< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
And David fled from Naioth in Ramah, and came and said before Jonathan: 'What have I done? what is mine iniquity? and what is my sin before thy father, that he seeketh my life?'
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
And he said unto him: 'Far from it; thou shalt not die; behold, my father doeth nothing either great or small, but that he discloseth it unto me; and why should my father hide this thing from me? it is not so.'
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
And David swore moreover, and said: 'Thy father knoweth well that I have found favour in thine eyes; and he saith: Let not Jonathan know this, lest he be grieved; but truly as the LORD liveth, and as thy soul liveth, there is but a step between me and death.'
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
Then said Jonathan unto David: 'What doth thy soul desire, that I should do it for thee?'
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
And David said unto Jonathan: 'Behold, to-morrow is the new moon, when I should sit with the king to eat; so let me go, that I may hide myself in the field unto the third day at even.
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
If thy father miss me at all, then say: David earnestly asked leave of me that he might run to Beth-lehem his city; for it is the yearly sacrifice there for all the family.
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
If he say thus: It is well; thy servant shall have peace; but if he be wroth, then know that evil is determined by him.
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
Therefore deal kindly with thy servant; for thou hast brought thy servant into a covenant of the LORD with thee; but if there be in me iniquity, slay me thyself; for why shouldest thou bring me to thy father?'
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
And Jonathan said: 'Far be it from thee; for if I should at all know that evil were determined by my father to come upon thee, then would not I tell it thee?
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
Then said David to Jonathan: 'Who shall tell me if perchance thy father answer thee roughly?'
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
And Jonathan said unto David: 'Come and let us go out into the field.' And they went out both of them into the field.
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
And Jonathan said unto David: 'The LORD, the God of Israel — when I have sounded my father about this time to-morrow, or the third day, behold, if there be good toward David, shall I not then send unto thee, and disclose it unto thee?
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
The LORD do so to Jonathan, and more also, should it please my father to do thee evil, if I disclose it not unto thee, and send thee away, that thou mayest go in peace; and the LORD be with thee, as He hath been with my father.
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
And thou shalt not only while yet I live show me the kindness of the LORD, that I die not;
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
but also thou shalt not cut off thy kindness from my house for ever; no, not when the LORD hath cut off the enemies of David every one from the face of the earth.'
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
So Jonathan made a covenant with the house of David: 'The LORD even require it at the hand of David's enemies.'
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
And Jonathan caused David to swear again, for the love that he had to him; for he loved him as he loved his own soul.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
And Jonathan said unto him: 'To-morrow is the new moon; and thou wilt be missed, thy seat will be empty.
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
And in the third day thou shalt hide thyself well, and come to the place where thou didst hide thyself in the day of work, and shalt remain by the stone Ezel.
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
And I will shoot three arrows to the side-ward, as though I shot at a mark.
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
And, behold, I will send the lad: Go, find the arrows. If I say unto the lad: Behold, the arrows are on this side of thee; take them, and come; for there is peace to thee and no hurt, as the LORD liveth.
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
But if I say thus unto the boy: Behold, the arrows are beyond thee; go thy way; for the LORD hath sent thee away.
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
And as touching the matter which I and thou have spoken of, behold, the LORD is between me and thee for ever.'
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
So David hid himself in the field; and when the new moon was come, the king sat him down to the meal to eat.
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
And the king sat upon his seat, as at other times, even upon the seat by the wall; and Jonathan stood up, and Abner sat by Saul's side; but David's place was empty.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
Nevertheless Saul spoke not any thing that day; for he thought: 'Something hath befallen him, he is unclean; surely he is not clean.'
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
And it came to pass on the morrow after the new moon, which was the second day, that David's place was empty; and Saul said unto Jonathan his son: 'Wherefore cometh not the son of Jesse to the meal, neither yesterday, nor to-day?'
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
And Jonathan answered Saul: 'David earnestly asked leave of me to go to Beth-lehem;
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
and he said: Let me go, I pray thee; for our family hath a sacrifice in the city; and my brother, he hath commanded me; and now, if I have found favour in thine eyes, let me get away, I pray thee, and see my brethren. Therefore he is not come unto the king's table.'
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
Then Saul's anger was kindled against Jonathan, and he said unto him: 'Thou son of perverse rebellion, do not I know that thou hast chosen the son of Jesse to thine own shame, and unto the shame of thy mother's nakedness?
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
For as long as the son of Jesse liveth upon the earth, thou shalt not be established, nor thy kingdom. Wherefore now send and fetch him unto me, for he deserveth to die.'
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
And Jonathan answered Saul his father, and said unto him: 'Wherefore should he be put to death? what hath he done?'
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
And Saul cast his spear at him to smite him; whereby Jonathan knew that it was determined of his father to put David to death.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
So Jonathan arose from the table in fierce anger, and did eat no food the second day of the month; for he was grieved for David, and because his father had put him to shame.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
And it came to pass in the morning, that Jonathan went out into the field at the time appointed with David, and a little lad with him.
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
And he said unto his lad: 'Run, find now the arrows which I shoot.' And as the lad ran, he shot an arrow beyond him.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
And when the lad was come to the place of the arrow which Jonathan had shot, Jonathan cried after the lad, and said: 'Is not the arrow beyond thee?'
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
And Jonathan cried after the lad: 'Make speed, hasten, stay not.' And Jonathan's lad gathered up the arrows, and came to his master.
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
But the lad knew not any thing; only Jonathan and David knew the matter.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
And Jonathan gave his weapons unto his lad, and said unto him: 'Go, carry them to the city.'
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
And as soon as the lad was gone, David arose out of a place toward the South, and fell on his face to the ground, and bowed down three times; and they kissed one another, and wept one with another, until David exceeded.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
And Jonathan said to David: 'Go in peace, forasmuch as we have sworn both of us in the name of the LORD, saying: The LORD shall be between me and thee, and between my seed and thy seed, for ever.' And he arose and departed; and Jonathan went into the city.

< 1 Samweli 20 >