< 1 Samweli 20 >
1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
And David flees from Naioth in Ramah, and comes, and says before Jonathan, “What have I done? What [is] my iniquity? And what [is] my sin before your father, that he is seeking my life?”
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
And he says to him, “Far be it! You do not die; behold, my father does not do anything great or small and does not uncover my ear; and why does my father hide this thing from me? This [thing] is not.”
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
And David swears again and says, “Your father has certainly known that I have found grace in your eyes, and he says, Do not let Jonathan know this, lest he is grieved; and yet, YHWH lives, and your soul lives, but—as a step between me and death.”
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
And Jonathan says to David, “What does your soul [desire]? Command and I do it for you.”
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
And David says to Jonathan, “Behold, the new moon [is] tomorrow; and I certainly sit with the king to eat; and you have sent me away, and I have been hidden in a field until the third evening;
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
if your father looks after me at all, then you have said, David earnestly asked of me to run to his city of Beth-Lehem, for there [is] a sacrifice of the days for all the family.
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
If thus he says: Good; [there is] peace for your servant; and if it is very displeasing to him—know that the evil has been determined by him;
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
and you have done kindness to your servant, for you have brought your servant into a covenant of YHWH with you—and if there is iniquity in me, put me to death yourself; for why [is] this [that] you bring me to your father?”
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
And Jonathan says, “Far be it from you! For I certainly do not know that the evil has been determined by my father to come on you, and I do not declare it to you.”
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
And David says to Jonathan, “Who declares [it] to me? Or what [if] your father answers you sharply?”
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
And Jonathan says to David, “Come, and we go out into the field”; and both of them go out into the field.
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
And Jonathan says to David, “YHWH, God of Israel, [is my witness]—when I search out my father about [this] time tomorrow [or] the third [day], and behold, [there is] good toward David, and I do not then send to you, and have uncovered your ear—
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
thus YHWH does to Jonathan, and thus He adds; when the evil concerning you is good to my father, then I have uncovered your ear, and sent you away, and you have gone in peace, and YHWH is with you, as he was with my father;
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
and not only while I am alive do you do the kindness of YHWH with me, and I do not die,
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
but you do not cut off your kindness from my house for all time, nor in YHWH’s cutting off the enemies of David, each one from off the face of the ground.”
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
So Jonathan cuts [a covenant] with the house of David, and YHWH has sought [it] from the hand of the enemies of David;
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
and Jonathan adds to cause David to swear, because he loves him, for he has loved him [as] the love [for] his own soul.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
And Jonathan says to him, “Tomorrow [is] the new moon, and you have been looked after, for your seat is looked after;
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
and on the third day you certainly come down, and have come to the place where you were hidden in the day of the work, and have remained near the stone of Ezel.
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
And I shoot three of the arrows at the side, sending out at a mark for myself;
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
and behold, I send the youth, [saying], Go, find the arrows. If I say to the youth at all, Behold, the arrows [are] on this side of you—take them and come, for [there is] peace for you, and there is no [adverse] word—[as] YHWH lives.
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
And if thus I say to the young man, Behold, the arrows [are] beyond you—go, for YHWH has sent you away;
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
as for the thing which you and I have spoken, behold, YHWH [is] between me and you for all time.”
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
And David is hidden in the field, and it is the new moon, and the king sits down by the food to eat,
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
and the king sits on his seat, as time by time, on a seat by the wall, and Jonathan rises, and Abner sits at the side of Saul, and David’s place is looked after.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
And Saul has not spoken anything on that day, for he said, “It [is] an accident; he is not clean—surely not clean.”
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
And it comes to pass on the second day of the new moon, that David’s place is looked after, and Saul says to his son Jonathan, “Why has the son of Jesse not come in, either yesterday or today, to the food?”
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
And Jonathan answers Saul, “David has earnestly asked [permission] from me [to go] to Beth-Lehem,
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
and he says, Please send me away, for we have a family sacrifice in the city, and my brother has given command to me himself, and now, if I have found grace in your eyes, please let me go away and see my brothers; therefore he has not come to the table of the king.”
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
And the anger of Saul burns against Jonathan, and he says to him, “Son of a perverse [woman] of rebellion! Have I not known that you are fixing on the son of Jesse to your own shame, and to the shame of the nakedness of your mother?
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
For all the days that the son of Jesse lives on the ground you are not established, you and your kingdom; and now, send and bring him to me, for he [is] a son of death.”
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
And Jonathan answers his father Saul and says to him, “Why is he put to death? What has he done?”
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
And Saul casts the javelin at him to strike him, and Jonathan knows that it has been determined by his father to put David to death.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
And Jonathan rises from the table in the heat of anger, and has not eaten food on the second day of the new moon, for he has been grieved for David, for his father put him to shame.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
And it comes to pass in the morning, that Jonathan goes out into the field for the appointment with David, and a little youth [is] with him.
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
And he says to his youth, “Now run, find the arrows which I am shooting”; the youth is running, and he has shot the arrow, causing [it] to pass over him.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
And the youth comes to the place of the arrow which Jonathan has shot, and Jonathan calls after the youth, and says, “Is the arrow not beyond you?”
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
And Jonathan calls after the youth, “Speed, hurry, do not stand”; and Jonathan’s youth gathers the arrows, and comes to his lord.
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
And the youth has not known anything, only Jonathan and David knew the word.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
And Jonathan gives his weapons to the youth whom he has and says to him, “Go, carry into the city.”
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
The youth has gone, and David has risen from Ezel, at the south, and falls on his face to the earth, and bows himself three times, and they kiss one another, and they weep with one another, until David exerted himself;
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
and Jonathan says to David, “Go in peace, in that we have sworn—the two of us—in the Name of YHWH, saying, YHWH is between me and you, and between my seed and your seed—for all time”; and he rises and goes; and Jonathan has gone into the city.