informerai aussi et je te ferai partir, afin que tu t’en ailles en paix, et que Yahweh soit avec toi, comme il a été avec mon père!
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
Et si je suis encore vivant, veuille user envers moi de la bonté de Yahweh, et, si je meurs,
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
ne pas retirer à jamais ta bonté de ma maison, pas même lorsque Yahweh retranchera de dessus la face de la terre chacun des ennemis de David! »
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
C’est ainsi que Jonathas fit alliance avec la maison de David, et que Yahweh tira vengeance des ennemis de David.
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
Jonathas adjura encore une fois David par l’amour qu’il avait pour lui, car il l’aimait comme son âme.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
Jonathas lui dit: « C’est demain la nouvelle lune; on remarquera que ta place est vide.
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
Le troisième jour, tu descendras promptement et tu viendras au lieu où tu étais caché, au jour de l’affaire, et tu resteras près de la pierre d’Ezel.
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
Je tirerai trois flèches du côté de la pierre, comme si je visais à un but.
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
Et voici, j’enverrai le garçon en lui disant: Va, retrouve les flèches. Si je dis au garçon: Voici, les flèches sont en deçà toi, prends-les! alors, viens, car tout va bien pour toi, et il n’y a nul danger, Yahweh est vivant!
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
Mais si je parle ainsi au garçon: Voici, les flèches sont au delà de toi, alors va-t-en, car Yahweh te fait partir.
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
Et quant à la parole que nous avons dite, moi et toi, voici que Yahweh est à jamais entre toi et moi. »
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
David se cacha dans les champs. La nouvelle lune venue, le roi prit place au festin pour manger;
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
comme à l’ordinaire, le roi s’assit sur son siège, sur le siège qui était près du mur; Jonathas se leva, et Abner s’assit à côté de Saül et la place de David resta vide.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
Saül ne dit rien ce jour-là, car, disait-il, « quelque chose lui est arrivé; il n’est pas pur, certainement il n’est pas pur. »
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
Le lendemain, second jour de la nouvelle lune, la place de David était encore vide; et Saül dit à Jonathas, son fils: « Pourquoi le fils d’Isaï n’est-il pas venu au repas, ni hier ni aujourd’hui? »
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
Jonathas répondit à Saül: « David m’a demandé avec instances la permission d’aller jusqu’à Bethléem.
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
Il a dit: Laisse-moi aller, je te prie, car nous avons dans la ville un sacrifice de famille, et mon frère m’a commandé d’y assister; si donc j’ai trouvé grâce à tes yeux, permets que je m’y rende et que je voie mes frères! C’est pourquoi il n’est pas venu à la table du roi. »
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
Alors la colère de Saül s’enflamma contre Jonathas, et il lui dit: « Fils d’une femme perverse et rebelle, ne sais-je pas que tu as pour ami le fils d’Isaï, à ta honte et à la honte de la nudité de ta mère?
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
Car aussi longtemps que le fils d’Isaï sera vivant sur la terre, il n’y aura de sécurité ni pour toi, ni pour ta royauté. Et maintenant, envoie-le prendre et amène-le-moi, car c’est un fils de la mort. »
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
Jonathas répondit à Saül, son père, et lui dit: « Pourquoi serait-il mis à mort? Qu’a-t-il fait? »
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
Et Saül brandit sa lance contre lui pour le frapper. Jonathas comprit que c’était chose arrêtée chez son père de faire périr David.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
Jonathas se leva donc de table dans une violente colère, et ne prit pas de nourriture, le second jour de la nouvelle lune; car il était affligé à cause de David, parce que son père l’avait outragé.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
Le lendemain matin, Jonathas alla aux champs, selon qu’il était convenu avec David; un petit garçon l’accompagnait.
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
Il dit à son garçon: « Cours, retrouve les flèches que je vais tirer. » Le garçon courut, et Jonathas tira une flèche de manière à le dépasser.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
Lorsque le garçon arriva à l’endroit de la flèche que Jonathas avait tirée, Jonathas cria après le garçon et dit: « La flèche n’est-elle pas plus loin que toi? »
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
Jonathas cria encore après le garçon: « Vite, hâte-toi, ne t’arrête pas! » Et le garçon de Jonathas ramassa la flèche et revint vers son maître.
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
Le garçon ne savait rien; Jonathas et David seuls comprenaient la chose.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
Jonathas donna ses armes au garçon qui était avec lui, et lui dit: « Va, et portes-les à la ville. »
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
Dès que le garçon fut parti, David se leva du côté du midi et, se jetant la face contre terre, il se prosterna trois fois devant Jonathas; puis ils s’embrassèrent l’un l’autre et pleurèrent au sujet l’un de l’autre, au point que David fondit en larmes.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
Et Jonathas dit à David: « Va en paix, après que nous avons juré l’un et l’autre, au nom de Yahweh, en disant: Que Yahweh soit entre moi et toi, entre ma postérité et ta postérité à jamais! » David se leva et s’en alla, et Jonathas rentra dans la ville.

< 1 Samweli 20 >