< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
Then David fled from Naioth, which is in Ramah, and he went and said before Jonathan: “What have I done? What is my iniquity, or what is my sin, against your father, so that he would seek my life?”
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
And he said to him: “May this not be! You shall not die. For my father will not do anything, great or small, without first revealing it to me. Therefore, has my father concealed this word solely from me? By no means shall this be!”
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
And he swore again to David. And David said: “Your father certainly knows that I have found favor in your sight, and so he will say, ‘Let Jonathan not know this, lest he be saddened.’ So truly, as the Lord lives, and as your soul lives, there is only one step (if I may say it) separating me from death.”
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
And Jonathan said to David, “Whatever your soul will tell me, I will do for you.”
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
Then David said to Jonathan: “Behold, tomorrow is the new moon, and I am accustomed to sit in a seat beside the king to eat. Therefore, permit me that I may be hidden in the field, until the evening of the third day.
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
If your father, looking around, will seek me, you shall respond to him: ‘David asked me if he may hurry to Bethlehem, his own city. For there are solemn sacrifices in that place for all of his tribe together.’
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
If he will say, ‘It is well,’ then your servant will have peace. But if he will be angry, know that his malice has reached its height.
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
Therefore, show mercy to your servant. For you have brought me, your servant, into a covenant of the Lord with you. But if there is any iniquity in me, you may kill me, and you shall not lead me in to your father.”
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
And Jonathan said: “May this be far from you. For certainly, if I ever realized that any wickedness was determined by my father against you, I would not be able to do anything other than report it to you.”
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
And David responded to Jonathan, “Who will repeat it to me, if your father may perhaps answer you harshly about me?”
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
And Jonathan said to David, “Come, and let us go out into the field.” And when they both had gone out into the field,
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
Jonathan said before David: “O Lord, God of Israel, if I will discover a decision by my father, tomorrow, or the day after, and if there will be anything good concerning David, and yet I do not immediately send to you and make it known to you,
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
may the Lord do these things to Jonathan, and may he add these other things. But if my father will have persevered in malice against you, I will reveal it to your ear, and I will send you away, so that you may go in peace, and so that the Lord may be with you, just as he was with my father.
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
And if I live, you shall show the mercy of the Lord to me. Yet truly, if I die,
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
you shall not take away your mercy from my house, even forever, when the Lord will have rooted out the enemies of David, each and every one of them, from the earth. May he take Jonathan from his house, and may the Lord require it from the hands of the enemies of David.”
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
Therefore, Jonathan formed a covenant with the house of David. And the Lord required it from the hands of the enemies of David.
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
And Jonathan continued to swear to David, because he loved him. For he loved him like his own soul.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
And Jonathan said to him: “Tomorrow is the new moon, and you will be sought.
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
For your seat will be empty until the day after tomorrow. Therefore, you shall descend quickly, and you shall go to the place where you are to be hidden, on a day when it is lawful to work, and you shall remain beside the stone that is called Ezel.
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
And I will shoot three arrows near it, and I will cast them as if I were practicing for myself toward a mark.
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
Also, I will send a boy, saying to him, ‘Go and bring the arrows to me.’
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
If I will say to the boy, ‘Behold, the arrows are before you, take them up,’ you shall approach before me, because there is peace for you, and there is nothing evil, as the Lord lives. But if I will have spoken to the boy in this way, ‘Behold, the arrows are away from you,’ then you shall go away in peace, for the Lord has released you.
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
Now about the word that you and I have spoken, may the Lord be between you and me, even forever.”
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
Therefore, David was hidden in the field. And the new moon came, and the king sat down to eat bread.
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
And when the king had sat down on his chair, (according to custom) which was beside the wall, Jonathan rose up, and Abner sat beside Saul, and David’s place appeared empty.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
And Saul did not say anything on that day. For he was thinking that perhaps something happened to him, so that he was not clean, or not purified.
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
And when the second day after the new moon had begun to dawn, David’s place again appeared empty. And Saul said to Jonathan, his son, “Why has the son of Jesse not arrived to eat, neither yesterday, nor today?”
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
And Jonathan responded to Saul, “He petitioned me earnestly that he might go to Bethlehem,
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
and he said: ‘Permit me. For there is a solemn sacrifice in the city. One of my brothers has summoned me. Now therefore, if I have found favor in your eyes, I will go quickly, and I will see my brothers.’ For this reason, he has not come to the table of the king.”
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
Then Saul, becoming angry against Jonathan, said to him: “You son of a woman wantonly seizing a man! Could I be ignorant that you love the son of Jesse, to your own shame, and to the shame of your disgraceful mother?
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
For all the days that the son of Jesse moves upon earth, neither you, nor your kingdom, will be secure. And so, send and bring him to me, here and now. For he is a son of death.”
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
Then Jonathan, answering his father Saul, said: “Why should he die? What has he done?”
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
And Saul picked up a lance, so that he might strike him. And Jonathan understood that it had been decided by his father that David be put to death.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
Therefore, Jonathan rose up from the table in a rage of anger. And he did not eat bread on the second day after the new moon. For he was saddened over David, because his father had confounded him.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
And when the morning had begun to dawn, Jonathan went into the field according to the agreement with David, and a young boy was with him.
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
And he said to his boy, “Go, and bring to me the arrows that I shoot.” And when the boy had run, he shot another arrow away from the boy.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
And so, the boy went to the place of the arrow which Jonathan had shot. And Jonathan cried out, from behind the back of boy, and said: “Behold, the arrow is there, farther away from you.”
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
And Jonathan cried out again, from behind the back of the boy, saying, “Go quickly! Do not stand still!” Then Jonathan’s boy collected the arrows, and he brought them to his lord.
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
And he did not understand at all what was happening. For only Jonathan and David knew the matter.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
Then Jonathan gave his weapons to the boy, and he said to him, “Go, and carry them into the city.”
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
And when the boy had gone away, David rose up from his place, which turned toward the south, and falling prone on the ground, he reverenced three times. And kissing one another, they wept together, but David more so.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
Then Jonathan said to David: “Go in peace. And let us both keep all that we have ever sworn in the name of the Lord, saying, ‘May the Lord be between me and you, and between my offspring and your offspring, even forever.’” And David rose up and went away. But Jonathan entered into the city.

< 1 Samweli 20 >