< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
David pobježe iz Najota u Rami i dođe k Jonatanu te mu reče: “Što sam učinio? Kakva je bila moja krivica i što sam zgriješio tvome ocu da traži moj život?”
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
A on mu odgovori: “Daleko od tebe ta misao! Ti nećeš poginuti. Eto, moj otac ne poduzima ništa, bilo veliko ili ne bilo, a da to meni ne otkrije. Zašto bi, dakle, moj otac krio od mene upravo to? Neće to biti!”
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
Ali se David zakle i reče: “Tvoj otac dobro zna da sam ja stekao tvoju naklonost, pa misli: 'Ne treba da Jonatan išta zna o tome, da ne bude žalostan.' Ali živoga mi Jahve i života mi tvoga, ima samo jedan korak između mene i smrti.”
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
Tada Jonatan upita Davida: “Što želiš da učinim za tebe?”
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
A David odgovori Jonatanu: “Evo, sutra je mladi mjesec i ja bih morao jesti s kraljem za stolom; ali me ti pusti da odem, da se sakrijem u polju do večera.
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
Ako tvoj otac opazi da me nema, reći ćeš mu ovako: 'David me uporno molio da ga pustim da skokne u svoj grad Betlehem, jer se ondje slavi godišnja žrtva za svu njegovu obitelj.'
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
Ako on rekne: 'Dobro!', tvoj je sluga spašen. Ako li plane gnjevom, znaj da je čvrsto naumio da me pogubi.
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
Iskaži, dakle, milost svome sluzi kad si slugu svoga uveo sa sobom u savez Jahvin. Ali ako ima kakva krivica na meni, ubij me sam; zašto bi me vodio k svome ocu?”
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
A Jonatan mu odgovori: “Daleko od tebe ta misao! Kad bih ja pouzdano znao da je moj otac čvrsto naumio da na tebe svali nesreću, zar ti ja ne bih dojavio?”
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
David upita Jonatana: “A tko će mi javiti ako ti tvoj otac odgovori što zlo?”
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
Jonatan odgovori Davidu: “Hodi, izađimo u polje!” I izađu obojica u polje.
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
Tada Jonatan reče Davidu: “Jahve, Bog Izraelov, neka mi bude svjedok! Ja ću iskušati svoga oca sutra u ovo doba. Ako bude dobro po Davida, a ja ne pošaljem k tebi da te obavijestim,
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
neka Jahve učini to zlo Jonatanu i neka mu doda drugo zlo! Ako li mome ocu bude drago da ti učini zlo, javit ću ti i pustit ću te da odeš u miru; i Jahve neka bude s tobom kao što je bio s mojim ocem!
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
Ako ja još budem živ, moći ćeš mi iskazati milosrđe Jahvino; ako li umrem,
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
ne uskrati svoje dobrote mome domu dovijeka! Kad Jahve redom iskorijeni Davidove neprijatelje s lica zemlje,
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
neka ime Jonatanovo ne iščezne s domom Šaulovim, inače će Jahve tražiti o tome račun od Davida.”
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
Tada se Jonatan još jednom zakune Davidu ljubavlju svojom, jer ga je ljubio svom ljubavlju duše svoje.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
Potom reče Jonatan Davidu: “Sutra je mladi mjesec i opazit će se da te nema, jer će tvoje mjesto biti prazno.
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
Prekosutra će se još očitije vidjeti da te nema, a ti dođi na mjesto gdje si se bio sakrio u dan onoga događaja i sjedni kraj onoga humka što ga znaš.
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
A ja ću prekosutra izmetati strijele na onu stranu kao da gađam onamo.
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
A onda ću poslati momka i reći mu: 'Idi! Nađi strijelu!' Ako onda doviknem momku: 'Pazi, strijela je ovamo bliže od tebe, donesi je!' - ti onda dođi, jer je za tebe dobro i nema nikakve opasnosti, tako mi Jahve živoga!
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
Ako li doviknem momku: 'Pazi, strijela je onamo dalje od tebe!' - ti onda otiđi, jer te Jahve šalje odavde.
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
A za ovaj dogovor što smo ga ugovorili ja i ti neka je Jahve svjedok između mene i tebe dovijeka!”
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
Potom se David sakri u polju. Kad je došao mlađak, kralj je sjeo za stol da jede.
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
Kralj sjede na svoje obično mjesto, na mjesto uza zid, Jonatan se smjesti sučelice njemu, Abner sjede kraj Šaula, a Davidovo mjesto osta prazno.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
Ali Šaul ne reče ništa onaj dan jer mišljaše: “Dogodilo mu se štogod, bit će da nije čist.”
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
Sutradan iza mladog mjeseca, drugi dan u mjesecu, opet Davidovo mjesto osta prazno, i Šaul upita svoga sina Jonatana: “Zašto Jišajev sin nije došao na objed ni jučer ni danas?”
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
A Jonatan odgovori Šaulu: “David me uporno molio da ga pustim da ide u Betlehem.
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
Rekao mi je: 'Pusti me da idem jer slavimo obiteljsku žrtvu u mom gradu i moja su me braća pozvala da dođem. Ako sam, dakle, stekao tvoju naklonost, daj mi dopust da pohodim svoju braću.' Eto, zato ga nema kod kraljeva stola.”
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
Tada Šaul planu gnjevom na Jonatana i reče mu: “Izrode i propalico! Misliš da ne znam da si u savezu s Jišajevim sinom, na sramotu svoju i na sramotu majčinu krilu!
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
Jer dokle god bude živ na zemlji Jišajev sin, nećeš biti siguran ni ti ni tvoje kraljevstvo. Zato sad pošalji po njega i dovedi ga k meni jer je osuđen na smrt.”
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
A Jonatan odvrati svome ocu Šaulu i reče mu: “Zašto on mora umrijeti? Što je učinio?”
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
Tada Šaul izmetnu koplje na sina da ga probode. Jonatan vidje da je njegov otac odlučio da ubije Davida.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
Jonatan ustade od stola sav jarostan i nije jeo ništa toga drugog dana u mjesecu jer se zabrinuo za Davida što ga je njegov otac pogrdio.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
Sutradan ujutro izađe Jonatan u polje prema dogovoru s Davidom; s njim je išao mlad momak.
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
I on reče svome momku: “Ti ćeš otrčati i naći strijele koje ću sada izmetnuti.” I momak otrča, a Jonatan odape strijelu tako da je preletjela preko njega.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
Kad je momak došao do mjesta gdje je bila strijela koju je izbacio Jonatan, viknu Jonatan za momkom: “Nije li strijela onamo dalje od tebe?”
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
Još Jonatan viknu za momkom: “Brže! Požuri se! Ne stoj!” Jonatanov momak diže strijelu i donese je svome gospodaru.
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
Momak nije ništa opazio, samo su Jonatan i David znali o čemu se radi.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
Nato Jonatan preda oružje momku i reče mu: “Idi i odnesi to u grad!”
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
Kad je momak otišao, David iziđe iza humka, pade ničice na zemlju i pokloni se tri puta. Potom se izljubiše i plakahu zajedno dok se nisu isplakali.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
Zatim Jonatan reče Davidu: “Idi u miru! Što smo se obojica zakleli Jahvinim imenom, neka Jahve bude svjedok između mene i tebe, između moga potomstva i tvoga potomstva dovijeka!” Nato David usta i ode, a Jonatan se vrati u grad.

< 1 Samweli 20 >