< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
But David fled from Najoth, which is in Ramatha, and came and said to Jonathan: What have I done? what is my iniquity, and what is my sin against thy father, that he seeketh my life?
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
And he said to him: God forbid, thou shalt not die: for my father will do nothing great or little, without first telling me: hath then my father hid this word only from me? no, this shall not be.
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
And he swore again to David. And David said: Thy father certainly knoweth that I have found grace in thy sight, and he will say: Let not Jonathan know this, lest he be grieved. But truly as the Lord liveth, and thy soul liveth, there is but one step (as I may say) between me and death.
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
And Jonathan said to David: Whatsoever thy soul shall say to me, I will do for thee.
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
And David said to Jonathan: Behold tomorrow is the new moon, and I according to custom am wont to sit beside the king to eat: let me go then that I may be hid in the field till the evening of the third day.
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
If thy father look and inquire for me, thou shalt answer him: David asked me that he might run to Bethlehem his own city: because there are solemn sacrifices there for all his tribe.
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
If he shall say, It is well: thy servant shall have peace: but if he be angry, know that his malice is come to its height.
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
Deal mercifully then with thy servant: for thou hast brought me thy servant into a covenant of the Lord with thee. But if there be any iniquity in me, do thou kill me, and bring me not in to thy father.
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
And Jonathan said: Far be this from thee: for if I should certainly know that evil is determined by my father against thee, I could do no otherwise than tell thee.
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
And David answered Jonathan: Who shall bring me word, if thy father should answer thee harshly concerning me?
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
And Jonathan said to David: Come and let us go out into the field. And when they were both of them gone out into the field,
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
Jonathan said to David: O Lord God of Israel, if I shall discover my father’s mind, tomorrow or the day after, and there be any thing good for David, and I send not immediately to thee, and make it known to thee,
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
May the Lord do so and so to Jonathan and add still more. But if my father shall continue in malice against thee, I will discover it to thy ear, and will send thee away, that thou mayest go in peace, and the Lord be with thee, as he hath been with my father.
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
And if I live, thou shalt shew me the kindness of the Lord: but if I die,
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
Thou shalt not take away thy kindness from my house for ever, when the Lord shall have rooted out the enemies of David, every one of them from the earth, may he take away Jonathan from his house, and may the Lord require it at the hands of David’s enemies.
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
Jonathan therefore made a covenant with the house of David: and the Lord required it at the hands of David’s enemies.
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
And Jonathan swore again to David, because he loved him: for he loved him as his own soul.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
And Jonathan said to him: Tomorrow is the new moon, and thou wilt be missed:
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
For thy seat will be empty till after tomorrow. So thou shalt go down quickly, and come to the place, where thou must be hid on the day when it is lawful to work, and thou shalt remain beside the stone, which is called Ezel.
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
And I will shoot three arrows near it, and will shoot as if I were exercising myself at a mark.
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
And I will send a boy, saying to him: Go and fetch me the arrows.
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
If I shall say to the boy: Behold the arrows are on this side of thee, take them up: come thou to me, because, there is peace to thee, and there is no evil, as the Lord liveth. But if I shall speak thus to the boy: Behold the arrows are beyond thee: go in peace, for the Lord hath sent thee away.
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
And concerning the word which I and thou have spoken, the Lord be between thee and me for ever.
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
So David was hid in the field, and the new moon came, and the king sat down to eat bread.
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
And when the king sat down upon his chair (according to custom) which was beside the wall, Jonathan arose, and Abner sat by Saul’s side, and David’s place appeared empty.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
And Saul said nothing that day, for he thought it might have happened to him, that he was not clean, nor purified.
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
And when the second day after the new moon was come, David’s place appeared empty again. And Saul said to Jonathan his son: Why cometh not the son of Isai to meat neither yesterday nor today?
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
And Jonathan answered Saul: He asked leave of me earnestly to go to Bethlehem,
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
And he said: Let me go, for there is a solemn sacrifice in the city, one of my brethren hath sent for me: and now if I have found favour in thy eyes, I will go quickly, and see my brethren. For this cause he came not to the king’s table.
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
Then Saul being angry against Jonathan said to him: Thou son of a woman that is the ravisher of a man, do I not know that thou lovest the son of Isai to thy own confusion and to the confusion of thy shameless mother?
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
For as long as the son of Isai liveth upon earth, thou shalt not be established, nor thy kingdom. Therefore now presently send, and fetch him to me: for he is the son of death.
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
And Jonathan answering Saul his father, said: Why shall he die: what hath he done?
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
And Saul caught up a spear to strike him. And Jonathan understood that it was determined by his father to kill David.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
So Jonathan rose from the table in great anger, and did not eat bread on the second day after the new moon. For he was grieved for David, because his father had put him to confusion.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
And when the morning came, Jonathan went into the field, according to the appointment with David, and a little boy with him.
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
And he said to his boy: Go, and fetch me the arrows which I shoot. And when the boy ran, he shot another arrow beyond the boy.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
The boy therefore came to the place of the arrow which Jonathan had shot: and Jonathan cried after the boy, and said: Behold the arrow is there further beyond thee.
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
And Jonathan cried again after the boy, saying: Make haste speedily, stand not. And Jonathan’s boy gathered up the arrows, and brought them to his master:
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
And he knew not at all what was doing: for only Jonathan and David knew the matter.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
Jonathan therefore gave his arms to the boy, and said to him: Go, and carry them into the city.
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
And when the boy was gone, David rose out of his place, which was towards the south, and falling on his face to the ground, adored thrice: and kissing one another, they wept together, but David more.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
And Jonathan said to David: Go in peace: and let all stand that we have sworn both of us in the name of the Lord, saying: The Lord be between me and thee, and between my seed and thy seed for ever. And David arose, and departed: and Jonathan went into the city.

< 1 Samweli 20 >